Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri Nishati, Judithi Kapinga leo Julai 19, 2024 akiwa katika ziara ya kikazi katika Vijiji vya Lubonde na Maweni wilayani Ludewa mkoani Njombe.
Kapinga amebainisha kuwa, nia ya Serikali ya Awamu ya Sita ni kuhakikisha wananchi wanapata maendeleo na kuongeza kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na wazalishaji binafsi wa umeme nchini.
Akizungumzia usambazaji wa umeme vijijini, Kapinga amesema kuwa Vijiji 151 tu nchi nzima bado havijafikiwa na huduma ya umeme kati ya Vijiji zaidi ya 12,000 na wilayani Ludewa vimebaki Vijiji nane.
Aidha, amemuagiza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kumsimamia Mkandarasi anayetekeleza miradi ya umeme Ludewa ili akamilishe kazi kwa wakati katika Vijiji nane vilivyobaki kati ya Vijiji ishirini vilivyopo Wilayani Ludewa.
Amesisitiza kuwa lengo la Serikali ni kuendelea kuzalisha umeme mwingi zaidi kutokana na mahitaji kuongezeka kila siku lakini pia uwepo wa miradi inayopeleka umeme nje ya Tanzania.
Awali, Mwenyekiti wa Bodi wa Kampuni ya Madope Padri Innocent Ngailo amesema Kanisa Katoliki Njombe liliiandikia Serikali barua ya kuomba TANESCO ipokee miundombinu ya umeme inayomilikiwa na Madope na kushukuru kwa Serikali kwa kuitikia ombi hilo.
Padri Innocent Ngailo amebainisha kuwa, Kampuni ya Madope yenyewe itabaki na kazi ya kuzalisha umeme ambao itaiuzia TANESCO.
Kwa upande wake Meneja wa TANESCO Mkoa wa Njombe, Abdulrahaman Nyenye amewaahidi wananchi wa Vijiji hivyo kuwa TANESCO itafika kutoa elimu na kuwatahadharisha kujiepusha na vishoka.
Mhandisi Nyenye ameongeza kuwa, takribani Vijiji ishirini vilivyokuwa vinahudumiwa na Kampuni ya Madope vitahudumiwa na TANESCO.
Mradi wa madope unamilikiwa na Kanisa Katoliki asilimia 55, Halmashauri ya Ludewa asilimia 45 na Jumuia ya Watumiaji Umeme Mawengi (JUWUMA) asilimia 5