Kampuni, taasisi au mradi unaoongozwa na waswahili lazima kuwe na ubabaishaji mkubwa!Simba si timu ya kushindwa kulipa wachezaji bonus!

Cashman

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2018
Posts
3,017
Reaction score
5,294
Nani alitulaani sisi watu weusi? Kwanini tunaendekeza ushenzi wakati mwingine bila sababu za msingi?

Neno 'ushenzi' ni kinyume cha neno ustaarabu.Tumeshindwa kuwa wastaarabu katika vitu vilivyo ndani ya uwezo wetu kwa maksudi tu.

Nimesikitishwa na madai kwamba eti ni kawaida kwa kampuni za kibiashara kulimbikiza madai ya watumishi na mara wapatapo huyalipa yote ndio sababu wachezaji wa Simba wanadai na kwamba watalipwa mara pesa inapopatikana!

Mi nasema huu ni uhuni ulio wazi.Lipeni madai ya watu kwa wakati.Kama hamna uwezo jitoeni kwenye kutengeneza madeni pasipo sababu.

Nasema ni uhuni kwa sababu ni nyie nyie Simba mlikataa udhamini wa Azam kwa kujifanya wajuaji eti hela kidogo.Kama ndivyo kwa nini mnachelewa kulipa wachezaji?

Msemaji anaposema Azam wamewazidi ubora,anazungumzia ubora upi?

Wakati mnawafunga yanga ubora wenu ulikuwaje?Au basi wakati mnawafunga Wydad ubora wenu ulikuwaje hadi mje kwa Azam na kusema mnazidiwa ubora na Azam?

Sisi nywele ngumu tuna shida gani hadi tuwe na ushenzi wa kila namna?
 
na hela za caf walikuwa wanatupigia mahesabu meengi mala wanapokea nyingi kuliko yanga .....
 
Nasikia zile peaa za udhamini wa m bet bado zipo kwenye ile tisheti 😅👈...

Timu kubwa afirika hii
 
na hela za caf walikuwa wanatupigia mahesabu meengi mala wanapokea nyingi kuliko yanga .....
Alafu posho zinawashinda mda huo huo unategemea atafanya overhaul ya kikosi kama tu posho ni kizungumkuti
 
Juzi niliuliza swali naona leo Ahmed Ally ameshajibu. Ukiangalia Simba ilivyoipress Yanga iliyokamilika mpaka ikapoteana, halafu ikaipeleka puta Wydad Dar na Moroco mpaka wakachomokea kwenye matuta. Halafu iangalie Simba jinsi ilivyocheza na Azam. Wachezaji walikuwa hawana morali kabisa. Chama sio wa kukosa utulivu ndani ya boksi. Kanoute pamoja na upuuzi wake wa kucheza rafu za hovyo lakini ile ya juzi ana kadi ya njano tayari halafu anaenda kumfyeka mcheza wa Azam mara tatu wakati refa kashapuliza kipenga moja kwa moja unaona wachezaji walikuwa na msongo wa mawazo baada ya kupewa ahadi hewa.

Pamoja na kuwa mshahara ni muhimu kuliko bonasi/posho lakini wachezaji ni kama watoto tu. Ukiwaahidi wape chao mapema. Kulikuwa na umuhimu gani kutoa ahadi ambayo haiwezi kutimizwa? Siku nyingine awe mwekezaji au viongozi msitoe ahadi kwa wachezaji kama hamna pesa za kutimiza hiyo ahadi.
 
Utajiri wa Mo una walakini Sana tajiri namba 1 Tanzania anashindwaje kulipa bonus za million 300?

Simba ludisheni timu kwa wanachama Mo anawaliza ile bilioni 20 iko wapi? Bilion 2 ya ujenzi wa uwanja bunju iko wapi?

Jamaa ni tapeli tuache siasa kwenye mpira.
 
Huko Simba ni mbali sana
Nenda kwenye hizi stand mpya zilizojengwa karibuni katazame vyoo vilivyo na hali mbaya ndiyo ujue sisi ni nani
Nenda kwenye masoko mapya yaliyojengwa hivi karibuni katazame hali ilivyo vyooni utatuelewa waswahili
Nensa kwenye viwanja vya ndege kadhalika utajiuliza kwanini mchawi wetu ametukimbia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…