Kampuni ya Adani na yakata usambazaji wa umeme Bangladesh kufuatia deni la dola milioni 800

Kampuni ya Adani na yakata usambazaji wa umeme Bangladesh kufuatia deni la dola milioni 800

Damaso

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2018
Posts
3,978
Reaction score
6,739
Bangladesh inakusanya malipo ya kampuni ya umeme ya Adani baada ya kampuni hiyo ya India kukata usambazaji wa umeme, huku ikiripotiwa kuwa ni kutokana na malipo ambayo hayajalipwa ya dollar $800m.

Maafisa wawili wakuu wa serikali waliiambia BBC kuwa tayari wanashughulikia baadhi ya malipo ya kampuni ya Adani, ambayo hutoa 10% ya umeme unaotumiwa na Bangladesh.

"Tumeshughulikia matatizo ya malipo na tayari tumetoa mkopo wa $170 milioni [£143m] kwa kampuni ya Adani," afisa mkuu wa Bodi ya Umeme ya Bangladesh aliambia BBC.

Kampuni ya Adani huipatia Bangladesh nguvu za umeme kutoka kwa kiwanda chake cha megawati 1600 kinachotumia makaa ya mawe mashariki mwa India.

Hata hivyo, kampuni hiyo haijajibu maswali ya BBC kuhusu kupunguzwa kwa usambazaji wa umeme kwa Bangladesh, ambayo inakabiliwa na uhaba wa umeme mara kwa mara.

Maafisa wanasema kampuni hiyo imetishia kusitisha usambazaji kabisa ikiwa pesa inayodai haitaikuwa imelipwa kikamilifu kufikia tarehe 7 Novemba.

images (33).jpeg

Karibu sana Tanzania Adani tumesimuliwa mambo mazuri na viongozi pamoja na wanasiasa. Ila kama tu Bangladesh wameanza kuumia sijui Tanzania tunasubiria nini?

Soma: Adani Group kutumia Tsh. Trilioni 2.4 kuwekeza kwenye Umeme Tanzania
 
Sio ndio hawa wamechukua uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta Kenya
 
Watanzania huyu mtu ni international conman (tapeli)! Uki Google tu jina lake au kampuni zake utaona utapeli wake nchi mbalimbali. Uswis, mpaka alifungiwa akaunti zake. Halafu mnamwachia Kafulila adili nae... Naona kesi ya matrillion yakulipa fidia ikija!:BanHammer:
 
Watanzania huyu mtu ni international conman (tapeli)! Uki Google tu jina lake au kampuni zake utaona utapeli wake nchi mbalimbali. Uswis, mpaka alifungiwa akaunti zake. Halafu mnamwachia Kafulila adili nae... Naona kesi ya matrillion yakulipa fidia ikija!:BanHammer:
Kafulila anatuambia kuwa ni mhindi wa tofauti
 
Adani Ports & SEZ (APSEZ) signed a 30-year concession agreement with the Tanzania Ports Authority to operate the Dar es Salaam container terminal. The Adani Ports-led consortium, East Africa Gateway Ltd. (EAGL), acquired the project company in Tanzania for $39.5 million. The port is important for trade and economic activity in the region, handling about 83% of Tanzania's total container volumes in 2023.
 
  • Mshangao
Reactions: Zed
Kampuni inayomilikiwa na Gautam Adani ilipunguza usambazaji wa umeme kwa Bangladesh hadi MW 700-800 mwezi huu, ikiwa ni zaidi nusu ya uzishaji wa umeme wa hapo awali, baada ya kushindwa kupata malipo yake ya $846 milioni.
 
Watanzania huyu mtu ni international conman (tapeli)! Uki Google tu jina lake au kampuni zake utaona utapeli wake nchi mbalimbali. Uswis, mpaka alifungiwa akaunti zake. Halafu mnamwachia Kafulila adili nae... Naona kesi ya matrillion yakulipa fidia ikija!:BanHammer:
Viongozi weru wanachojali ni ten percent zao hayo mengine sio shida zao.
 
Viongozi weru wanachojali ni ten percent zao hayo mengine sio shida zao.
Sijui viongozi tumewakosea wapi!? Yaani Khanji akitupiga kina Kafulila hii laana itawatafuna mpaka kesho
 
Back
Top Bottom