Kampuni ya Bakhresa inajishusha hadhi

kasindaga

Senior Member
Joined
Sep 6, 2013
Posts
165
Reaction score
165
Kweli Kampuni hii imejipambanua katika kuzalisha vyakula kwa matumizi ya binadamu ulimwenguni.Wakati nikiwa Uholanzi/Amsterdam niliweza kukutana na bidhaa km unga, biscuits nk zenye nembo ya Azam/Bakhresa Tz.Nilifurahi na kupongeza juhudi za mwekezaji mzawa.

Tofauti na nilivyotarajia kuona nikiwa hapa Tanzania ni kuona usafirishaji, upokeaji na uhifadhi wa malighafi ya matunda km maembe, machungwa nanasi, ukwaju nk hapo Kiwandani Mwandege Wilaya ya Mkuranga.

Shehena za matunda zinaozea kwenye magari yangojeao kuingia ndani. Harufu mbaya, mainzi, mafunza yametapakaa. Yanatia kinyaa sana. Hali hii inahatarisha afya za walaji. Kwa machache boredsha huduma zenu
 


Unaona wanyarwanda hao wasafi hatari na bidhaa zao bora juice ya embe sio nzito kama matope mfano wa ile ya azam hao inyange bidhaa zao ni bora Tanzania hatuwafikii
 
Azam ni dubwana Fulani hivi kubwa,mnahangaika sana
 
Watanganyika na ujuha wa kutukuza vya nje,Rwanda pa kulima mahindi hawana,hayo maembe,machungwa na mananasi wanatoa wapi!?

Kalia ujinga wako huohuo nenda kaangalie mashamba ya matunda huko ujifunze
 




Au wakajifunze kwa kasapreko wa Ghana wana chain ya vinywaji vingi kuanzia maji, juice, soda, wine za aina nyingi ikiwamo za kahawa na mabibo ya korosho na wanauza vinywaji vyao hadi ulaya na mazingira yao bora na vinywaji vyao ni viwango vya juu hata pombe kali wanazo nzuri sana
 
Matunda yanaozea getini na kwenye Gari Kwa sababu hawajiongezi kupewa kupaumbele cha kupakua matunda.

Bongo nyoso... Mtu hajali biashara yako... Anajali mgao wake.
 
Hivi nyinyi so ndo mlikuja humu mkasema kuwa juisi ya embe ya Azam sio matunda halisi?
Tena sasa hivi mmegeuza imekuwa juisi ya Azam ina tengenezwa na maembe yaliyo oza.
Wabongo buana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…