Kampuni ya China kuendesha miradi ya Mchuchuma, Liganga

MPadmire

JF-Expert Member
Joined
Mar 7, 2006
Posts
3,957
Reaction score
3,245
:: IPPMEDIA April 12.

Haya mkataba mwingine huo... Wabunge wa Upinzani chunguzeni na wazalendo mliopo wizarani huko mtupe habari kama kuna uzembe au harufu ya 10%

Ni vizuri mikataba ijayo iangaliwe sana ili tusipoteze rasilimali za taifa.

Ni muhimu rasilimali za watanzania ziwanufaishe watanzania, hasa faida imfikie mtanzania mmoja mmoja.

Inabidi tujue serikali ina share kiasi gani?

Serikali itapata gawio la faida na mrahaba kwa kiasi gani?

umeme utauzwa kwa gani??

Huo umeme utapungua bei au kuongezeka?

Makaa ya mawe, pamoja na kuzalisha umeme, je excess inaweza kutumika majumbani?

Ili kupunguza athari katika ukataji wa miti na kuangamiza misitu yetu ya asili, inabidi huo mkaa pia utengenezwe ili utumike majumbani pia.

Unajua hizi kampeni za kupanda miti kila mwaka sijui zinazingatia au wanajua tofauti kati ya indigineous trees and exotic trees.

Misitu yetu ya asili (indigineous) ndo muhimu katika kutunza mazingira yetu zaidi. Na mkaa mzuri au kuni bora zinatokana na miti ya asili.

Hata mbao bora za furniture na milango ni za miti ya asili.

Je hizo kampeni za upandaji miti, wanapanda miti gani??

Hivyo nashauri umeme utakaozalishwa uwe bei rahisi sana ili watanzania waepuka kukata miti. Na pia mkaa wa mawe utumike domestic.

Nime unganisha umuhimu wa mkaa wa mawe,umeme na mazingira Tanzania.
 
Kwahiyo unaungamkono wachina waendeshe liganga na mchuchuma ilimradi umeme upungue bei na makaa ya mawe yapatikane kwa matumizi ya nyumbani ili kupunguza ukataji miti- thanks for this.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…