Kampuni ya kuagiza magari ya Orbit imekwenda kinyume na makubaliano yetu katika ununuzi wa gari

Kampuni ya kuagiza magari ya Orbit imekwenda kinyume na makubaliano yetu katika ununuzi wa gari

Kiroho Safii

Member
Joined
Aug 15, 2015
Posts
24
Reaction score
53
IMG_1124.jpeg


Hii ni kampuni inaitwa Orbit Group Limited (Orbit tz) inayoagiza magari kutoka nje ya nchi. Biashara hio inahusisha pia kutoa mkopo wa mpaka miaka miwili ili kukamilisha gharama ya gari.

Sasa hawa watu, kuna taarifa wanamficha mteja na wanakuja kukwambia baadae sana ambapo pengine unaweza kufikia uamuzi wa kutolichukua kabisa gari, na huku umeshatanguliza hela ya mwanzo, na ndio hapo matatizo.

Mfano, kuna ishu ilitokea (gari liliagizwa na kufika nchini) ambapo kwa makubaliano ya mwanzo, riba ya mkopo wa gari ilitakiwa iwe asilimia 3 kwa mwezi, kwa mkopo wa milioni 11, mchanganuo waliotoa ni kama huo hapo chini
d9b38368-e382-419e-8564-ff6a0981677e.jpeg

Ambapo kwa mwezi ningetakiwa nilipe 650,000 tsh. Lakini, gari lilivofika nchini, wakanitaarifu kua riba imebadilika na kua asilimia 4.5 kwa mwezi, wakanipa mchanganuo mpya ambapo ningetakiwa nilipe 830,000 tsh kwa mwezi.

bbb98c31-23fd-41d8-be86-f11b2686ea5f.jpeg

Ukiachilia mbali mabadiliko hayo, taarifa nyingine ni kwamba mkopo ule una gharama yake na pia gari inatakiwa ilipiwe premium, ambayo ikawa kama milioni 1.3 nyingine kutoka mfukoni.
IMG_1127.jpeg


Baada ya kufikia uamuzi wa kukataa mabadiliko haya na kuomba hela niliyolipa awali irudi, ndipo wakaanza kuzunguka. Mara wanasema mpaka gari iuzwe ndio walipe.

Na pia zaidi ya hapo. Wakaendelea kusema kwenye ile hela ya awali. Watakata gharama yao ya kuagiza gari.

Ingawa nilikubaliana na yote hayo. Bado wameendelea kuzunguka na mpaka hivi sasa kuna kesi ya madai inaendelea mahakamaini kurudisha hio hela.

Hivyo huu uzi uwe ni tahadhari kwa mtu ambae yuko kwenye hatua ya kutaka kufanya biashara na hawa jamaa. Jua kwamba sio waaminifu.

Na huu uzi sio kwamba ninaandika kuharibia biashara, hapana. Hii hapa ni screenshot ya chat na namba yao, ambayo pia wameeka kwenye ukurasa wao wa Instagram.

IMG_1128.png
 
Aiseee pole sana, hao jamaa usiwalazie damu ni matapeli live. Kama mlishasaini halafu wakaja kubadilisha angani una haki ya kurudishiwa hela yako uliyolipa na pasipo makato ya aina yeyote maana wao ndiyo waliokiuka masharti.
 
Inakuaje mnaingia kingi Kwa watu wasio na mtaji hata kidogo, watafute wenye showroom nunua gari, au ingia nao mkataba wakuagizie gari, hapo utakua salama lakini hawa wa vijiofisi uchwara wasio na mtaji ni madalali wanaonuka umaskini na utapeli.
 
View attachment 3056960

Hii ni kampuni inayoagiza magari kutoka nje ya nchi. Biashara hio inahusisha pia kutoa mkopo wa mpaka miaka miwili ili kukamilisha gharama ya gari.

Sasa hawa watu, kuna taarifa wanamficha mteja na wanakuja kukwambia baadae sana ambapo pengine unaweza kufikia uamuzi wa kutolichukua kabisa gari, na huku umeshatanguliza hela ya mwanzo, na ndio hapo matatizo.

Mfano, kuna ishu ilitokea (gari liliagizwa na kufika nchini) ambapo kwa makubaliano ya mwanzo, riba ya mkopo wa gari ilitakiwa iwe asilimia 3 kwa mwezi, kwa mkopo wa milioni 11, mchanganuo waliotoa ni kama huo hapo chini
View attachment 3056964
Ambapo kwa mwezi ningetakiwa nilipe 650,000 tsh. Lakini, gari lilivofika nchini, wakanitaarifu kua riba imebadilika na kua asilimia 4.5 kwa mwezi, wakanipa mchanganuo mpya ambapo ningetakiwa nilipe 830,000 tsh kwa mwezi.

View attachment 3056965
Ukiachilia mbali mabadiliko hayo, taarifa nyingine ni kwamba mkopo ule una gharama yake na pia gari inatakiwa ilipiwe premium, ambayo ikawa kama milioni 1.3 nyingine kutoka mfukoni.
View attachment 3056967

Baada ya kufikia uamuzi wa kukataa mabadiliko haya na kuomba hela niliyolipa awali irudi, ndipo wakaanza kuzunguka. Mara wanasema mpaka gari iuzwe ndio walipe.

Na pia zaidi ya hapo. Wakaendelea kusema kwenye ile hela ya awali. Watakata gharama yao ya kuagiza gari.

Ingawa nilikubaliana na yote hayo. Bado wameendelea kuzunguka na mpaka hivi sasa kuna kesi ya madai inaendelea mahakamaini kurudisha hio hela.

Hivyo huu uzi uwe ni tahadhari kwa mtu ambae yuko kwenye hatua ya kutaka kufanya biashara na hawa jamaa. Jua kwamba sio waaminifu na ni matapeli…

Na huu uzi sio kwamba ninaandika kuharibia biashara, hapana. Hii hapa ni screenshot ya chat na namba yao, ambayo pia wameeka kwenye ukurasa wao wa instagram.
View attachment 3056985
Kampuni ni Beforward na SBT kwa wale wa kipato cha chini tuchezee humo tu. Nje ya hapo unajiweka kwenye hatari ya kupigwa
 
Pole ila najiuliza kama ulikua tayari kulipa 600k + kila mwezi ulikuwa na haja gani ya kukopa gari.... uvumilivu ulikushinda kukusanya hela ya gari.....

Inakuaje unakopa gari?
Watu kama nyie mkiambiwa muingie showroom za bongo mnakimbilia ohh wameshusha km mara gari mbovu 😂😂😂😂 pole ila jifunze.
 
pole ila najiuliza kama ulikua tayari kulipa 600k + kila mwezi ulikua na haja gani ya kukopa gari.... uvumilivu ulikushinda kukusanya hela ya gari.....

inakuaje unakopa gari?
watu kama nyie mkiambiwa muingie showroom za bongo mnakimbilia ohh wameahusha km mara gari mbovu 😂😂😂😂 pole ila jifunze.
Acha wapigwe ni wageni wa jiji,
 
Inakuaje mnaingia kingi Kwa watu wasio na mtaji hata kidogo, watafute wenye showroom nunua gari, au ingia nao mkataba wakuagizie gari, hapo utakua salama lakini hawa wa vijiofisi uchwara wasio na mtaji ni madalari wanaonuka umaskini na utapeli
Mkataba upo na ulisigniwa na una mhuri wa mwanasheria. Na mpaka kumpata mwanasheria nilikaza sana ili nijilinde kisheria. Nadhani hawa jamaa ni watu ambao wanachukulia vitu poa tu.
 
Inakuaje mnaingia kingi Kwa watu wasio na mtaji hata kidogo, watafute wenye showroom nunua gari, au ingia nao mkataba wakuagizie gari, hapo utakua salama lakini hawa wa vijiofisi uchwara wasio na mtaji ni madalari wanaonuka umaskini na utapeli
Shida watu wanataka gari chap chap.
Kwamba peleka kianzio M6, urudi nyumbani na IST. Nyingine utalipa mdo mdo within 2yrs.

Bora hizo 2yrs utunze hizo hela mwenyewe tu,
 
Pole sana

Sina msaada zaidi ya kutoa lawama nami naanza hivi
Umeyataka mwenyewe kama huna hela ya kununua gari kwanini ulazimishe.
When the deal is too good......
Ungenunua gari mkononi usingekuwa unalialia na kesi mahakamani au showroom za bongo
 
Shida watu wanataka gari chap chap.
Kwamba peleka kianzio M6, urudi nyumbani na IST. Nyingine utalipa mdo mdo within 2yrs.

Bora hizo 2yrs utunze hizo hela mwenyewe tu,
Watu wana kimuhemuhe cha magari na nikutopiga hesabu vizuri tu ila kama zimo kichwani gari sio kitu ya kukopa....

Utajikuta unacheza opa gangnam style
 
pole ila najiuliza kama ulikua tayari kulipa 600k + kila mwezi ulikua na haja gani ya kukopa gari.... uvumilivu ulikushinda kukusanya hela ya gari.....

inakuaje unakopa gari?
watu kama nyie mkiambiwa muingie showroom za bongo mnakimbilia ohh wameahusha km mara gari mbovu 😂😂😂😂 pole ila jifunze.
Mh. Nimejiuliza kama nijibu kiufasaha ila nimeona ya nini… hata hivyo hili ni jukwaa la wengi na maoni ya watu yatakuwa tofauti tofauti pia, ndio uzuri wa mawazo huru.

Mimi ninaweka hapa sio kwamba natafuta huruma humu wala kwamba nitapata haki yangu humu, hapana. Ninatoa tu tahadhari ya kampuni ambayo iko huko mtaani na ambayo imesajiliwa na BRELA, na wana ofisi yao pale luther house Azania front.

Kwahiyo sio kwamba niliwaokota mtaani bila kujihakikishia inatambulika kisheria, na wala sio kwamba sijui kuwa hela inaweza kutunzwa.

Kuipata hela nitaipata tu, nina uhakika na hilo. Naona tu ni kadhia ambayo si vizuri iendelee kuwepo kwa watu wengine baadae.
 
Wabongo tunapenda sana kujikakamua wakati uwezo mdogo, unakopaje gari? Kulikuwa na haraka gani ya kuwa na hilo gari mpaka uingie kwenye madeni?
Mimi sijui ni watu hamjaelewa. Ningekuwa nataka sana hio gari sana ningekubali hayo masharti mapya ningechukua gari mradi niwe nayo. Ieleweke kuwa gari walileta ila makubaliano ndio yakabadilika. Mbona kuna watu pale wamechukua mkopo wa gari zao.

Mimi tu niliona sio sawa na sio lazima kulipata gari sasa hivi nikakataa ndo wakakataa kurudisha gharama za awali nilizolipa. Sasa hata nisingekopa kama ni watu wa kubadilisha makubaliano si wangebadilisha tu maana ndio biashara wanayofanya?
 
Back
Top Bottom