DOKEZO Kampuni ya kuzoa taka nyumbani Mbezi ya Chini inatuumiza Wananchi, inaongeza bei kutoka Tsh 3,000 hadi 15,000

DOKEZO Kampuni ya kuzoa taka nyumbani Mbezi ya Chini inatuumiza Wananchi, inaongeza bei kutoka Tsh 3,000 hadi 15,000

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
Huku kwetu mtaa ya Mbezi ya Chini (Mbezi Chini) kuna changamoto moja ambayo imekuwa kero kwa watu wengi kuhusu uzoaji taka.

Iko hivi, mamlaka za Serikali za Mtaa za mitaa ya Mbezi Chini, Afrikana na sehemu nyingine ambazo bado sijajua zimekuwa zikitoza kiasi cha shilingi 3,000 hadi 5,000 kwa kila nyumba kwa ajili ya taka za nyumbani.

Yaani kila nyumba inatoa kiasi hicho cha fedha, lakini kuna kampuni ambayo imepewa tenda ya kukusanya taka kwenye nyumba mbalimbali yenyewe imekuwa ikiongeza cha juu na kutoza hadi shilingi 15,000 kwa nyumba.

Inavyoonekana wanachagua baadhi ya nyumba wakiona mambo safi, basi wanaongeza bei na sio ile buku tatu kama inavyotozwa za Serikali za Mtaa.

Naomba mamlaka ziangalie kinachoendelea kwani hii hali inatuumiza, kwa jinsi gharama za maisha zilivyo juu, tuna mambo mengi ya kufanya na yanayotupa stress, hawa wazoa taka nao wanakuja kutongezea stress, watatupasua kichwa

Changamoto nyingine ni hii Kampuni iliyopewa tenday a kukusanya taka, kwanza ukiwauliza kampuni yao inaitwaje wao wanakwambia tu wewe toa hela na kudai wao ndio wamekabidhia jukumu hilo.

Ukiuliza Serikali za Mtaa nao inavyoonekana kuna watu wamepiga cha juu kwa kuwa hawatoi majibu ya kueleweka kuhusu kampuni walizozipa tenda.
 
Uko mbezi gani wewe unalia kisa 15000 Amia Mbagala huku 2000 kwa mwezi kila nyumba
 
Huku kwetu mtaa ya Mbezi ya Chini (Mbezi Chini) kuna changamoto moja ambayo imekuwa kero kwa watu wengi kuhusu uzoaji taka.

Iko hivi, mamlaka za Serikali za Mtaa za mitaa ya Mbezi Chini, Afrikana na sehemu nyingine ambazo bado sijajua zimekuwa zikitoza kiasi cha shilingi 3,000 hadi 5,000 kwa kila nyumba kwa ajili ya taka za nyumbani.

Yaani kila nyumba inatoa kiasi hicho cha fedha, lakini kuna kampuni ambayo imepewa tenda ya kukusanya taka kwenye nyumba mbalimbali yenyewe imekuwa ikiongeza cha juu na kutoza hadi shilingi 15,000 kwa nyumba.

Inavyoonekana wanachagua baadhi ya nyumba wakiona mambo safi, basi wanaongeza bei na sio ile buku tatu kama inavyotozwa za Serikali za Mtaa.

Naomba mamlaka ziangalie kinachoendelea kwani hii hali inatuumiza, kwa jinsi gharama za maisha zilivyo juu, tuna mambo mengi ya kufanya na yanayotupa stress, hawa wazoa taka nao wanakuja kutongezea stress, watatupasua kichwa

Changamoto nyingine ni hii Kampuni iliyopewa tenday a kukusanya taka, kwanza ukiwauliza kampuni yao inaitwaje wao wanakwambia tu wewe toa hela na kudai wao ndio wamekabidhia jukumu hilo.

Ukiuliza Serikali za Mtaa nao inavyoonekana kuna watu wamepiga cha juu kwa kuwa hawatoi majibu ya kueleweka kuhusu kampuni walizozipa tenda.
Ni hatari halafu sasa unakuta taka taka zinachukuliwa kwa mwezi mara 1 au ikizidi 3
 
Back
Top Bottom