remon
JF-Expert Member
- Sep 21, 2011
- 295
- 48
Wadau naomba kujuzwa kuhusu kampuni ya maxmalipo, hasa wale mawakala au kwa yeye kujua. Ni miezi kadhaa sasa machine maxmalipo zimekuwa zinausumbufu mkubwa sana, nikiwa na maana mara nyingi imekuwa ukitaka kulipia huduma fulani hamna mtandao , huduma moja wapo ni umeme(kununua luku) tra (vehicle road licence), vocha na nyingine nyingi. Hii kitu imekuwa inaleteta usumbufu mkubwa kwa utumiaji na mawakala. Je hawa jamaa ni kwamba wameshindwa kazi? Maana wanaingiza bidhaa nyingi huku ikionekana hawana uwezo. Je makampuni yanayoingia nao ubia kufanya malipo mbali mbali wanaliangalia hili?