DOKEZO Kampuni ya Mkwawa Leaf haijawalipa wakulima wa tumbaku tangu wanunue tumbaku mwezi Aprili

DOKEZO Kampuni ya Mkwawa Leaf haijawalipa wakulima wa tumbaku tangu wanunue tumbaku mwezi Aprili

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Sexless

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2017
Posts
23,683
Reaction score
55,898
Kwa msiofahamu tumbaku hununuliwa na makampuni tofauti. Makampunj yaliyopewa leseni ya kununua tumbaku mkoani Tabora ni pamoja na Voedsel, Alliance One, TLTC, GTI, Mkwawa na mengine nimeyasahau.

Katika makampuni yote haya kampuni iliyopewa zabuni kubwa zaidi ni Mkwawa Leaf kwa madai kuwa ni kampuni ya wazawa. Na ilipigiwa promo sana na vyombo vya habari pamoja na serikali.


Masoko ya ununuzi wa tumbaku mwaka huu yalifunguliwa mwezi April, na makampuni yalipewa sharti la kuwalipa wakulima fedha zao ndani ya wiki mbili tu. Makampuni karibu yote yametekeleza sharti hilo, na hivi ninavyoandika dokezo hili vyama vyote vya ushirika wa wakulima vilivyouza tumbaku yao katika makampuni ya kigeni wamelipwa fedha zao.

Lakini wakulima waliouza tumbaku yao kenye kampuni ya Mkwawa Leaf tangu mwezi April mpaka leo wanapigwa kalenda.

Kiburi cha kamapuni hii kinatoka wapi?
Za ndani kabisa zinasema kampuni ya Mkwawa Leaf imeundwa na vigogo wa serikali pamoja na wafanyabiashara wakubwa ikiwa ni pamoja na waziri Bashe. Nani atawagusa hawa? Wakubwa waliopaswa kuwasaidia wakulima nao wanashiriki dhulma.

Bashe akiwa mbele ya kamera anaongea mpaka povu linamtoka akiigiza kuwatetea na kuwapigania wakulima. Lakini kwenye suala la dhulma inayofanywa na kampuni ya Mkwawa Leaf hasemi chochote kwasababu naye ni miongoni mwa wahusika katika dhulma hii.
 
Watamleta Diamond awaburudishe wanatabora msahahu shida zenu kama ilivyokuwa mwanza jana.

Kwenye hiyo kampuni ya leaf Majaliwa hawezi kuwepo wengine uliowataja sawa.
 
Baadhi wanasema wameshalipwa hili limekaaje mkuu?
Bado mpk leo mkuu. Wamekuwa wakiirusha tarehe tangu kipindi hicho mpk leo. Mara ya mwisho waliahidi kulipa ifikapo July 31, lkn baadaye wakatoa sababu lukuki na kutoa tarehe mpya ya malipo kuwa itakuwa tarehe 15 August. Mpk Sasa bado siku 2 tufike 15 August lkn hakuna hata dalili za michakato ya awali kuonesha kuwa watalipa.
 
Mt huwel kanjanja from Iringa who act as a owner of the company on behalf of several corrupted gvt officials...ushetu pia wanalalamika wengi hawajalipwa had leo...
 
Mt huwel kanjanja from iringa who act as a owner of the company on behalf of several corrupted gvt officials...ushetu pia wanalalamika wengi hawajalipwa had leo...
Nchi ngumu sana hii. Bora Mwarabu apewe tenda ya kununua mazao ya wakulima kuliko hawa wakoloni weusi
 
Failed state Tanzania hii nchi kufikia 2030 tutajua na sura nyingine kabisa ata coup inaweza tokea watu tumeumizwa Kwenye tumbaku
 
Kwa msiofahamu tumbaku hununuliwa na makampuni tofauti. Makampunj yaliyopewa leseni ya kununua tumbaku mkoani Tabora ni pamoja na Voedsel, Alliance One, TLTC, GTI, Mkwawa na mengine nimeyasahau.

Katika makampuni yote haya kampuni iliyopewa zabuni kubwa zaidi ni Mkwawa Leaf kwa madai kuwa ni kampuni ya wazawa. Na ilipigiwa promo sana na vyombo vya habari pamoja na serikali.


Masoko ya ununuzi wa tumbaku mwaka huu yalifunguliwa mwezi April, na makampuni yalipewa sharti la kuwalipa wakulima fedha zao ndani ya wiki mbili tu. Makampuni karibu yote yametekeleza sharti hilo, na hivi ninavyoandika dokezo hili vyama vyote vya ushirika wa wakulima vilivyouza tumbaku yao katika makampuni ya kigeni wamelipwa fedha zao.

Lakini wakulima waliouza tumbaku yao kenye kampuni ya Mkwawa Leaf tangu mwezi April mpaka leo wanapigwa kalenda.

Kiburi cha kamapuni hii kinatoka wapi?
Za ndani kabisa zinasema kampuni ya Mkwawa Leaf imeundwa na vigogo wa serikali pamoja na wafanyabiashara wakubwa ikiwa ni pamoja na waziri Bashe. Nani atawagusa hawa? Wakubwa waliopaswa kuwasaidia wakulima nao wanashiriki dhulma.

Bashe akiwa mbele ya kamera anaongea mpaka povu linamtoka akiigiza kuwatetea na kuwapigania wakulima. Lakini kwenye suala la dhulma inayofanywa na kampuni ya Mkwawa Leaf hasemi chochote kwasababu naye ni miongoni mwa wahusika katika dhulma hii.
Hao wahuni kumekucha
 
Baadhi wanasema wameshalipwa hili limekaaje mkuu?
Hawa jamaa walichofanya ni kwamba wamelipa robo tu (yaani kama kama kulifanyika minada 4 wanalipa 1). Ndiyo maana ukiuliza baadhi ya wakulima wanasema wamelipwa. Wamemtumia ujanja huo.

Kinachoonekana hawana mtaji wa kutosha. Kwasbb watu wao wanaowatuma kuongea na wakulima wanadai tumbaku ilikuwa nyingi kuliko uwezo wa kampuni.
 
Pesa zenu Mkwawa leaf wameenda kujinunulia magari ya kifahari, 'yametapakaa' mkoa wa Morogoro, mji mzima!
 
Ilikuwa kosa kubwa sana kuwakimbiza Universal kwenye uwekezaji wa tumbaku. Na sijui kama watarudi tena. Zile kodi ambazo sijui walikuwa wanazitoa wapi, zimesababisha mengi sana
 
Back
Top Bottom