Wakuu habari zenu? Naomba maelekezo na ushauri juu ya uanzishaji na uendeshaji wa kampuni binafsi ya ulinzi (security guard).
Nahitaji kujifunza juu ya;
- Taratibu na mahitaji ya usajili wa kampuni (specifically ya ulinzi)
- Hali ya soko na namna ya kupenya sokoni
- Makadirio ya vifaa vya lazima kuanzia kazi
- Makadirio ya gharama za uanzishaji
- Mengineyo ya muhimu.
Tafadhali sana, na Mungu awanyeshee baraka zake kila mmoja kwa kadiri ya imani yake.