hahahaha MMK umenikumbusha hii kauli aliwayi kuitoa kama si Mzee Msekwa ni Mzee Mkapa alisema "Watanzania wana Wivu wa kike" Lol
Ukikumbuka kilichomkuta mzee msekwa ndo hapo utajua kwanini jamaa liamua kumnasa kibao "my wife" wake.
Hakika hata ningekua mimi ningefanya kama alivyofanya huyu jamaa,...mimi mwanaume ninawivu wa kiume na mwanamke ana wivu wa kwake_hii ni kama kuingilia mambo ya kike ambayo ni jinsia ingine...period
Wewe unajitambua na sina shaka kwamba mkeo hawezi kuthubutu kukusemea maneno mbofu mbofu kama hiyo.
Mimi nafikiri tatizo sio kuambiwa una wivu wa kike, tatizo ni ile dharau aliyoipata kwa mkewe na kulinganishwa na mwanamke!. Hayo ni mawazo yangu, ngoja wenyewe wajisemee...............
Ahsante bi.mdogo, mumeo kapata mke mwema na mwenye busara hadi nakaribia kumuonea wivu!
wivu wa kike ni wa kumtakia mwanaume mema zaidi ktk kudumisha ndoa yake, wivu wa kiume hauelezeki maana hautabiriki
Acha uongo mwana, tangu lini wivu wa kike ukawa ni kumtakia mema? kama ndivyo unamdanganya mumeo, basi siku akijua umekwisha!
Mwanamke alikosea kumwambia ana wivu wa kike hata ningekuwa mimi ningemdunda
Yeah man, heshima ni muhimu kama mke hataki unamlazimisha, kata vibao kwa kwenda mbele!
Chonde chonde Fidel,waoneeni huruma kinamama,wao sio gunia la mpunga kwamba unawadunda ili upate mchele,ni binadamu ati kama wewe,na kumbuka usilotaka ufanyiwe wewe katu usimfanyie binadamu mwenzio.
Kwani kumtukana mume wake napo si ni domestic violence. Mke naye amuonee huruma mume wake ili naye aonewe huruma, ebo!
Hiyo red dah kumbe kuna wanaume bado wanadunda wanawake zao?? Mie ukinyoosha mkono tu nafungasha virago huyooo kwa mama yangu
Kama hupendi mumewako anyooshe mkono basi nawe usinyanyue mdomo. Kama unafunga virago kurudi kwa mama yako naye anakupokea basi tutamhoji mama alikuleaje hadi unakuwa mkaidi kiasi hicho!?
Kwa yeyote atakae kwazika naomba in Advance anisamehe....
Wivu wa Kike...
Tokana na tamaduni zetu ambazo zilikua mfumo dume... ilifanya wanawake kazi zao mara nyingi ziwe za kijamii zaidi (sijui niseme za kifamilia??) shughuli kubwa ilikua kushinda nyumbani akifanya akihandle nyumba kama kupika na usafi wa home related (deki, vyombo, kufua).. na baada ya hapo kujikuta hawana shughluli zaidi ya kukaa kijiweni wakisukana nywele na kupiga soga - Soga ambazo mara nyingi zilikua nimelenga kuzungumzia habari za watu wengine... Hayo mazungumzo mara nyingi huwa base on Chuki na Wivu - Wivu ambao hutakana na kuzidiana katika mambo kama uzuri, kupendwa na opposite sex, nailing mwanaume wa maana na mambo mengine kibao....
It should be noted kua sasa hivi ulimwengu umebadilika na wivu wa kijinga kwa kiasi kikubwa unapungua thou bado kuisha.... Hivo basi traditionally inajulikana mwanamke ana wivu wa kijinga sababu tu sio Wivu ambao ni constructive....
Wivu wa Kiume...
Kama nilivoeleza hapo juu basi ni vise versa kwa wanaume... Wengi walikua/wanaji shughulisha na mambo ya maendeleo katika jamii... kama vile kusoma... Hio iliwapelekea kua na shughuli za kuajiriwa ama kujiajiri... na ilizoeleka hako nyuma wanaume ndio wapo sorely responsible taking care of the family (thou kuna conflicting schools of thot - tokana na kazi kubwa bibi zetu walifanya hasa za mashambani).. Wao mara nyingi ili/imeonekana hata wakizungumzia mwanaume mwenzao wanazungumzia maendeleo alonayo... Mtaji... Mafanikio - Hio kujenga wivu among wengi... Hivo wivu wao kuonekana kama ni wa Msingi na wa kujenga... Hivo mara nyingi pharase ya wivu wa Kiume ni ule wivu ambao unafanywa huku ukileta matunda fulanai...
However hata wao wamechange... wanaume wengi wamekua na mtindo wa kubweteka... Wakimzungumzia jamaa na mafanikio yake - wanaishia kusema kapata deal... Hivo nae anakaaa hapo kijiweni kusubiri deal ije badala ya kujishughulisha...
Note that Niloongea hapo sio Universal but in most cases according my opinion....
Ahsante kwa somo zuri bibie, ila huo wivu wa kiume bado sijauelewa elewa!
Uzuri wakina mama mkwe wa siku hizi ukirudi tu home wanakutimua rudi huko huko
Mama mkwe asipomtimua, basi huyo atakuwa ni wale waliofundwa ku handle mafiga matatu!!
Kuambiwa una wivu ni jambo moja lakini kuambiwa una wivu wa kike huyo mtu kakutusi.
Sangara there you are, kula gwala!
Kwa maana rahisi ni kwamba mambo yako yote ni ya kike kike.Kwa hiyo ndo maana jamaa alikasirika sana.
Ndio manake mkuu, huyo mwanamke alipata alichostahili.
Mods siku ile sijui kwa nini walitupeleka kule bana au ndo huo "Wivu wa kike" lol
Mkuu angalia usije ukanaswa kibao na mods!!
Matusi yoyote yanayocross gender bounderies yanahitaji kushughulikiwa kwa umakini na haraka zaidi...Ukicheka cheka kama mzee wetu utaambulia patupu!!
Huyo jamaa ni dume kweli kwani hata mimi ningefanya hivyo hivyo!! Hii inasaidia kuifanya nchi (familia) itawalike!!
Halafu sijui kwa nini, ila duniani hakuna wivu wa kiume.....Kama kuna mtu alishawahi kusikia atueleze alikoupata!!
Mkuu nadhani hapa umefunga kazi, sina cha kuongezea. Naungana nawe kusubiri "ripoiti" ya wivu wa kiume.