Kanda ya Ziwa wanastahili pongezi kwa uendeshaji wa baiskeli

Kanda ya Ziwa wanastahili pongezi kwa uendeshaji wa baiskeli

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,189
Reaction score
10,375
Unaweza ukashindana na watu wa Kanda ya Ziwa kwa mambo fulani fulani, lakini usithubutu kwenye uendeshaji wa baiskeli kama wewe si mmoja wao. Utaumbuka! Nazungumzia baiskeli za kawaida au za kazi, siyo zile za "starehe".

Sina uthibitisho wa kitakwimu, lakini kwa makisio yangu, Kanda ya Ziwa inaongoza kwa uendeshaji baiskeli.

Najua Singida nako wako vizuri, lakini sidhani kama wanawafikia "Wasukuma"

Ni nadra kwa mkoa niliokulia kumkuta mwanamke akiendesha baiskeli, lakini ni kitu cha kawaida kwa Geita, Shinyanga, na Mwanza, hasa maeneo ya vijijini. Huko, si ajabu kukutana na mwanamke amebeba mzigo mkubwa kwenye baiskeli ambao mwanaume wa mikoa mingine asingeweza.

Najua kuendesha baiskeli, lakini watu wa Kanda ya Ziwa walinifanya nijione Chekechea kwenye uendeshaji baiskeli.

Wakati fulani, nilikuwa Misungwi maeneo ya vijijini mkoani Mwanza, nilipoamua kukodi baiskeli kwa lengo la kuitumia kama usafiri wa kunifikisha mahala fulani. Usafiri uliokuwa ukipatikana huko ni wa pikipiki na baiskeli za kukodi. Niliamua kukodi baiskeli.

Nikiwa njiani, mama mmoja wa Kisukuma akiwa na baiskeli, alikuwa amebeba mzigo juu ya baskeli na mtoto mgongoni, alinipita kama vile nimesimama.

Sikutaka ligi naye, ingawa sikupenda alivyonipita kwa "dharau". Niliishia kumwambia kimoyo moyo, "nenda salama mama"

Kanda ya Ziwa hongereni!!!
 
Unaweza ukashindana na watu wa Kanda ya Ziwa kwa mambo fulani fulani, lakini usithubutu kwenye uendeshaji wa baiskeli kama wewe si mmoja wao. Utaumbuka! Nazungumzia baiskeli za kawaida au za kazi, siyo zile za "starehe".

Sina uthibitisho wa kitakwimu, lakini kwa makisio yangu, Kanda ya Ziwa inaongoza kwa uendeshaji baiskeli.

Najua Singida nako wako vizuri, lakini sidhani kama wanawafikia "Wasukuma"

Ni nadra kwa mkoa niliokulia kumkuta mwanamke akiendesha baiskeli, lakini ni kitu cha kawaida kwa Geita, Shinyanga, na Mwanza, hasa maeneo ya vijijini. Huko, si ajabu kukutana na mwanamke amebeba mzigo mkubwa kwenye baiskeli ambao mwanaume wa mikoa mingine asingeweza.

Najua kuendesha baiskeli, lakini watu wa Kanda ya Ziwa walinifanya nijione Chekechea kwenye uendeshaji baiskeli.

Wakati fulani, nilikuwa Misungwi maeneo ya vijijini mkoani Mwanza, nilipoamua kukodi baiskeli kwa lengo la kuitumia kama usafiri wa kunifikisha mahala fulani. Usafiri uliokuwa ukipatikana huko ni wa pikipiki na baiskeli za kukodi. Niliamua kukodi baiskeli.

Nikiwa njiani, mama mmoja wa Kisukuma akiwa na baiskeli, alikuwa amebeba mzigo juu ya baskeli na mtoto mgongoni, alinipita kama vile nimesimama.

Sikutaka ligi naye, ingawa sikupenda alivyonipita kwa "dharau". Niliishia kumwambia kimoyo moyo, "nenda salama mama"

Kanda ya Ziwa hongereni!!!
Waje wayapokee maua yao! Kongole za kutosha (kina mama) wamewakilisha vyemaaaa
 
Unaweza ukashindana na watu wa Kanda ya Ziwa kwa mambo fulani fulani, lakini usithubutu kwenye uendeshaji wa baiskeli kama wewe si mmoja wao. Utaumbuka! Nazungumzia baiskeli za kawaida au za kazi, siyo zile za "starehe".

Sina uthibitisho wa kitakwimu, lakini kwa makisio yangu, Kanda ya Ziwa inaongoza kwa uendeshaji baiskeli.

Najua Singida nako wako vizuri, lakini sidhani kama wanawafikia "Wasukuma"

Ni nadra kwa mkoa niliokulia kumkuta mwanamke akiendesha baiskeli, lakini ni kitu cha kawaida kwa Geita, Shinyanga, na Mwanza, hasa maeneo ya vijijini. Huko, si ajabu kukutana na mwanamke amebeba mzigo mkubwa kwenye baiskeli ambao mwanaume wa mikoa mingine asingeweza.

Najua kuendesha baiskeli, lakini watu wa Kanda ya Ziwa walinifanya nijione Chekechea kwenye uendeshaji baiskeli.

Wakati fulani, nilikuwa Misungwi maeneo ya vijijini mkoani Mwanza, nilipoamua kukodi baiskeli kwa lengo la kuitumia kama usafiri wa kunifikisha mahala fulani. Usafiri uliokuwa ukipatikana huko ni wa pikipiki na baiskeli za kukodi. Niliamua kukodi baiskeli.

Nikiwa njiani, mama mmoja wa Kisukuma akiwa na baiskeli, alikuwa amebeba mzigo juu ya baskeli na mtoto mgongoni, alinipita kama vile nimesimama.

Sikutaka ligi naye, ingawa sikupenda alivyonipita kwa "dharau". Niliishia kumwambia kimoyo moyo, "nenda salama mama"

Kanda ya Ziwa hongereni!!!
Sasa hawajielewi walitakiwa wawe na Mashindano makubwa ya baiskeli,tour de Shinyanga via Gamboshi 😆😆

Mwisho Kuna siku ya baiskeli Duniani Huwa inaadhimishwa mwezi May Kila mwaka.
 
Nijuzi hapa nilikua mkoani shinyanga nmestaajabu mno kuona uwingi wabaiskel tena kati yamji wao wanaziita daladala, kimbembe mwenyej wangu akanambia chukua daladala uje town wakat mi niko kitangili subir daladala sion kumuliza vizur akacheka sana akanambia ni baiskel ndo daladala
 
Wewe nenda kilombero morogoro ukaone mama kabeba mzigo kichwani wa kuni,mgongoni kambeba mtoto,mkono mmoja kabeba chupa ya uji wa mtoto,anaendesha baiskeli kwa mkono mmoja tena baiskeli za seewa
 
Geographical area yao ni tambalale almost yote.

Hivyo inakuwa ni rahisi kwa matumizi ya baiskel
 
Sasa hawajielewi walitakiwa wawe na Mashindano makubwa ya baiskeli,tour de Shinyanga via Gamboshi 😆😆

Mwisho Kuna siku ya baiskeli Duniani Huwa inaadhimishwa mwezi May Kila mwaka.
Angepatikana promota wa huo mchezo, Kanda ya Ziwa wangeufaidi sana.
 
Nijuzi hapa nilikua mkoani shinyanga nmestaajabu mno kuona uwingi wabaiskel tena kati yamji wao wanaziita daladala, kimbembe mwenyej wangu akanambia chukua daladala uje town wakat mi niko kitangili subir daladala sion kumuliza vizur akacheka sana akanambia ni baiskel ndo daladala
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣

Hukuonekana mshamba?
 
Wewe nenda kilombero morogoro ukaone mama kabeba mzigo kichwani wa kuni,mgongoni kambeba mtoto,mkono mmoja kabeba chupa ya uji wa mtoto,anaendesha baiskeli kwa mkono mmoja tena baiskeli za seewa
Aisee!

Tanzania ina vivutio vingi vya utalii ambavyo havitumiki ipasavyo. Hiyo staili inaweza kutumika kama kivutio cha kitalii.
 
Angepatikana promota wa huo mchezo, Kanda ya Ziwa wangeufaidi sana.
Angepatikana promota wa huo mchezo, Kanda ya Ziwa wangeufaidi sana.
Shida mashindano ya baiskeli huwa ni kuchawiana sana. Kuna mashindano yalifanyika Kahama jamaa wanakimbiza pikipiki inasoma speed 60 na wao nyuma wanaifuzia pikipiki bampa to bampa
 
Yani mtu anaona ajabu na kuwashangaa kanda ya ziwa wakiendesha baiskeli, ajabu yake nini sasa! Mbona india, china n.k watu wanadrive!! Nongwa ni msukuma!! Ni bora mkoa uongoze kwa baiskeli kuliko mkoa uongoze kwa walevi wa gongo/mbege na ujambazi
 
Nilikuwa kahama kitu nilikuwa naogopa barabarani baiskel na bajaji nyingi mno kupitia hata pikipiki.
 
Shida mashindano ya baiskeli huwa ni kuchawiana sana. Kuna mashindano yalifanyika Kahama jamaa wanakimbiza pikipiki inasoma speed 60 na wao nyuma wanaifuzia pikipiki bampa to bampa
😀
 
Back
Top Bottom