Kanga hatagi Utumwani ?

Kanga hatagi Utumwani ?

Kennedy

JF-Expert Member
Joined
Dec 28, 2011
Posts
54,894
Reaction score
64,043
Salam kwa wote wana jukwaa pendwa la Dokta.

Kumekuwepo na hadithi(simulizi) kuwa unapofunga Ndege aina ya Kanga huwa ni vigumu sana kumuweka kwenye mfano banda kama Kuku halafu kwa muda atakaoishi wakiwa wawili wa jinsia ya jike na dume wakataga mayai ndani ya banda hilo . Baadhi ya watu hushauri kuwa unafuga Kanga baada ya kuzoea hapo unapowafuga ni vizuri ukawapa uhuru wa kutembea huku na kule pia itafanya wao kutaga vichakani na kufukia mayai chini muda wa kuanguliwa unapofika hurudi na vifaranga sehemu wanapoishi lakini sio kutagia kwenye Banda kama Kuku,Bata,Njiwa na n.k.



Wataalam,Madokta wetu wa jukwaa hili kuhusu jambo hili nimekuwa na maswali kadhaa najiuliza bila kupata majibu:-

1. Kanga wanapofugwa kwenye banda huwa hawakutani kimwili mpaka awe huru ama hujizuia fanya tendo la kukutana kimwili mpaka kuwe na vichaka ama pori?

2. Hukutana kimwili lakini kusikoweza kufanya watage mayai kwa kipindi hicho wanapokuwa Bandani?

3. Ama kwa kuwa Kanga hatamii mayai kama kuku afanyavyo na badala yake huyafukia kwenye mchanga tu.



Karibu kwa michango mbalimbali ya kitaalam,kisayansi
.
 
ndugu si kweli sis hap nyumbani tunakanga wale wa kawaida n weupe.huwa wanatag ndani sema kutamia ndo ishu.
 
Jukwaa LA elimu ,au hapa had I watu wavetenary wapo? LA mie sijui
 
ndugu si kweli sis hap nyumbani tunakanga wale wa kawaida n weupe.huwa wanatag ndani sema kutamia ndo ishu.



Mkuu nimekuelewa vizuri lakini kumbuka hao kanga weupe nadhani ni wa kisasa zaidi ninaongelea hapa ni wale wa asili ya porini wenye madoadoa maana baadhi ya sehemu huenda porini na kupata mayai halafu huweka kwa kuku anaatamia
halafu vifanga vinapatikana.

Hao mara nyingi huwa hawatagi wanapowekwa kwenye banda mpaka wapewe uhuru wa kwenda huku na huko na hatimaye kupata vichaka vya kutaga.
 
Hii mada kama sio mahali lake?



Mkuu Phil mada hii nimeileta hapa kwa maana wataalam wa masuala ya tiba hasa mambo ya uzazi lakini ushauri wako sio mbaya Invisible/Mods kama wakiona inafaa kuwa labda jukwaa la Intelijensi wanawezaipeleka kule.
 
Unazidi kukosea. Sasa inteligensia tumpeleleze kanga!. Bora jukwaa la elimu au hoja mchanganyiko.QUOTE=Kennedy;8239732]Mkuu Phil mada hii nimeileta hapa kwa maana wataalam wa masuala ya tiba hasa mambo ya uzazi lakini ushauri wako sio mbaya Invisible/Mods kama wakiona inafaa kuwa labda jukwaa la Intelijensi wanawezaipeleka kule.[/QUOTE]
 
Jukwaa LA elimu ,au hapa had I watu wavetenary wapo? LA mie sijui



Mkuu Phill


Jukwaa la Elimu/Dokta/Intelijensi nadhani Uongozi wa JF utasidia kupeleka pale panapofaa zaidi lakini
naona kama hapa ilipo ni sawa tu.
 
Labda wakiwa bandani watakua wanakatuana kwa kondo.mu. Otherwise nyota ya kijani itakua inahusika unabisha?
 
Labda wakiwa bandani watakua wanakatuana kwa kondo.mu. Otherwise nyota ya kijani itakua inahusika unabisha?



Teh ha ha
ndege na haya mambo ya uzazi najua huwa hawatumii kamwe.
 
Back
Top Bottom