Kanisa Kulipa $ 166 milllions kwa waliopatikana na maovu ya mapadre

Kanisa Kulipa $ 166 milllions kwa waliopatikana na maovu ya mapadre

Percival

JF-Expert Member
Joined
Mar 23, 2010
Posts
3,676
Reaction score
2,621
Kanisa katoliki litalipa dola za kimarekani zipatazo millioni 166 kwa watu walio ingiliwa na mapadre wakati wakiwa watoto wadogo na wakiishi katika himaya za kanisa. Wengi wa watu hawa ni wananchi wa marekani wajulikanao kama wahindi wekundu ambao kanisa lilikua likisema linawasaidia kwa mashule na malezi. Habari hizi za kusikitisha zilizosababishwa na mapadre waliopotoka zinaendelea kujitokeza na kuharibu jina zuri la kanisa katoliki.

Cha kushangaza ni kua hii fidia ya mamilioni ya dola inatoka kwenye mfuko wa sadaka na zaka ambao waumini wa kanisa hilo hutoa kwa moyo wa kidini.

http://www.boston.com/news/nation/articles/2011/03/26/jesuit_order_to_pay_abuse_victims_166m/?p1=Well_MostPop_Emailed4

Swali kubwa la kujiuliza ni Je inawezekana mambo haya yametokea hapa Tanzania ? Uwezekano kua mambo haya pia yametokea hapa ni mkubwa sana ukichukulia kuwa watoto wadogo wengi walikua wakipewa mafundisho na upendo katika seminari mbali mbali hapa nchini. Ni muhimu kuwahimiza watu wajitokeze ili jambo hili pia lijadiliwe hapa na lizikwe. sababu utakuta watu hao walio chezewa wakiwa wadogo hawana raha au amani katika mioyo yao mpaka watakapo ona mambo yamejadiliwa. pia inawezekana bado yanaendelea katika hizo seminari.
 
Ninachowapendea watu wa western na mifumo yao ni uwazi na kuwajibishana... Nenda nchi za kiarabu uone madhila wanayofanyiwa watumishi wa ndani toka far-east na Africa, kubakwa, kuteswa kwa vipigo nk. ikiwa public maskin wa Mungu anarudishwa kwao na kesi imeisha!
 
Serikali ingefaa ianzishe uchunguzi wa jambo hili na kuwaambia watu waliopata majamga haya wakati wakiwa wadogo wajitokeze ili mambo yaangaliwe kwa kina.

Ni lazima kuna mapadre ( wazungu ) walifanya mambo machafu kwa watoto hapa nchini kwa miaka ya nyuma sababu siku zote utawakuta wako na watoto na watachagua na kuwachukuwa mmoja au wawili kwnye pikipiki au gari na kutoka nao au watasema wana kazi au masuala ya maombi nyumbani kwa padre.

Haiwezekani hawa wakafanya haya machafu huko Ulaya na Amerika pekee lazima yametokea huku pia.
 
....kuharibu jina zuri la kanisa katoliki.

Cha kushangaza ni kua hii fidia ya mamilioni ya dola inatoka kwenye mfuko wa sadaka na zaka ambao waumini wa kanisa hilo hutoa kwa moyo wa kidini.

kwenye red....mmmhhhh
kwenye blue, ikiwa wanatoa sadaka na zaka kwa dini na si Mungu, wacha zitumike kufidia uchafu walioufanya wenye dini.
 
Kanisa katoliki litalipa dola za kimarekani zipatazo millioni 166 kwa watu walio ingiliwa na mapadre wakati wakiwa watoto wadogo na wakiishi katika himaya za kanisa. Wengi wa watu hawa ni wananchi wa marekani wajulikanao kama wahindi wekundu ambao kanisa lilikua likisema linawasaidia kwa mashule na malezi. Habari hizi za kusikitisha zilizosababishwa na mapadre waliopotoka zinaendelea kujitokeza na kuharibu jina zuri la kanisa katoliki.

Cha kushangaza ni kua hii fidia ya mamilioni ya dola inatoka kwenye mfuko wa sadaka na zaka ambao waumini wa kanisa hilo hutoa kwa moyo wa kidini.

http://www.boston.com/news/nation/articles/2011/03/26/jesuit_order_to_pay_abuse_victims_166m/?p1=Well_MostPop_Emailed4

Swali kubwa la kujiuliza ni Je inawezekana mambo haya yametokea hapa Tanzania ? Uwezekano kua mambo haya pia yametokea hapa ni mkubwa sana ukichukulia kuwa watoto wadogo wengi walikua wakipewa mafundisho na upendo katika seminari mbali mbali hapa nchini. Ni muhimu kuwahimiza watu wajitokeze ili jambo hili pia lijadiliwe hapa na lizikwe. sababu utakuta watu hao walio chezewa wakiwa wadogo hawana raha au amani katika mioyo yao mpaka watakapo ona mambo yamejadiliwa. pia inawezekana bado yanaendelea katika hizo seminari.
Duu
 
kwenye red....mmmhhhh
kwenye blue, ikiwa wanatoa sadaka na zaka kwa dini na si Mungu, wacha zitumike kufidia uchafu walioufanya wenye dini.
Hivi mungu anahitaji sadaka??? 🤔🤔
 
Back
Top Bottom