Kanisa lililojaa wapalestina laripuliwa Gaza

Kanisa lililojaa wapalestina laripuliwa Gaza

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Baada ya hospitali maarufu kupigwa bomu hapo jana na wagonjwa na madaktari 500 kuuliwa, leo imekuwa ni zamu ya kanisa na misikiti iliyojaa wakimbizi kuripuliwa na majeshi ya Israel.

Hayo yametokea huko Kusini ya Gaza watu walikotakiwa kukimbilia. Sambamba na kanisa na misikiti barabara vile zimebomolewa na makombora hayo ya kutoka kwenye ndege za kivita kuzifanya zisipitike kupeleka misaada inayosubiriwa kwa haraka na jamii hizo za kipalestina.

Mashambulizi yote hayo yanatokea huku umeme na maji vikiwa vimekatwa kwa takriban wiki moja sasa kwenye eneo kubwa la Gaza.

Kama kwamba lengo ni kuwaua wapalestina kwa njaa na kiu malori 20 tu yamekuwa yakipigwa danadana kuingia Gaza kwa muda mrefu kutokea kituo cha Rafah ilhali mahitaji ni tani zinazojaza mamia ya malori kutokana na kusihiwa na mahitaji yote muhimu.

Shambulio la kwenye hospitali lilitanguliwa na tangazo la takriban siku mbili likiwataka wagonjwa na madakrari kuondoka hospitalini hapo ambapo madaktari waligoma kuondoka kwa tamko la kutoweza kuondoka na kuacha wagonjwa wao.Hapo ndio likafuata bomu zito kutoka angani.

Kilichowashangaza wengi kuhusu mashambulio kwenye makanisa na misikiti ni kwamba kila aliyepata nafasi kuingia humo alihisi yuko salama zaidi kinyume na kilichowatokea.
 
Netanyahu mwaga nyuki . Sisi tunasema kama wauaji wa HAMAS wanajificha mahospitalini , makanisani , misikitini nk . Hamna namna mwaga upupu siafu watoke 😂😂🇮🇱🇮🇱🇮🇱
 
Baada ya hospitali maarufu kupigwa bomu hapo jana na wagonjwa na madakrar 500 kuuliwa, leo imekuwa ni zamu ya kanisa na misikiti iliyojaa wakimbizi kuripuliwa na majeshi ya Israel.

Hayo yametokea huko kusini ya Gaza watu walikotakiwa kukimbilia.Sambamba na kanisa na misikiti barabara vile zimebomolewa na makombora hayo ya kutoka kwenye ndege za kivita kuzifanya zisipitike kupeleka misaada inayosubiriwa kwa haraka na jamii hizo za kipalestina.

Mashambulizi yote hayo yanatokea huku umeme na maji vikiwa vimekatwa kwa takriban wiki moja sasa kwenye eneo kubwa la Gaza.

Kama kwamba lengo ni kuwaua wapalestina kwa njaa na kiu malori 20 tu yamekuwa yakipigwa danadana kuingia Gaza kwa muda mrefu kutokea kituo cha Rafah ilhali mahitaji ni tani zinazojaza mamia ya malori kutokana na kusihiwa na mahitaji yote muhimu.

Shambulio la kwenye hospitali lilitanguliwa na tangazo la takriban siku mbili likiwataka wagonjwa na madakrari kuondoka hospitalini hapo ambapo madaktari waligoma kuondoka kwa tamko la kutoweza kuondoka na kuacha wagonjwa wao.Hapo ndio likafuata bomu zito kutoka angani.

Kilichowashangaza wengi kuhusu mashambulio kwenye makanisa na misikiti ni kwamba kila aliyepata nafasi kuingia humo alihisi yuko salama zaidi kinyume na kilichowatokea.
Takbirrrr.
Naona hamas wameamua kumtolea Allah sadaka ya wenzao walioamua kutetea nafsi zao. Hayo magaidi yameleta dhahama sana hapo Gaza.
 

Hiyo video haina viashiria vilivyodhibitika kuonesha kuwa kombora lilitoka ardhini likafeli.vIdeo kama hiyo watoto wa mtaani wana uwezo wa kuitengeneza.ukiangalia vizuri hakuna sehemu ya kombora kutua juu ya hospitali.Badala yake inaoneshwa moto mkali ukiwaka ambao hata Ukraine mabaki wanayodai ya makombora mazito ya Urusi hayatoi moto kama huo.
Kumbuka hiyo hospitali mayahudi waliitaka ihamwe kwa siku tatu nyuma,madaktari wakagoma.
 
Kama hamas anawapenda hao watoto zaidi, si ajitokeze tu, ili awaokoe hao watu wanaouawa kisa ni yeye?!!
FB_IMG_16977776558088898.jpg
 
Kama hamas anawapenda hao watoto zaidi, si ajitokeze tu, ili awaokoe hao watu wanaouawa kisa ni yeye?!!
Hamas ni kikundi kidogo cha watu waliojihami na silaha hawana uwezo wa kupambana na jeshi la Israel mie nashangaa muisrael anapiga mabomu ovyo ovyo hajiamini kuingia gazq
 
Hamas ni kikundi kidogo cha watu waliojihami na silaha hawana uwezo wa kupambana na jeshi la Israel mie nashangaa muisrael anapiga mabomu ovyo ovyo hajiamini kuingia gazq
Njia wanayotumia ya kujificha kwenye makazi ya watu, ndio inayoleta maafa, kwa watu, na sio kwamba anapiga mabomu hovyo tu, bali ni target zake hizo, lasivyo si angekuwa ameimaliza Gaza yote?!! Muda ukifika ataingia tu
 
Back
Top Bottom