Kanjanja

cuth_luxy

Member
Joined
Apr 29, 2013
Posts
15
Reaction score
21
Wadau wa lugha, ivi hili neno ni msamiati rasmi ama ni neno lililoibuka tu kuwatambulisha waandishi wazamiaji au linaweza kutumika kwa mtu yeyote?
 
Mimi nadhani limezuka tu, halimo kwenye kamusi.
 
Wadau wa lugha, ivi hili neno ni msamiati rasmi ama ni neno lililoibuka tu kuwatambulisha waandishi wazamiaji au linaweza kutumika kwa mtu yeyote?
Kwa mara ya kwanza hili neno nililisikia kutoka kwa prof. (kabla halijasikika mitaani wala kwenye tv) aliyekuwa anatufundisha kozi ya Lexicography; alisema Kanjanja ni mtu anayefanya kazi asiyokuwa na taaluma nayo. Alilitumia neno kanjanja alipokuwa anajaribu kufafanua jinsi kamusi zinavyoundwa....ndipo akasema..."Kuna kamusi huko mtaani zinauzwa lakini zimetengenezwa na makanjanja" akiwa na maana kwamba hao watu hawana taaluma ya uundaji kamusi (Lekskografia). Kwa hiyo nafikiri hili ni neno la kiswahili sanifu.
 
ni neno sanifu lilosanifiwa hivi karibuni hasa kwa kuona matumizi yake ni sahihi ( mwandishi wa habari asiye na taaluma)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…