Kanuni kali ikiwepo kunyang'anya pointi timu inayofanya au kuwa na viashiria vya ushirikina ni za lazima

Kanuni kali ikiwepo kunyang'anya pointi timu inayofanya au kuwa na viashiria vya ushirikina ni za lazima

Cashman

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2018
Posts
3,017
Reaction score
5,294
Nimesikia mwenyekiti wa bodi ya ligi akigusia uandwaaji wa kanuni kali.

Naunga mkono kanuni ziwe kali zaidi hususan inayopiga vita ushirikina katika soka. Hatutaki kuona mazingaombwe uwanjani bali vijana wacheze soka halali.

Tabia ya kuvunja makufuli ya mageti,kuruka ukuta na ujinga mwingine kama huo haukubaliki. Adhabu iwe kunyang'anywa pointi na hata ukifumgwa unakatwa pointi nyingine tatu kwenye alama ulizo nazo.

Hii ni kukomesha kabisa biashara ya mazonge zonge kwenye soka
 
Hivi Taasisi kama TFF imakomaa kuongelea ushirikina.

Ushirikina ni jambo ambalo huwezi kuthibitisha.

Hizi ni tamaduni zetu mbona wazungu wanafanya mambo ya ovyo kwenye mpira tunaona ni usasa
 
Hivi Taasisi kama TFF imakomaa kuongelea ushirikina.
Ushirikina ni jambo ambalo huwezi kuthibitisha.
Hizi ni tamaduni zetu mbona wazungu wanafanya mambo ya ovyo kwenye mpira tunaona ni usasa
Tatizo ni pamoja na watu wanaofikiri kama wewe
 
Ni aibu mpaka Karne hii timu bado zinaendekeza Imani za kishirikina, kuzitoza faini haisaidii.
Hayo masuala ni imani ya mtu. Kuna wachezaji wakiaingia uwanjani wanapiga ishara ya msalaba wengine wakifunga goli wanapiga makoti na kuinama kama wanavyofanya waislamu wakati wa kuswali na haionekani ni shida, as long as mtu hasababishi hatari au usumbufu kwa wengine basi kila mmoja abaki na imani yake.
Mtu akivaa rozali ni sawa ila akivaa hirizi kelele kibao wakati kimsingi lengo la hao wote ni moja wametofautiana imani tu.
 
Hayo masuala ni imani ya mtu. Kuna wachezaji wakiaingia uwanjani wanapiga ishara ya msalaba wengine wakifunga goli wanapiga makoti na kuinama kama wanavyofanya waislamu wakati wa kuswali na haionekani ni shida, as long as mtu hasababishi hatari au usumbufu kwa wengine basi kila mmoja abaki na imani yake.
Mtu akivaa rozali ni sawa ila akivaa hirizi kelele kibao wakati kimsingi lengo la hao wote ni moja wametofautiana imani tu.
Hatutaki kusikia mtu anavunja geti,au anamwaga unga uwanjani au anafukua taulo la kipa.Hivi vitendo na vingine kama hivyo vinapaswa kutovumiliwa
 
Hatutaki kusikia mtu anavunja geti,au anamwaga unga uwanjani au anafukua taulo la kipa.Hivi vitendo na vingine kama hivyo vinapaswa kutovumiliwa
Huu ndo utamu wa soka . Shirikisho halina hata viwanja 10 vya mpira safi mnawaza uchawi .


Amna app , media nzuri , mashabiki , coverage ya 4k , var

Mnawaza uchawi 🚮🚮 . Bodi nzima amna akili
 
Mwenyekiti wa bodi, mpira wetu una maeneo ya msingi sana yanayohitaji marekebisho kabla ya hili, waamuzi, viwanja vibovu, utaratibu wa team zinashuka daraja zinacheza play off tena na team za chini n.k haya ya ushirikina ni madogo sana.
 
Hayo masuala ni imani ya mtu. Kuna wachezaji wakiaingia uwanjani wanapiga ishara ya msalaba wengine wakifunga goli wanapiga makoti na kuinama kama wanavyofanya waislamu wakati wa kuswali na haionekani ni shida, as long as mtu hasababishi hatari au usumbufu kwa wengine basi kila mmoja abaki na imani yake.
Mtu akivaa rozali ni sawa ila akivaa hirizi kelele kibao wakati kimsingi lengo la hao wote ni moja wametofautiana imani tu.
Malengo ya Rozali na Hirizi ni tofauti kabisa.
 
Bodi ya Ligi, TFF, waandishi wa habari za michezo na wapenzi wa soka wanaacha kushughulika na mambo ya msingi kwenye soka wanahangaika na imani za watu kana kwamba mchezo wa soka upo kwa nia ya kuhubiri dini.
Soka la Tanzania linaendeshwa na viwango vya juu sana vya rushwa.
Maofisa wa TFF na bodi ya ligi wanajua, marefarii wanajua na waandishi wa habari wanajua.
Mchezo wa soka Tanzania unazalisha matokeo bandia.
Na hatujafanya chochote kusafisha rushwa kwenye mchezo huu.
Acheni watu waamini wanachoamini safisheni rushwa kwenye soka
 
Hivi Taasisi kama TFF imakomaa kuongelea ushirikina.

Ushirikina ni jambo ambalo huwezi kuthibitisha.

Hizi ni tamaduni zetu mbona wazungu wanafanya mambo ya ovyo kwenye mpira tunaona ni usasa
TFF wamepotoka
 
Back
Top Bottom