Kanuni za mpira tulipokuwa watoto

Fakyuol

Senior Member
Joined
Nov 26, 2023
Posts
148
Reaction score
325
Kanuni za mpira tulipokuwa watoto:

1. Mtoto mnene daima alikuwa mlinda mlango.

2. Mmiliki wa mpira ndiye anayeamua na niacheza.

3. Kama hukushiriki kutengeneza mpira, huchezi mechi.

4.Mwenye mpira akikasirika, mchezo unakwisha.

5. Ukigonga vidole vyako kwenye jiwe na damu inatoka, unafunika eneo la jeraha kwa mchanga kama huduma ya kwanza na mchezo unaendelea.

6. Humpigi chenga sana mmiliki wa mpira, hii inaweza kumsababishia kuchukua mpira wake na kumaliza mchezo.

7. Hakuna kuotea.

8. Hakuna refa.

9. Kuna kosa tu ikiwa kosa ni kubwa.

10. Wachezaji bora wawili hawawezi kuwa kwenye timu moja, kila mtu anachagua wachezaji wake.

11. Mchezaji bora uwanjani daima yupo kwenye timu moja na mmiliki wa mpira.

12. Daima kuna nyumba ambapo mpira ukidondoka huko, tulijua mchezo umemalizika. Hivyo lazima mjilinde usiende huko mpira!

13. Kutofautisha timu, moja ya timu inavua mashati yao.

14. Mchezo unamalizika wakati wa giza na hatuoni mpira vizuri, tunatawanyika katika makundi tukichekeshana hadi tunapofika nyumbani kukutana na adhabu nyingine kutoka kwa wazazi wetu. [emoji23][emoji23]

Utoto raha sana aisee!

C&P [emoji2398]owner
 

Dah umenikumbusha mbali sana ingawa iyo namba 2 mimi sikuwahi kuchagua wachezaji bali kuna jamaa mmoja alikuwa kipanga sana kwa uchezaji alikuwa akipenda kucheza na mimi ingawa kwa sisi wachezaji wazuri tulikuwa wengi kwaiyo ilikuwa changamoto kuchaguana
 
1. Mtoto mnene daima alikuwa mlinda mlango.

2. Mmiliki wa mpira ndiye anayeamua na niacheza.

3. Kama hukushiriki kutengeneza mpira, huchezi mechi.

4.Mwenye mpira akikasirika, mchezo unakwisha.

5. Ukigonga vidole vyako kwenye jiwe na damu inatoka, unafunika eneo la jeraha kwa mchanga kama huduma ya kwanza na mchezo unaendelea.

6. Humpigi chenga sana mmiliki wa mpira, hii inaweza kumsababishia kuchukua mpira wake na kumaliza mchezo.

7. Hakuna kuotea.

8. Hakuna refa.

9. Kuna kosa tu ikiwa kosa ni kubwa.

10. Wachezaji bora wawili hawawezi kuwa kwenye timu moja, kila mtu anachagua wachezaji wake.

11. Mchezaji bora uwanjani daima yupo kwenye timu moja na mmiliki wa mpira.

12. Daima kuna nyumba ambapo mpira ukidondoka huko, tulijua mchezo umemalizika. Hivyo lazima mjilinde usiende huko mpira!

13. Kutofautisha timu, moja ya timu inavua mashati yao.

14. Mchezo unamalizika wakati wa giza na hatuoni mpira vizuri, tunatawanyika katika makundi tukichekeshana hadi tunapofika

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ujakoseaa mzee sahihi kabsaa sikupingi
 
You remind me those days, hata maisha hayakuwa magumu sana.
 
Sisi left leg lazima utungwe jina ( guu la mavi,mashoto etc) jina langu naitwa Prince..watoto wenzangu walikuwa wanafananisha jina langu na la mchezaji wa zamani wa Yanga alikuwa anaitwa Primus Kasonso .. walikuwa wakiniita Kasonso..miaka imekimbia sana.
 
Andiko kama lako limetrend sana tokea kitambo na Uzi humu ulishawahi kuwepo , anyway inaburudisha sana ..
 
15. Hurusiwi kutumia ndole ,unaharibu Mpira na mwenye Mpira anaweza kukutoa nje.๐Ÿ˜ƒ๐Ÿ™Œ
16.
Mimi nilikuwa napata tabu sana mร ana Ndio ulikuwa upigaji wangu halafu karibia kila mtaa kupiga madochi ni kosa kubwa sana.
 
Watoto wa siku hizi hakuna mambo hayo zamani chandimu ilikuwa chandimu kweli haswa mitaa ya Yombo ilikuwa kama vita mitaa kwa mitaa ikikutana .
 
Ukitolewa ukagoma kutoka unaiwa chakula, maana yake timu yako imetoa rukhsa uchezewe rafu.
Hivyo utachezewa rafu hatakama haujagusa mpira.
Hii mbaya sana ,mtaani kwetu ilikuwa inatangazwa kuwa fulani nyama hapo ukigoma kutoka kama mnyonge utapigwa rafu na mabuti mpaka utatoka mwenyewe..
 
Mtaani kwetu ilikuwa tulicheza Chandimu mida ya jioni kabisa watu wamechoka ilikuwa inatangazwa kuwa sasa ni muda wa shaolin soccer ili kama mtu hauwezi shoo atoke mapema hapo ni full mabuti hakuna lawama..
 
Namba 12 imenikubusha mbali sana kwa Mzee mmoja nyuma ya goli la kaskazini aliweka fensi ya mabati kuzunguka nyumba yake ,basi ikawa mashuti yetu yalikuwa yanapiga mabati yake na kumletea kero .Mpira bahati mbaya ukidumbukia kwake basi hakuna kuupata mechi imeisha hapo ikiwa kero sometimes boli lipo kwenye burudani ya hali ya ghafla Vibe linaisha mpira ukiingia huko tunabaki tumekasirika Tu .

Kuna uwanja mmoja dirisha la mwamba mmoja lipo nyuma ya goli tulichana mpaka nyavu kwa mashuti ,na sometimes mpira penya dirishan mpaka ndani ikiwa jamaa mwembamba kuliko wote alikuwa anaitwa Tom kazi yake yeye ni kupenya katikati ya Nondo kufuata mpira . Baada ya mwamba kugundua ikawa akirudi safari zake akikuta watu Wanacheza mpira ni kuwatoa Balu na ikawa akitoka Tu watu hakuna kuuliza ni mbio Tu mpk wengine wanaacha viatu sometimes mpira.
 
Kosa kubwa lilikuwa kushika Mpira sisi tuliita "Enzi" sijui nyie.
 
Utoto raha sana aisee!
Disorganized football.
Sijui kama ni raha. Kumbeleza mwenye mpira na kuweka mchanga kwenye vidonda.

Haijatusaidia lolote kwenye mpira wa dunia. Wenzetu hawana hizi practice za toka utotoni na bado wanatushinda.

We were neglected children. Tulitelekezwa. Ulaya baba yake mtoto mmoja angekuja kuwa kocha, refa, au kutu organize tusicheze kama vitoto vya nyani na kuumizana na msiweke michanga kukausha vidonda. Sisi tulikuwa wenyewe wenyewe tu, nobody's father gave a flying fvuk about none of us. Na mpira hatujui mpaka kesho.

Siku nyingine mnaenda kucheza mpira bichi. Na mnaogelea. Hakuna cha life guards wala cha life vests. Fatally risky plays. Parents didn't give a shit, they were absolute dunderheads.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ