Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,771
- 41,027
Kazimwaga zake sera, ilani kanipatia,
Kaniomba zangu kura, moyo kuuchagulia,
Imekuwa werawera, nia kanitangazia,
Kapita bila kupingwa, ni mgombea pekee!
Bila ya kuchakachua, mgombea kajinadi
Ahadi nimechambua, nimeshindwa ukaidi,
Mwishoni nimeamua, ni mgombea stadi,
Kapita bila kupingwa, ni mgombea pekee![/QOUTE]
Hahitaji chakachua, kuuwini wako moyo
Tayari alijifua, kuukabili wako moyo
Alijua tachukua, jimbo la wako moyo
Wastahili pongezi, kupapa mtu shujaa
Kura nimempatia, asubiri kuapishwa,
Wengine wamekimbia, yeye pekee kapishwa,
Hongera nampatia, wote mtafurahishwa,
Kapita bila kupingwa, ni mgombea pekee!!
By. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)
Mgombea Pekee!
Kura siingeweza mnyima, ni stadi mashuhuri
Ameuweza mtima, akapanga ushauri
akajitoa mazima, kunasa wako uturi
Hongera zake hongera, mgombea wa pekee
Kila la heri kaka..........
Wastahili pongezi, wa kijiji nakwambia
Ni wazi umemuenzi, sera zake kutambia
Aliupanga utenzi, kura zako kuomnea
Umechagua sawia, Mgombea anofaa
Bila ya kuchakachua, mgombea kajinadi
Ahadi nimechambua, nimeshindwa ukaidi,
Mwishoni nimeamua, ni mgombea stadi,
Kapita bila kupingwa, ni mgombea pekee![/QOUTE]
Hahitaji chakachua, kuuwini wako moyo
Tayari alijifua, kuukabili wako moyo
Alijua tachukua, jimbo la wako moyo
Wastahili pongezi, kupapa mtu shujaa
Kila la heri kaka..........
Kumbe MJ1 na wewe wamo lakini HAWAVUMI ............. :happy: