Kapteni Ibrahim Traore azindua kiwanda cha kusindika nyanya

Kapteni Ibrahim Traore azindua kiwanda cha kusindika nyanya

Strong ladg

Senior Member
Joined
Jul 15, 2021
Posts
170
Reaction score
445
Rais wa Burkina Faso Kapteni Ibrahim Traore amezindua kiwanda cha kusindika nyanya kilichopo katika mji wa Bobo-Dioulasso.

Uzinduzi wa kiwanda hicho umefanyika leo tarehe 30 Novemba 2024 . Kiwanda hicho chenye uwezo wa kuchakata tani 6 za nyanya kwa saa moja, kinatazamiwa kuiwezesha nchi hiyo ya Afrika magharibi kukabiliana na tatizo la upotevu mkubwa wa nyanya baada ya mavuno uliotokana na ukosefu wa kiwanda cha kusindika zao hilo.

Fedha za kujenga kiwanda hicho zilitolewa na wananchi wa Burkina Faso kupitia mpango wa ununuzi wa hisa uliowezesha hata wananchi wa kipato cha chini kuwa sehemu ya umiliki wa kiwanda hicho.

Viwanda vingine viwili kama hicho vinajengwa katika miji mingine na vinatarajiwa kuwa tayari kuanza uzalishaji hapo mwakani.

Nchi ya Burkina Faso ni ya pili kwa uzalishaji wa nyanya katika nchi za Afrika magharibi nyuma ya Nigeria na huuza nyanya nje ya nchi hasa katika nchi za Bénin na Ghana.

Katika hotuba yake wakati wa uzinduzi, Kapteni Traore aliwashukuru raia wa Burkina Faso kwa kuitikia mpango wa ununuzi wa hisa uliowezesha kupatikana kwa fedha zilizowezesha ujenzi wa kiwanda hicho ambacho ni alama ya maono waliyonayo ya kuwezesha upatikanaji wa maendeleo kwa raia wote wa Burkina Faso.Pia alisema kwamba anaamini nchi ya Burkina Faso ina raslimali muhimu zinazohitajika ili kuiletea usitawi na maendeleo nchi hiyo.

CHANZO/ SOURCE:Shirika la habari la Burkina Faso (RTB)

20241130_183719.jpg
20241130_183721.jpg
20241130_140459.jpg
 
Hivi kwa mfumo wa hisa watanzania si tujenge cha matairi size zote tuhudumie East na Central Africa.
 
Tungekuwa na viongozi wenye maono, tungekuwa mbali kama taifa, wangetuibia lakini bado tungekuwa mbali mnoo, hawa wanatuibia lakini BICHWA ni empty set. Hakuna la maana linafanyika.. Juzi tu mtu kaleta uziwa fursa za mtwara kwa haraka haraka kuna hitajika viwanda kama viwili ama vi3, ila kwa kuwa ni EMPTY BOX hawawezi kuona.
 
Rais wa Burkina Faso Kapteni Ibrahim Traore amezindua kiwanda cha kusindika nyanya kilichopo katika mji wa Bobo-Dioulasso.

Uzinduzi wa kiwanda hicho umefanyika leo tarehe 30 Novemba 2024 . Kiwanda hicho chenye uwezo wa kuchakata tani 6 za nyanya kwa saa moja, kinatazamiwa kuiwezesha nchi hiyo ya Afrika magharibi kukabiliana na tatizo la upotevu mkubwa wa nyanya baada ya mavuno uliotokana na ukosefu wa kiwanda cha kusindika zao hilo.

Fedha za kujenga kiwanda hicho zilitolewa na wananchi wa Burkina Faso kupitia mpango wa ununuzi wa hisa uliowezesha hata wananchi wa kipato cha chini kuwa sehemu ya umiliki wa kiwanda hicho.

Viwanda vingine viwili kama hicho vinajengwa katika miji mingine na vinatarajiwa kuwa tayari kuanza uzalishaji hapo mwakani.

Nchi ya Burkina Faso ni ya pili kwa uzalishaji wa nyanya katika nchi za Afrika magharibi nyuma ya Nigeria na huuza nyanya nje ya nchi hasa katika nchi za Bénin na Ghana.

Katika hotuba yake wakati wa uzinduzi, Kapteni Traore aliwashukuru raia wa Burkina Faso kwa kuitikia mpango wa ununuzi wa hisa uliowezesha kupatikana kwa fedha zilizowezesha ujenzi wa kiwanda hicho ambacho ni alama ya maono waliyonayo ya kuwezesha upatikanaji wa maendeleo kwa raia wote wa Burkina Faso.Pia alisema kwamba anaamini nchi ya Burkina Faso ina raslimali muhimu zinazohitajika ili kuiletea usitawi na maendeleo nchi hiyo.

CHANZO/ SOURCE:Shirika la habari la Burkina Faso (RTB)

View attachment 3165953View attachment 3165954View attachment 3165955
Sifa kwenye tuvitu twa kijinga zimezisi,hii ndio shida ya wajamaa mbuzi.

Nchi nyingi zinafanya mambo makubwa kuanzia Ivory Coast,Tanzania Hadi Benin lakini huwezi simia masifa ya kipumbavu kama huko Burkinabe

View: https://x.com/AfricaFactsZone/status/1897345565358162154?t=M_d561pMYAqpsiOUUDlHrQ&s=19
 
Back
Top Bottom