Manyanza
JF-Expert Member
- Nov 4, 2010
- 16,464
- 35,629
Kiongozi wa Burkina Faso, Ibrahim Traoré amepiga marufuku majaji kuvaa mawigi yanayofanana na mitindo ya kikoloni ya Uingereza na Ufaransa, ikiwa ni juhudi za kuondoa athari za ukoloni kwenye mfumo wa mahakama wa taifa hilo.
Mawigi hayo yalianzishwa na wakoloni kama sehemu ya mavazi rasmi ya mahakama ili kuashiria mamlaka, utulivu, na heshima na baada ya ukoloni kumalizika, baadhi ya nchi za Afrika zimeendeleza matumizi ya mawigi hayo katika mifumo yao ya kisheria.