KERO Kariakoo kuna chemba zinatema maji machafu na kuhatarisha afya za Watu, Viongozi wapo kimya

KERO Kariakoo kuna chemba zinatema maji machafu na kuhatarisha afya za Watu, Viongozi wapo kimya

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Nyakijooga

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2018
Posts
276
Reaction score
473
kari.jpg

Licha ya kutambulika wazi kwamba Kariakoo ni sehemu muhimu ya kibiashara ambayo inajumuisha shughuli mbalimbali ambazo zinafanya kuwa chanzo nyeti cha mapato nchini, lakini nashangazwa na mamlaka kushindwa kuwajibika kuzingatia usafi wa mazingira katika eneo hilo.

Ni zaidi ya Wiki mbili sasa kuna chemba zinatema maji machafu na taka, jambo la kusikitisha chemba hizo zinatililisha uchafu huo kwenye maeneo ambayo watu wanapita pamoaja na magari.

kari1.jpg

Lakini kibaya zaidi unakuta pembeni mwa barabara watu wamepanga bidhaa za chakula huku maji ya machafu yanayotimuliwa na magari yakidondokea vitu hivyo, jambo ambalo ni hatari kwa walaji, mfano eneo la njia panda karibia na Soko(Mtaa wa Pemba) na Mtaa na Mtaa wa Nyamwezi ambako Watu wanapanga chini matunda na viungo vya vyakula.

Soma Pia: Kituo cha Mwendokasi Kimara acheni kutiririsha maji machafu usiku

Hali hiyo sio rafiki na imekuwa endelevu kwa kujitokeza mara kwa mara, siwezi kukaa kimya kwa sababu tunao Viongozi wa Jiji ambao wanatakiwa kusimamia mambo kama hayo, najiuliza viongozi wetu hao kama wameweza kuweka Watu wa kukusanya ushuru kila siku, iweje sasa wakose taarifa za chemba kuhatarisha afya za Watu.

kari2.jpg

Kushindwa kuweka eneo la Kariakoo katika mazingira salama ni sawa na kutuma meseji kwa Watu kwamba wasije eneo hilo au waje kwa tahadhari zaidi.
 
Licha ya kutambulika wazi kwamba Kariakoo ni sehemu muhimu ya kibiashara ambayo inajumuisha shughuli mbalimbali ambazo zinafanya kuwa chanzo nyeti cha mapato nchini, lakini nashangazwa na mamlaka kushindwa kuwajibika kuzingatia usafi wa mazingira katika eneo hilo.

Ni zaidi ya Wiki mbili sasa kuna chemba zinatema maji machafu na taka, jambo la kusikitisha chemba hizo zinatililisha uchafu huo kwenye maeneo ambayo watu wanapita pamoaja na magari .

Lakini kibaya zaidi unakuta pembeni mwa barabara watu wamepanga bidhaa za chakula huku maji ya machafu yanayotimuliwa na magari yakidondokea vitu hivyo, jambo ambalo ni hatari kwa walaji, mfano eneo la njia panda karibia na Soko(Mtaa wa Pemba) na Mtaa na Mtaa wa Nyamwezi ambako Watu wanapanga chini matunda na viungo vya vyakula.

Hali hiyo sio rafiki na imekuwa endelevu kwa kujitokeza mara kwa mara, siwezi kukaa kimya kwa sababu tunao Viongozi wa Jiji ambao wanatakiwa kusimamia mambo kama hayo, najiuliza viongozi wetu hao kama wameweza kuweka Watu wa kukusanya ushuru kila siku, iweje sasa wakose taarifa za chemba kuhatarisha afya za Watu.

Kushindwa kuweka eneo la Kariakoo katika mazingira salama ni sawa na kutuma meseji kwa Watu kwamba wasije eneo hilo au waje kwa tahadhari zaidi.
Wako busy na matamasha ya kuntukuza mtu huko kwa mauzinde
 
Hapa ndio unaona namna mfumo wetu unavyozalisha watu tegemezi kwa sababu kwa kariakoo hizo brain zilizoko hapo hakuna tatizo zitashindwa kutatua zikiungana ila hata mbwa akifa watu watangoja mamlaka na bad enough ni wao wenyewe ndio wameharibu chemba
Ustaraabu uanze na sisi
 
Hapa ndio unaona namna mfumo wetu unavyozalisha watu tegemezi kwa sababu kwa kariakoo hizo brain zilizoko hapo hakuna tatizo zitashindwa kutatua zikiungana ila hata mbwa akifa watu watangoja mamlaka na bad enough ni wao wenyewe ndio wameharibu chemba
Ustaraabu uanze na sisi
Wamelipa Kodi na tozo ya mazingira. Ni wajibu wa wakusanya Kodi na tozo kukarabati migumo ya maji taka.
 
Maghorofa hayaendani na mfumo wa maji taka wa kale. Hivi hayo maji taka huwa yanatritiwa au huenda moja kwa moja baharini?
 
Ni balaa mpaka kichefu chefu maana yaan nimeshuhudia mitaa mingi hapa kariakoo ikiwa inanuka sanaa

All in all Kuna ambao wamezoea HARUFU izo mpaka wanaona normal na wanakula KABISA
 
For sure kariakoo haina miundombinu thabit ukilinganishw na hadhi inayopew.sahiv jua linawak kipind Cha mvua sas ndo hapatamanik
 
Last time tulfatilia hili.....tulimshitikisha mtendaj na viongoz baadhi......kulkua na changamoto kadhaaa.....ila kutakua solved naamini
 
Back
Top Bottom