Karo mpya UDSM zimezingatia nini?

Karo mpya UDSM zimezingatia nini?

Katufu

JF-Expert Member
Joined
May 8, 2012
Posts
523
Reaction score
309
Wakuu wanaJF na wadau wote. Chuo kikuu cha Dar es Salaam kimepitia upya ada zake za masomo ya uzamili na uzamivu ambazo zinatumika kuanzia mwaka huu (2013/2014) wa masomo. Jambo la kushangaza ni kuwa karo hizo zimepanda kwa karibu au zaidi ya asilimia 100% kwa kweli nashindwa kuelewa kigezo au vigezo hasa vilivyozingatiwa ili kupandisha karo kwa viwango hivi?

Kwa mfano, mimi mwenyewe nimemaliza Postgraduate diploma in education (PGDE) hapo mlimani mwaka huu na sasa nipo nafanya teaching practice ili kukamilisha course mbili zilizobaki. Yaani CT513 na FE599. Karo ya course hii ilikuwa 1,647,500/= lakini imepandishwa na kuwa 3,250,000/=; kozi nyingine nazo mwelekeo ni huohuo. Nyingine ni admission fee ambayo ilikuwa 20,000/= lakini imepandishwa mpaka 50,000/= zaidi ya 100%. Kwa taarifa zaidi fungua attachment au fuata link hii: http://postgraduate.udsm.ac.tz/medi...aduate_Studies_Fee_Structure_Revised_2013.pdf

Wadau kwa kweli mpaka sasa nashindwa kuelewa kabisa walizingatia nini hasa? Au ndiyo suala la wasomi na viongozi wetu kuwa out of touch na wananchi? Hebu tulijadili hili suala kwa makini.

Naomba kuwasilisha.
 

Attachments

Mkuu hili ni janga. Nilipochukua barua wiki iliyopita nilitahayaruki. Je hawajui wengi wetu ni watu wa kawaida na tunajikamua tu kuhakikisha tunajitafutia elimu? Bora hata ingekuwa ni HESLB wanatudhamini tuje tuwalipe kidogo kidogo.

Hakuna sababu ya chuo cha umma kuwa na ada ndefu hivi. Kodi yangu ya kila mwezi si ndiyo inakiendesha?
 
Mkuu hili ni janga. Nilipochukua barua wiki iliyopita nilitahayaruki. Je hawajui wengi wetu ni watu wa kawaida na tunajikamua tu kuhakikisha tunajitafutia elimu? Bora hata ingekuwa ni HESLB wanatudhamini tuje tuwalipe kidogo kidogo.

Hakuna sababu ya chuo cha umma kuwa na ada ndefu hivi. Kodi yangu ya kila mwezi si ndiyo inakiendesha?

Serikali haina hela ya kuendesha chuo kwa sasa, isitoshe inajikopesha hata hela za wafanyakazi wa chuo zinazotakiwa kupelekwa kwenye Pension Funds (esp PSPF).

So badala ya serikali kuendesha chuo, chuo kinaendesha serikali.
 
mafisadi watakaaje wawajali nyinyi, waliopata wamepata waliokosa shauri yao. si umeona hata mishahara wameongezewa zaidi wenye mishahara mikubwa?

kwa namna
  • mafuta yalivyopanda
  • nauli juu
  • maisha kwa ujumla wake juu
  • sokoni bidhaa kila kitu juu
hushangai hilo, nauli zilipanda siku 100(4 months) zaidi zilizopita, wananchi hawakuwa na popote pa kujazia
gharama za kila kitu zilipanda 20% with effect 1/7/2013

who care?
 
he he he he he he he he he he da hizi ada mwenyewe zilinishtua da ila kwa staili hii watasoma wachache aisee da.....
 
ccm wameanza kukusanya hela za kampeni kwa ajili ya uchaguzi mkuu 2015
 
Lengo la serikali sikivu ni kupunguza idadi ya wasomi.
 
Back
Top Bottom