Kaskazini kwa sasa hapafai kwa Kilimo kabisa

Kaskazini kwa sasa hapafai kwa Kilimo kabisa

MURUSI

JF-Expert Member
Joined
Jun 25, 2013
Posts
4,537
Reaction score
8,824
Zamani ulikuwa huwezi taja kilimo bila kuitaja Kaskazini, mkoa kama Arusha na nazania Arusha ndio ilikuwa kituo cha kilimo Tanzania hii, Kaskazini hasa Arusha ndiko hata kulikuwa na Makao makuu ya TFA, makampuni makubwa ya mbegu yote ni Arusha na taasisi zingine.

Pia kwenye Kilimo hasa Mahindi, Ngano/Shayri, mboga mboga na Kahawa na ndizi huko ndio ilikuwa kwao.

Ila kwa miaka ya hivi karibuni naona kabisa kaskazini hasa Arusha ikiwa haifai tena kwa Kilimo kama zamani.

Ukame ikiwa ni moja ya sababu kubwa sana kwa sasa, Arusha na mikoa mingine kama Kilimanjaro na Manyara zina ukame usio isha, na sioni Dalili za hali kuja kuwa nzuri tena. Kuna Ukame mrefu sana kaskazini na bahati mbaya hakuna hata mito mikubwa ya kutumika kwa Irrigation kama mikoa mingine.

Bei kubwa ya Ardhi, kaskazini Ardhi ni ghari mno, kiasi kwamba unahitajika kuwa vizuri mno kupata shamba huko Kaskazini jamaa wali jua thamani mapema sana.

Ardhi ni chache ni haba sana kwa sasa, Ukitoa wilaya kama mbili za Kaskazini yaani Simanjro na Kiteto hakuna tena sehemu unaweza mapata mashamba kwa huko kaskazini.

Watu wanchache wana hodhi ardhi kubwa sana, Kaskazini kuna Mastle kama wale wa Zimbabwe, wana milik hekari za kutosha za Ardhi na hii inapelekea uhaba na bei kuwa juu sana.

Kwa anaye fanya kilimo simshauri huko kaskazini kwakweli binafisi napaona hapafai kabisa kwa sasa.
 
Sema huu mwaka jua limekuwa kali sana Chuga
 
Ukinunua shamba jirani yako akawa mchaga..fanya fasta weka fensi au ukuta..ukizubaa utakuta kaingia shambani mwako kajisogezea eneo lake na ukimwambia anakua mkali balaa na kukutishia kukuua..wachaga washenzi sana.

#MaendeleoHayanaChama
 
Baada ya kutenganisha mkoa wa Manyara kutoka Arusha historia ya kilimo iliishia hapo maana Manyara ilikuwa inabeba Arusha, kuhusu uzalishaji wa mazao ni mwaka huu tu ukame ulikuwa mkubwa.
Kuhusu bei ya Ardhi ni kweli mikoa ya Kazkazini ardhi haishikiki kwa bei lakini pia bei ya mazao iko juu kama ukizalisha ukilinganisha na sehemu zingine za Tanzania
 
Zamani ulikuwa huwezi taja kilimo bila kuitaja Kaskazini, mkoa kama Arusha na nazania Arusha ndio ilikuwa kituo cha kilimo Tanzania hii, Kaskazini hasa Arusha ndiko hata kulikuwa na Makao makuu ya TFA, makampuni makubwa ya mbegu yote ni Arusha na taasisi zingine.

Pia kwenye Kilimo hasa Mahindi, Ngano/Shayri, mboga mboga na Kahawa na ndizi huko ndio ilikuwa kwao.

Ila kwa miaka ya hivi karibuni naona kabisa kaskazini hasa Arusha ikiwa haifai tena kwa Kilimo kama zamani.

Ukame ikiwa ni moja ya sababu kubwa sana kwa sasa, Arusha na mikoa mingine kama Kilimanjaro na Manyara zina ukame usio isha, na sioni Dalili za hali kuja kuwa nzuri tena. Kuna Ukame mrefu sana kaskazini na bahati mbaya hakuna hata mito mikubwa ya kutumika kwa Irrigation kama mikoa mingine.

Bei kubwa ya Ardhi, kaskazini Ardhi ni ghari mno, kiasi kwamba unahitajika kuwa vizuri mno kupata shamba huko Kaskazini jamaa wali jua thamani mapema sana.

Ardhi ni chache ni haba sana kwa sasa, Ukitoa wilaya kama mbili za Kaskazini yaani Simanjro na Kiteto hakuna tena sehemu unaweza mapata mashamba kwa huko kaskazini.

Watu wanchache wana hodhi ardhi kubwa sana, Kaskazini kuna Mastle kama wale wa Zimbabwe, wana milik hekari za kutosha za Ardhi na hii inapelekea uhaba na bei kuwa juu sana.

Kwa anaye fanya kilimo simshauri huko kaskazini kwakweli binafisi napaona hapafai kabisa kwa sasa.
Kwa sasa unapendekeza kanda ipi
 
uchira ya miwaleni, kukodi ekari just kulima mahindi tu laki mbili. lima ukivuna ondoka, siyo mambo ya kukodi msimu mzima.
 
Ukinunua shamba jirani yako akawa mchaga..fanya fasta weka fensi au ukuta..ukizubaa utakuta kaingia shambani mwako kajisogezea eneo lake na ukimwambia anakua mkali balaa na kukutishia kukuua..wachaga washenzi sana.

#MaendeleoHayanaChama

Hizo ni myth tu, ukweli kuwa shamba linaweza vamiwa na yoyote regardless kabila dini au alipotoka
 
Nmekaa manyara miaka kumi nmeishia kuwa mteja wa kukod mashamba mwaka huu nmeona nijsogeze kusin! Ngjeni nikitimiza hekar 500 nitawapa mpango mzma
changamoto ya kusini unauza mazao yako kwa bei ya kimskini, labda ufanye processing mwenyewe
 
changamoto ya kusini unauza mazao yako kwa bei ya kimskini, labda ufanye processing mwenyewe
Kaka tunavyoongea hii Leo gunia la mahind Ni lak na 20 mbinga, mpunga unachezea 130000 kwa gunia, pia nchi hii kwa sasa usafrshaj sio shida ukizalisha mazao unauwezo wa kupeleka popote! Na hata wakenya wanafata mahind mbinga na songea! Mambo y kukosa Bei ilkuwa siku za nyuma! Maisha Ni kuchagua tu atakaeona kaskazn anapata manufaa akomae mim nmechemka huko
 
Achana na kulima, jichukulie stores uhifadhi ni nzuri kuliko mbilinge mbilinge za kulima kama unataka faida
 
Hao ni wafugaji ndio wanaharibu mazingira kutokana kuweka mifugo mingi eneo moja na kuharibu uoto wa asili.

Tazama maeneo ambayo wamepita jamii za wafugaji utagundua zinabadilika na kuwa kame.

Sasa hivi wafugaji unaona wanasafiri wakuja mikoa ambayo hakuna shughuli za ufugaji kuswaga kama Mtwara, tanga, morogoro, Mbeya na kwingineko.

Sasa wameharibu hiyo mikoa saa hii wanasafiri kuelekea mikoa mingine na kuharibu kama walivyoharibu mazingira mikoa waliyotoka

Wafugaji wadhibitiwe. Wapunguze idadi ya mifugo au wakae sehemu moja, waanze kulisha mifugo kisasa na kufanya zero grazing.
 
Baada ya kutenganisha mkoa wa Manyara kutoka Arusha historia ya kilimo iliishia hapo maana Manyara ilikuwa inabeba Arusha, kuhusu uzalishaji wa mazao ni mwaka huu tu ukame ulikuwa mkubwa.
Kuhusu bei ya Ardhi ni kweli mikoa ya Kazkazini ardhi haishikiki kwa bei lakini pia bei ya mazao iko juu kama ukizalisha ukilinganisha na sehemu zingine za Tanzania
Aisee ni miaka 2 mfululizo Sasa Manyara mvua za kulrnga na manati, jàna nimeshuhudia mtu anavina mabua ya mahindi Babati...inasikitisha sana!
Hata Kilimo Cha mpunga Magugu kimeathirika sana..hali ni hiyo Kwa miwa,karanga na mazao mengine,ikiwemo maharagr!
 
Back
Top Bottom