Kasulu: Chawa wengi waonekana darasani

Kasulu: Chawa wengi waonekana darasani

brucella

Member
Joined
Mar 15, 2019
Posts
74
Reaction score
77
Nawasalimia kwa jina la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Unaposikia duniani kuna mengi, kweli mengi yapo. Mengine ni ngumu kuyapatia ufumbuzi hususa kwa akili ya kawaida ya kibinadamu inapotumika.

Kwa sababu kuna matukio ambayo huwaga yanatokea inakuwa ngumu kuyaelewa labda uwe na nguvu ya ziada ya kiMungu au kishetani.

Wale waliokulia kwenye familia za kimasikini pamoja na vijijini wamewahi kukumbwa na tatizo la chawa, na pia kuna baadhi ya maeneo hususa kipindi cha nyuma ambayo ilisharipotiwa kuwa na chawa wengi sana, lakini pia hata sasa wale ambao hawazingatii usafi wa nguo wanaweza wakapata chawa.

Katika Hali ya kushangaza kuna tukio moja limetokea katika Kijiji cha Kabanga halmashauri ya mji Kasulu - Kigoma 30/4/2021 asubuhi, chawa wengi mno kuonekana darasani.

Msimuliaji anasema katika darasa hilo, siku ya Jana yake jioni darasa limefanyiwa usafi vizuri na wanafunzi maana lilikuwa linaandaliwa kwa ajili ya mtihan na pia ndoo darasa hilo linalotumika siku zote na darasa 7.

Anaendelea kusema, wanafunzi kama kawaida waliingia darasani asubuhi mmoja ya wanafunzi akakuta kuna kama kichuguu kikubwa cha chawa kimetengenezwa ndani karibu na sehemu anapokaa, akajaribu kukigusa basi hapo ndoo ikawa shughuli, wale chawa walisaambaa darasa zima ikabidi wanafunzi waanze kupiga makelele huku wakikimbia nje.

Ndipo walimu wakaja wakakuta chumba kizima kimejaa chawa, madaftari ya wanafunzi yamejaa chawa, na baadhi ya wanafunzi wameshapata chawa hali ambayo watu walishindwa kuielewa kwa sababu kila mmoja alizungumza la kwake. Kutokana na Hali hiyo ilibidi darasa zima lipuliziwe dawa ili kuwaua chawa. Ni tukio ambalo limekuwa gumzo kijijini hapo.

Wataalamu wa Mambo mtusaidie hilo tukio unaweza ukalielezaje? Maana watu humu JF tunatofautiana. Kina Mshana jr na wengine karibuni sana.

Naomba kuwasilisha.
 
Mkuu Ni Shule Ipi hapo?? Maana Ipo Kabanga Mazoezi Lugoyi Tulashashe na Nyingine Nimezisahau. Ila Kuna Shule Mojawapo Hapo ina Historia Ya Matukio yasiyoeleweka nakumbuka Miaka Ya 2008 Nikiwa Huko
 
Chawa ni wadudu tu. Wabongo watasema ni wa kichawi. Mwingine anasema eti kuna mtu alishikwa na debe la Nairobi fly/Narrow bee sijui.

Muafrika kama haelewi kitu anasema ni uchawi. Mzungu anasema ni sayansi, zamani naye alikuwa anasingizia uchawi na adhabu kutoka mbinguni.
 
Kapicha jmn kuweni serious
Kwa ambao hawajui chawa kwa kiingereza anaitwa LICE
giphy.gif
 
Hayo ni mazingaombwe kweli.
Chawa wanaweza wakawepo lkn siyo wa kusambaa darasa zima
 
Hivi chawa, kunguni, viroboto, mbu, panya na nzi wanafananaje? Nisaidieni jamani. Natamani kuwaona kwa macho in person hata ning'atwe nao nami nipate experience na changamoto za ndugu zangu wa dunia ya tatu.

Nimewazoea vipepeo na ladybird.
 
Hivi huku kasulu ndio anapotokea Makamu wetu wa Raisi?
Nawasalimia kwa jina la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Unaposikia duniani kuna mengi, kweli mengi yapo. Mengine ni ngumu kuyapatia ufumbuzi hususa kwa akili ya kawaida ya kibinadamu inapotumika.

Kwa sababu kuna matukio ambayo huwaga yanatokea inakuwa ngumu kuyaelewa labda uwe na nguvu ya ziada ya kiMungu au kishetani.

Wale waliokulia kwenye familia za kimasikini pamoja na vijijini wamewahi kukumbwa na tatizo la chawa, na pia kuna baadhi ya maeneo hususa kipindi cha nyuma ambayo ilisharipotiwa kuwa na chawa wengi sana, lakini pia hata sasa wale ambao hawazingatii usafi wa nguo wanaweza wakapata chawa.

Katika Hali ya kushangaza kuna tukio moja limetokea katika Kijiji cha Kabanga halmashauri ya mji Kasulu - Kigoma 30/4/2021 asubuhi, chawa wengi mno kuonekana darasani.

Msimuliaji anasema katika darasa hilo, siku ya Jana yake jioni darasa limefanyiwa usafi vizuri na wanafunzi maana lilikuwa linaandaliwa kwa ajili ya mtihan na pia ndoo darasa hilo linalotumika siku zote na darasa 7.

Anaendelea kusema, wanafunzi kama kawaida waliingia darasani asubuhi mmoja ya wanafunzi akakuta kuna kama kichuguu kikubwa cha chawa kimetengenezwa ndani karibu na sehemu anapokaa, akajaribu kukigusa basi hapo ndoo ikawa shughuli, wale chawa walisaambaa darasa zima ikabidi wanafunzi waanze kupiga makelele huku wakikimbia nje.

Ndipo walimu wakaja wakakuta chumba kizima kimejaa chawa, madaftari ya wanafunzi yamejaa chawa, na baadhi ya wanafunzi wameshapata chawa hali ambayo watu walishindwa kuielewa kwa sababu kila mmoja alizungumza la kwake. Kutokana na Hali hiyo ilibidi darasa zima lipuliziwe dawa ili kuwaua chawa. Ni tukio ambalo limekuwa gumzo kijijini hapo.

Wataalamu wa Mambo mtusaidie hilo tukio unaweza ukalielezaje? Maana watu humu JF tunatofautiana. Kina Mshana jr na wengine karibuni sana.

Naomba kuwasilisha.
 
Back
Top Bottom