LGE2024 Katavi: Mgombea Mpanda adai amepigwa na Diwani, Polisi Kata asema hana uwezo wa kumsaidia

LGE2024 Katavi: Mgombea Mpanda adai amepigwa na Diwani, Polisi Kata asema hana uwezo wa kumsaidia

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607

Mgombea wa nafasi Mwenyekiti wa Kijiji cha Kabwaga, Kata ya Mwamkulu Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi, Helman Lutambi Mzee amesema Novemba 27, 2024 siku ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa amedai kupigwa na Diwani wa Kata hiyo, Kalipi Katani na kumsababishia maumivu makali mwilini mwake.

Ameeleza licha ya kuchukua hatua ya kwenda kutoa taarifa kwa polisi kata alijibiwa na polisi kata hayo kuwa hana uwezo wa kumsaidia kwa sababu zoezi hilo liko juu ya uwezo wake.

Mzee ametoa malalamiko hayo akisisitiza kuwa kitendo cha kupigwa kilikuwa na nia ovu ya kufifisha juhudi zake za kufanya ufuatiliaji wa haki na uwazi ili kudhibiti njama zozote za hujuma.

Pia, soma: LIVE - LGE2024 - Special Thread: Matukio ya Rafu za Uchaguzi na Malalamiko kwenye Zoezi zima Uchaguzi Serikali za Mitaa
 
Hao wafuasi wa chadema wako wapi? inakuwaje diwani moja analeta vurugu alafu wao wanamwangalia?je kwnn yeye hakujibu?
 
Polisi wamekanusha, wanasema taarifa imetiwa chumvi.

Dawa ya uovu wa ccm ni kuchapana tu.
 
Ndani ya manispaa kuna mwenyekiti wa kijiji......hiyo mpya mleta mada
 

Mgombea wa nafasi Mwenyekiti wa Kijiji cha Kabwaga, Kata ya Mwamkulu Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi, Helman Lutambi Mzee amesema Novemba 27, 2024 siku ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa amedai kupigwa na Diwani wa Kata hiyo, Kalipi Katani na kumsababishia maumivu makali mwilini mwake.

Ameeleza licha ya kuchukua hatua ya kwenda kutoa taarifa kwa polisi kata alijibiwa na polisi kata hayo kuwa hana uwezo wa kumsaidia kwa sababu zoezi hilo liko juu ya uwezo wake.

Mzee ametoa malalamiko hayo akisisitiza kuwa kitendo cha kupigwa kilikuwa na nia ovu ya kufifisha juhudi zake za kufanya ufuatiliaji wa haki na uwazi ili kudhibiti njama zozote za hujuma.

Pia, soma: LIVE - LGE2024 - Special Thread: Matukio ya Rafu za Uchaguzi na Malalamiko kwenye Zoezi zima Uchaguzi Serikali za Mitaa
Poleni kwa masaibu hayo.
 
Back
Top Bottom