Kati ya mpangaji na mwenye nyumba, nani anayeruhusiwa kuvunja mkataba

Kati ya mpangaji na mwenye nyumba, nani anayeruhusiwa kuvunja mkataba

EDWINI

Member
Joined
Apr 27, 2013
Posts
36
Reaction score
3
Mpangaji mwenzangu alilipa kodi ya miezi sita, kumbe pale kuna mauzauza kibao yani uchawi. Suspect ni mwenye nyumba madharau, matusi kibao na vijana wake baada ya huyo mpangaji kuyasema bayana wakataka kumrudishia kodi ya miezi 3 iliyobaki kwa kukata pesa za umeme na maji ili aondoke.

Anayevunja mkataba ni mwenyenyumba?

Nimeshindwa nimsaidiaje please tupe njia maana hata yeye sheria hajui.
 
Wote wawili wana haki ya kuvunja mkataba isipo kuwa yule anae taka kubunja mkataba ni lazima aingiliwe maana kisheria kuvunja mkataba ni kusababisha usumbufu,hivyo mpangaji ana haki ya kuvuunja mkataba hali kadhalika na mwenye nyumba anahaki ya kuvunja mkataba isipo kuwa katika uvunjaji huo wa mkataba itazingatia zaidi mkataba wenu wa awali wakati wa kupangishana una semaje endapo mmoja kati yenu atataka kuuvunja mkataba.


NB: mkataba wowote ili utambulike kisheri ni vema zaidi ukapitia kwa wakili anaye tambulika kisheria ili kuupa mkataba wenu nguvu maana yake at list uwe umegongwa muhuri unao tambulika kisheria na mihuri inapatikana kwa wanasheria wanao tambulika kisheria.
 
Kimsinga hakuna kwenye haki kisheria kuvunja mkataba, maana kuvunja mkataba Ni kosa la madai na atakayesababisha mkataba kuvunjika atalipa fidia kwa uharibifu na hasara itakayopatika.
....pia hakuna mkataba unompa mtu haki ya kuuvunja, zaidi ya pale upande mmoja kwenda kinyume na masharti na vingezo vya mkataba.

...yeyote anaweza sahihisha
 
ni kweli.. japokuwa hausemi lakini indirect unasema kwa kuzingatia mashart yake kan yatarukw
 
Mpangaji mwenzangu alilipa kodi ya miezi sita, kumbe pale kuna mauzauza kibao yani uchawi. Suspect ni mwenye nyumba madharau, matusi kibao na vijana wake baada ya huyo mpangaji kuyasema bayana wakataka kumrudishia kodi ya miezi 3 iliyobaki kwa kukata pesa za umeme na maji ili aondoke.

Anayevunja mkataba ni mwenyenyumba?

Nimeshindwa nimsaidiaje please tupe njia maana hata yeye sheria hajui.

Hizi headache hizi zipo kibao uswazi
 
Yoyote aliye ktk mkataba huo anaweza kuuvunja either kwa njia zifuatazo;notice,surrender,disclaimer,frustration,merger e.t.c. Pia njia zote hizo lazima ziangaliwe kwa makini ili kuendana na yale yaliyoandikwa kwenye mkataba km.kuheshim clauses mf.pesa ikilipwa hairudishwi hivo loss lies where it falls
 
Back
Top Bottom