Costa hamfikii canavaro..yule mpemba kwenye kiwango chake alikua anakaba..muulize etoo na drogba..Costa kamkaba nani!?Kweli mkuu Kijuram . Costa anawazidi Canavaro na Kelvin lakini kuwa beki bora wa muda wote sidhani .
masatu na aswile unamchagua nani?Victor costa ni mashine nyingine wewe.....ila kiboko yao wote hao ni geogre masatu
Masatumasatu na aswile unamchagua nani?
Kiboko ya wote alikuwa George Masatu, baada yake hajawahi kutokea mwingine. Masatu alikuwa anawageuza washambuliaji wa timu pinzani ndani ya eneo lake la hatari.Mleta mada . Kevin na Nadir ni mabeki wazuri kwa viwango vyao ila Victor Costa ni habari tofauti kabisa . Huyo alikuwa beki kisiki na fundi haswa . Alikuwa anajiamini na kipaji kikubwa mno .
Aisee tangu miaka ya 1980 hakuna beki bora kama George Masatu, yaani alikuwa anajiamini na ball control yake ni ya hali ya juu. Jela Mtagwa, Mohammed Tall, Godwin Aswile walijitahidi ila Masatu ni mwishoAma kweli simulizi hii naifananisha na ya yule kipofu aliyebahatika kuona kwa muda ! hamad mbele yake kuna punda!!! Laiti kama ungebahatika kumuona George Masatu au Jella Mtagwa au Leodgar Tenga au hata Juma Shabani usingethubutu kuleta kichekesho chako humu!!!!.
Hahaha hapo kwenye Mibangee... [emoji23] Ndio wanaonekana Hamnazoo.Mkuu tutake radhi wanamichezo kwa kutukosea heshima.
Yaani hao akina Cannavaro ndio wawe mabeki bora wa wakati wote?
Umepata walau kusikia tu habari za akina George Magere Masatu, Jamhuri Kihwelu " Mrema ", Said Mwamba Nassoro Kizota, na wengineo?
Ukija kwa hao akina Yondani, Cannavaro na Victor Costa, ungewashindanisha kwa nafasi ya beki bora kwa miaka 10 au 15 iliyopita walau ingeleta maana mzuri.
Lakini katika hao watatu uliowataja hakuna kama Victor Costa Nampoka Nyumba! Kwangu mimi huyu ndiye Beki bora wa kati kwa miaka 15 iliyopita, alibarikiwa kipaji kikubwa sana na Muumba ikiwemo matumizi makubwa ya akili kushinda hao watumia nguvu Cannavaro na Yondani Mibange.
Niishie hapa!!