Katiba inayopendekezwa imeweka wazi misingi ya utawala bora

Katiba inayopendekezwa imeweka wazi misingi ya utawala bora

Dragunov Sniper

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2015
Posts
2,795
Reaction score
9
Mara kadhaa tumesikia kilio cha wananchi wa ngazi zote wakitaka nchi yetu iwe imara na madhubuti katika kuweka na kuzingatia utawala bora.


Katiba Inayopendekezwa katika IBARA YA 6 inaiweka wazi misingi ya utawala bora kama masharti ya kufuatwa na viongozi na watumishi wa umma.


Kuiweka misingi hii katika ibara ya 6 (na siyo ibara ya 5 inayohusu tunu za taifa) ni kuifanya iwe kipimo cha utendaji na utumishi wa umma. Huu utakuwa ni wajibu na si hiyari ya mtumishi wa umma kuamua kama anaienzi misingi hiyo au la, tofauti na kama ambavyo angeweza kuzienzi tunu zilizomo kwenye ibara ya 5, lakini zisingeweza kuchukuliwa kama kigezo cha kupima uwajibikaji na utendaji wake kwa umma endapo atashindwa kuizingatia.
 
Tunataka inayoelezea misingi ya uongozi bora, utawala bora tutawaachia wakina joka la makengeza, "Good governance vs good ruling".......BVR inapotea sababu ya utawala bora na sio uongozi bora...............
 
Tunataka inayoelezea misingi ya uongozi bora, utawala bora tutawaachia wakina joka la makengeza, "Good governance vs good ruling".......BVR inapotea sababu ya utawala bora na sio uongozi bora...............

Huna haja ya kupanic kwasababu kila kitu kiko wazi ndani ya Katiba Inayopendekezwa, ushauri wangu kwako ni kuisoma na kuielewa vema ili maswali yenye majibu wazi wazi uweze kuyapata zaidi na zaidi.
 
Back
Top Bottom