Katiba inayopendekezwa, uchaguzi mkuu utafanyika kama ilivyopangwa!

Katiba inayopendekezwa, uchaguzi mkuu utafanyika kama ilivyopangwa!

gwamaka aswile

Senior Member
Joined
Mar 26, 2015
Posts
186
Reaction score
106
Awali ya yote napenda kuwatoa wasiwasi Watanzania wenzangu ambao kwa namna moja au nyingine wamekuwa na wasiwasi kama Katiba Inayopendekezwa itapigiwa kura ya maoni na kama uchaguzi mkuu utafanyika.
Napenda kuwaambia kwamba Katiba Inayopendekezwa itapigiwa kura ya maoni na uchaguzi mkuu utafinyika kama ilivyopangwa licha ya kasoro chache zilizojitokeza.
Nimeamua kuwatoa wasiwasi Watanzania wenzangu kwa sababu wapo baadhi ya watu wamekuwa wakipiga propoganda kwamba mambo hayo hayatafanyika mwaka huu na Rais Jakaya Kikwete ataendelea kuongoza lengo likiwa ni kukiwekea mazingira mazuri Chama cha Mapinduzi kuendelea kushika madaraka.
Wapo wanaodai kitendo cha kuahirishwa zoezi la kuipigia kura ya maoni Katiba Inayopendekezwa ni moja ya mkakati huo pamoja na kutoichapisha kwa wingi katiba hiyo ili isomwe na kila Mtanzania mwenye sifa ya kupiga kura ili ieleweke.
Napenda kusema, watu hao wakiwemo viongozi wa vyama vya siasa vya upinzani hawaitakii mema nchi yetu na lengo lao ni kutaka kuleta machafuko.
Ninavyoelewa ni kwamba serikali inafanya mambo yake kwa weledi mkubwa hivyo wananchi wasiwe na wasiwasi kwani kila kitu kitakwenda kama kilivyopangwa.


:wink2:
 
Unauhakika apr30 tutaipigia kura kama walivyokua wanajitapa viongozi wako? Au una andika andika tu ilimradi?
 
Jina lake haliendani na alichopost, jinale lina mana mtu mwenye nguvu alichopost kinamaanisha mtu dhaifu hasa kifikraaa...haiwezekani akajitokeza mtu kuisemea gvnment wakt anajua oredy failed...mbona hawasemi kura ya maoni itapgwa lini??
 
Hivi kwa wale wanaosema pia upigaji Kura katiba inayopendekezwa hautakuwepo wana uhakika gani!mie nadhan kwa kuleta Hali ya utulivu nchini hakuna haja kutoka povu kwa mambo ambayo bado hayajatokea!ni Jambo la kusubiri na kuona!
 
We ni nani katika serikali. Semea jambo hili hadharani ili wa-tz wakuelewe.
Kwani kuna ubaya gani yeye kusema hivo? Si amesikia kutoka kwenye vyombo vya habari, kama wewe ni mvivu wa kufuatilia habari basi usimlaumu huyo jamaa na hata mimi niliona kupitia kwenye blogs hiyo taarifa baada ya Ukawa kulalamika na kuwa na wacwac eti huenda uchaguzi mkuu usifanyike na huenda rais akaongezewa muda mambo amabyo NEC iliyafafanua vema na kutoa tamko hilo.
 
Jina lake haliendani na alichopost, jinale lina mana mtu mwenye nguvu alichopost kinamaanisha mtu dhaifu hasa kifikraaa...haiwezekani akajitokeza mtu kuisemea gvnment wakt anajua oredy failed...mbona hawasemi kura ya maoni itapgwa lini??
Hivi wewe unafatiliaga taarifa za habari kaka, NEC walishafafanua hayo yote.
 
Jitokeze kujiandikisha na hatimaye kupiga kura ya ndio kwa katiba inayopendekezwa
 
Jina lake haliendani na alichopost, jinale lina mana mtu mwenye nguvu alichopost kinamaanisha mtu dhaifu hasa kifikraaa...haiwezekani akajitokeza mtu kuisemea gvnment wakt anajua oredy failed...mbona hawasemi kura ya maoni itapgwa lini??
Mi nachojua kuna time walitangaza kuahirisha tena ni Tume na ilisema imeahirisha kura ya maoni mpaka itakapotangaza tena,kupanga ni kuchagua najua watakuja watuambie tena tarehe rasmi,kuhusu uchaguzi mkuu hilo ni kama kawa kwa mujibu wa Katiba.Mungu ibariki Tanzania.
 
We ni nani katika serikali. Semea jambo hili hadharani ili wa-tz wakuelewe.

Ndugu raia makini ni yule anayefuatlia masuala ya nchi yake,mzalendo na ambaye yuko tayari kuwasaidia wenzake na kulitetea taifa,huwezi kusikia jambo baya linasemwa na mgeni juu ya nchi yako ukakaa kimya,mzalendo wa kweli lazima aseme ukweli na awe tayari kuitetea nchi yake,huyo ndugu ana haki ya kufanya hivyo!
 
We ni nani katika serikali. Semea jambo hili hadharani ili wa-tz wakuelewe.
Jombaaa hauna hata redio hapo kitaaa? Njoo nikuazimemyangu ili habari muhimu kama hizo zisiwe zinakupita daily. Nec walishazungumza kwenye vyombo tena yapata wiki sasa.
 
Back
Top Bottom