Katiba: Kwa mara ya kwanza Dr Banna apaza sauti, na kuilaani CCM

Katiba: Kwa mara ya kwanza Dr Banna apaza sauti, na kuilaani CCM

sixgates

JF-Expert Member
Joined
Mar 19, 2011
Posts
3,979
Reaction score
1,665
Mchambuzi wa masuala ya kisiasa nchini Dr Benson Banna ambaye kwa mara nyingi uchambuzi wake umekuwa ukitiliwa shaka haswa kwa kuonekana kuegemea CCM na kuitetea serikali kwa kila jambo, leo kupitia kipindi cha Nipashe cha redio one asubuhi hii ameilaani CCM kwa yanayoendelea bungeni kwa kusema ndio kikundi pekee ambacho kinaonekana kimejipanga kukwamisha zoezi la kupata katiba mpya.

" CCM ni chama tawala, unapokuwa kiongozi inabidi uonyeshe mfano, lakini ukiangalia yanayoendelea ni wazi ccm ndio wanavuruga mchakato wa kupata katiba, hata kuandaa mwenyekiti sio kitu kilichopaswa kufanywa na ccm. Ukiangalia utaona ccm wanapinga hata mambo yasiyo na maana, kitu kinachotia shaka sana." Alisema Banna.

Banna akiongea kwa masikitiko, amelaani yanayofanywa na ccm, na kusema wana agenda yao ya siri lazima waache ukweli uprevail.
 
Huyu Bana nadhani atakuwa hajapewa fungu muda sasa ndo maana amewapa live.
 
Njaa tuu huwa zinatufanya tuishabukie ccm!ukweli ni kuwa ccm ni kansa kwa watanzania
 
Akuna ambaye afahamu kuwa ccm ni watu wa ovyo kwenye mchakato wa katiba hii
Swala la mwenyekiti siyotaabu sana kwa sababu walitaka chenge au migiro ndo lati ya hao mmoja wapo awe mwenyekiti wakapima upepo wakaona autakaa vizuri baada ya kufanya utafiti wao na kuona sita ayachukua fomu yeye kama yeye na kushinda ndipo walipomwita na kumpa mashariti kuwa asije kuwageuka ila huyu mzee anakubalika na watu wengi sana ambao ni wabunge wa bunge maalumu.
 
lete mauzo ya DVD,we umeambiwa ugawe bure,we unauza

Mkuu hivi Kalenga hali ya kisiasa ipoje, baada ya chadema kuambulia viti vitatu vya udiwani kati ya 27 Dr Slaa hata hataki kuisikia kalenga anaogopa aibu. Any way tunawasubiri chalinze
 
Mchambuzi wa masuala ya kisiasa nchini Dr Benson Banna ambaye kwa mara nyingi uchambuzi wake umekuwa ukitiliwa shaka haswa kwa kuonekana kuegemea CCM na kuitetea serikali kwa kila jambo, leo kupitia kipindi cha Nipashe cha redio one asubuhi hii ameilaani CCM kwa yanayoendelea bungeni kwa kusema ndio kikundi pekee ambacho kinaonekana kimejipanga kukwamisha zoezi la kupata katiba mpya. " CCM ni chama tawala, unapokuwa kiongozi inabidi uonyeshe mfano, lakini ukiangalia yanayoendelea ni wazi ccm ndio wanavuruga mchakato wa kupata katiba, hata kuandaa mwenyekiti sio kitu kilichopaswa kufanywa na ccm. Ukiangalia utaona ccm wanapinga hata mambo yasiyo na maana, kitu kinachotia shaka sana." Alisema Banna.

Banna akiongea kwa masikitiko, amelaani yanayofanywa na ccm, na kusema wana agenda yao ya siri lazima waache ukweli uprevail.
Hana jipya Dr.njaa
 
Kupata katiba katika nchi za Kiafrika hasa zile ambazo zilikuwa kwenye himaya ya siasa za mashariki ni mpambano wa kisiasa kwa sababu jamii bado ina element ndani ya fikra kama nchi bado iko kwenye chama kushika hatamu kwa sababu utendaji wa serikali bado uko kwenye mlengo huo.

Kama kuna mtu na hasa wa upande wa pili alidhani kuwa CCM watakubaliana kwenye sinia la kisiasa na vyama vingine kuondokana na kile kilichoifanya kuwa madarakani mpaka sasa kwa urahisi basi huyo atakuwa ndiyo ana matatizo ya fikra.

Kwanza mimi nimeshangazwa sana na jinsi mambo yanavyokwenda kwa makubaliano bila misuguano mikali hasa nikilinganisha na ukweli halisi wa siasa nchini kwa sababu hili swala la katiba linahusu nchi mbili kuziunganisha kuwa pamoja ndani ya katiba.
 
Dr.Benson Banna ni mchambuzi aliyetulia sana huwa hamung'unyi maneno na katika mambo yakitaifa huwa yuko mbele nampongeza sana kuweka wazi kuwa ccm wanavuruga kitiba.hongera sana Dr.wangu.
 
Tusitegemee katiba,kama kawaida kile kijiwe watu wameenda kupiga pesa
 
Dr.Benson Banna ni mchambuzi aliyetulia sana huwa hamung'unyi maneno na katika mambo yakitaifa huwa yuko mbele nampongeza sana kuweka wazi kuwa ccm wanavuruga kitiba.hongera sana Dr.wangu.

Wewe utakuwa Bana mwenyewe. Nyambaffu kabisa!
 
Bana na maigizo ya redet....

Akaandae research ya redet na aseme ccm wapo juu 2015.

vinginevo ni mjinga tu.
 
Dr.Benson Banna ni mchambuzi aliyetulia sana huwa hamung'unyi maneno na katika mambo yakitaifa huwa yuko mbele nampongeza sana kuweka wazi kuwa ccm wanavuruga kitiba.hongera sana Dr.wangu.
Una maslahi na baba ako kenge wewe
 
Huyo Dr. anauma na kupuliza tu, aala hutakiwi kuambiwa jinsi wanavyofanya rafu kwenye bunge maalumu la katiba.
Wangeacha uccm wao pembeni katiba ikiisha wauvae.
Nachukia yeyote mule anayeingiza siasa kwenye katiba, ile ni ya watanzania wote.
 
Mkuu hivi Kalenga hali ya kisiasa ipoje, baada ya chadema kuambulia viti vitatu vya udiwani kati ya 27 Dr Slaa hata hataki kuisikia kalenga anaogopa aibu. Any way tunawasubiri chalinze
Yaani ni kama umelogwa kama huelewi alichokisema mleta mada,
 
Dr.Benson Banna ni mchambuzi aliyetulia sana huwa hamung'unyi maneno na katika mambo yakitaifa huwa yuko mbele nampongeza sana kuweka wazi kuwa ccm wanavuruga kitiba.hongera sana Dr.wangu.


Join Date : 6th March 2014
Posts : 7
Rep Power : 302
Likes Received0
Likes Given



Wewe inaelekea unauelewa mdogo sana juu ya huyu jamaa ama unafanya makusudi kuandika hayo. Nani asiyejua kuwa Dr. Bana ni mnafiki namba moja na mara zote huwa anajipendekeza kwa CCM. Ndiyo maana watu wengi wanasema kuwa CCM wanavuruga mchakato wa upatikanaji wa katiba mpya, lakini huyu ndiyo tunashangaa naye kusema haya. Huyu amechangia sana kupotosha umma kwa kuitetea CCM kwenye udhaifu wake badala ya kuikosoa na kuishauri. Sasa wameshakuwa hawashauriki ndiyo anajifanya kuwalaani. Ni heri angekaa kimya tu kuliko kututia kichefuchefu..
 
Back
Top Bottom