masopakyindi
Platinum Member
- Jul 5, 2011
- 18,207
- 13,839
Mchakato wa kutengeneza katiba mpya ndo umeanza, na mambo yana badilika kila uchao.
Katika mchakato huu wa kihisoria, pengine muasisi wa mchakato huu, Rais Jakaya Kikwete hatasahaulika na wanahistoria watakuwa na maoni tofauti katika hili.
Hata hivyo mchakato mzima unaelekea kukiumbua kwa kiasi fulani Cha cha Mapinduzi, kwa vile hakionekani kama kilikuwa kimejiandaa vyema.
Kuna mambo kadhaa yanayoonyesha kuwa kujiandaa kwa CCM katika mchakato huu yatakiletea msimamo hasi mbele ya jamii.
Naweza kuwa nimekosea katika uchambuzi huu, lakini yanayooneka kisiasa yanaashiria udhhiri wa kukosa msimamo dhabiti katika hili.
La kwanza ni kwamba suala la mchakato wa katiba mpya halikuwa katika ilani ya uchaguzi mwaka 2010.
Mchakato huu umekuja kwa shinikizo toka nje ya chama, hivyo basi wanachama wa CCM hawakuweza kupata muda wakujitayarisha kisaikolojia na kwa kupata mifumo endelevu kwa nchi na chama chao.
Hili halina ubishi.
Pili,Chama hakutoa maoni yakekiufasaha juu ya suala la muungano hasa pale Zanzibar kupitia Baraza la Wawakilishi lilipoamua kujifanyia marekebisho ya katiba Ya Zanzibar bila kutilia maanani nafasi yao na madhara yake kwa muungano.
Kimsingi mabadiliko ya katiba ya Zanzibar ni kama ya repudiate uhalali wa mungano kwa vile Zanzibar waliamua kuwa Nchi.
hatujasahau wajumbe wa Baraza la Wawakilishi walivyo mdharau mh Miz engo Pinda juu ya hili Bungeni alipolielezea hili kisheria, tukijua kwa ni mwanasheria.
Tatu, ulipoanzishwa mchakato wenyewe kwa kupitia Tume ya Warioba, chama kimejisahau kuwa Tume hii iliwauliza wananchi juu ya kile wakitakacho katika marekebisho ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Tume haikuja na mawazo yake yenyewe bali yale wananchi walivyotaka.
Dalili ya kwanza ya kuonyesha kuwa chama sasakimechanganyikiwa ni kilipo anza kumshambulia Mzee Warioba kwa kuonyesha kile wananchi wakitakacho.
Ni kama vile chama kilikuwa kinajaribu kukivunja kioo kinachoonyesha taswira ya kile kinachoonekana ndani ya kioo.
Habari ambazo hazijathibitishwa ni kwamba chama kimetayarisha msimamo wake tayari juu ya kile ikitakacho, maoni ambayo hayana baraka ya wananchi walio wengi.
Hapa ndio nasema chama kinajiwekea mzingira nagumu kisiasa, maana kuna uwezekano mkubwa sana si kupingwa na wananchi tu, bali hata na wanachama wenyewe na dhamira zao.
Kama chama kingependa kurudisha its moral authority, lazima kifanye maamuzi magumu sana.
Kwanza, kuryudisha imani ya wananchi na wanachama kwa kurekebisha kasoro za katiba iliyorekebishwa ya Zanzibar, ili supremacy ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania isitiliwe shaka na mtu yeyote.
Pili chama kione uwezekano wa kuwa na serikali moja tu, ili kuondoa shaka toka pande zote za muungano juu ya dhamira zisizoeleweka.
Tatu, all along chama kimekuwa defensive katika mchakato mzima wa katiba mpya, chama kikae chini kijiulize kilipo jikwaa, maana sana sana inavyoonekana sasa ni kama chama kinalazimisha kutetea nafasi ya viongozi wake bila kufikiria au kuwa pamoja na wananchi.
Mpaka naandika haya, huwa najiuliza wale strtegic thinkers wa chama waliishia wapi?
Lakini kimsingi, hapa tulipo hatukufika kwa bahati mbaya, tumejiwekea mazingira magumu sisi wenyewe.
Katika mchakato huu wa kihisoria, pengine muasisi wa mchakato huu, Rais Jakaya Kikwete hatasahaulika na wanahistoria watakuwa na maoni tofauti katika hili.
Hata hivyo mchakato mzima unaelekea kukiumbua kwa kiasi fulani Cha cha Mapinduzi, kwa vile hakionekani kama kilikuwa kimejiandaa vyema.
Kuna mambo kadhaa yanayoonyesha kuwa kujiandaa kwa CCM katika mchakato huu yatakiletea msimamo hasi mbele ya jamii.
Naweza kuwa nimekosea katika uchambuzi huu, lakini yanayooneka kisiasa yanaashiria udhhiri wa kukosa msimamo dhabiti katika hili.
La kwanza ni kwamba suala la mchakato wa katiba mpya halikuwa katika ilani ya uchaguzi mwaka 2010.
Mchakato huu umekuja kwa shinikizo toka nje ya chama, hivyo basi wanachama wa CCM hawakuweza kupata muda wakujitayarisha kisaikolojia na kwa kupata mifumo endelevu kwa nchi na chama chao.
Hili halina ubishi.
Pili,Chama hakutoa maoni yakekiufasaha juu ya suala la muungano hasa pale Zanzibar kupitia Baraza la Wawakilishi lilipoamua kujifanyia marekebisho ya katiba Ya Zanzibar bila kutilia maanani nafasi yao na madhara yake kwa muungano.
Kimsingi mabadiliko ya katiba ya Zanzibar ni kama ya repudiate uhalali wa mungano kwa vile Zanzibar waliamua kuwa Nchi.
hatujasahau wajumbe wa Baraza la Wawakilishi walivyo mdharau mh Miz engo Pinda juu ya hili Bungeni alipolielezea hili kisheria, tukijua kwa ni mwanasheria.
Tatu, ulipoanzishwa mchakato wenyewe kwa kupitia Tume ya Warioba, chama kimejisahau kuwa Tume hii iliwauliza wananchi juu ya kile wakitakacho katika marekebisho ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Tume haikuja na mawazo yake yenyewe bali yale wananchi walivyotaka.
Dalili ya kwanza ya kuonyesha kuwa chama sasakimechanganyikiwa ni kilipo anza kumshambulia Mzee Warioba kwa kuonyesha kile wananchi wakitakacho.
Ni kama vile chama kilikuwa kinajaribu kukivunja kioo kinachoonyesha taswira ya kile kinachoonekana ndani ya kioo.
Habari ambazo hazijathibitishwa ni kwamba chama kimetayarisha msimamo wake tayari juu ya kile ikitakacho, maoni ambayo hayana baraka ya wananchi walio wengi.
Hapa ndio nasema chama kinajiwekea mzingira nagumu kisiasa, maana kuna uwezekano mkubwa sana si kupingwa na wananchi tu, bali hata na wanachama wenyewe na dhamira zao.
Kama chama kingependa kurudisha its moral authority, lazima kifanye maamuzi magumu sana.
Kwanza, kuryudisha imani ya wananchi na wanachama kwa kurekebisha kasoro za katiba iliyorekebishwa ya Zanzibar, ili supremacy ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania isitiliwe shaka na mtu yeyote.
Pili chama kione uwezekano wa kuwa na serikali moja tu, ili kuondoa shaka toka pande zote za muungano juu ya dhamira zisizoeleweka.
Tatu, all along chama kimekuwa defensive katika mchakato mzima wa katiba mpya, chama kikae chini kijiulize kilipo jikwaa, maana sana sana inavyoonekana sasa ni kama chama kinalazimisha kutetea nafasi ya viongozi wake bila kufikiria au kuwa pamoja na wananchi.
Mpaka naandika haya, huwa najiuliza wale strtegic thinkers wa chama waliishia wapi?
Lakini kimsingi, hapa tulipo hatukufika kwa bahati mbaya, tumejiwekea mazingira magumu sisi wenyewe.