Katiba mpya ifute uwakilishi haramu

Katiba mpya ifute uwakilishi haramu

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
219,468
Reaction score
911,184
Uwakilishi bungeni kwa zaidi ya asilimia sabini ni haramu kwa sababu hautokani na wananchi wanaoishi maeneo husika ila wahamiaji kutoka mijini huwanyang'anya wakaazi wa maeneo yale uwakilishi husika na hivyo kufanya uwakilishi huo kuwa ni haramu au kwa lugha ya kimombo carpetbaggers.........................

Katiba mpya iweke legal residence status requirements za kuhakikisha watu kutoka mijini au nje ya nchi ambao hawakukaa kwenye majimbo yao kwa wakati mwafaka hawaruhusiwi kugombea maeneo yale....................

Mfano utakuta mkaazi wa Dar eti kwa vile alizaliwa jimbo fuilani na kusomea kule lakini haishi pale kwa miaka nenda rudi bado anajiandikisha kuwa mgombea wa hilo jimbo kwa minajili ya kuukwaa ubunge kwenye jimbo ambalo haishi humo na matatizo yake wala hayajui ila ni ya kujulishwa tu......................

Hata kwenye kugombea uraisi upo uhaja wa kuweka legal residence requirements kwa minajili ya kuwazuia walowezi wetu waliokaa nje ya nchi kwa miaka mingi kutokuja na kuvuruga utawala wetu kwa kugombea nafasi hii nyeti wakati hawajaishi humu nchini ili kuyafahamu matatizo yetu.................
 
Uwakilishi bungeni kwa zaidi ya asilimia sabini ni haramu kwa sababu hautokani na wananchi wanaoishi maeneo husika ila wahamiaji kutoka mijini huwanyang'anya wakaazi wa maeneo yale uwakilishi husika na hivyo kufanya uwakilishi huo kuwa ni haramu au kwa lugha ya kimombo carpetbaggers.........................

Katiba mpya iweke legal residence status requirements za kuhakikisha watu kutoka mijini au nje ya nchi ambao hawakukaa kwenye majimbo yao kwa wakati mwafaka hawaruhusiwi kugombea maeneo yale....................

Mfano utakuta mkaazi wa Dar eti kwa vile alizaliwa jimbo fuilani na kusomea kule lakini haishi pale kwa miaka nenda rudi bado anajiandikisha kuwa mgombea wa hilo jimbo kwa minajili ya kuukwaa ubunge kwenye jimbo ambalo haishi humo na matatizo yake wala hayajui ila ni ya kujulishwa tu......................

Hata kwenye kugombea uraisi upo uhaja wa kuweka legal residence requirements kwa minajili ya kuwazuia walowezi wetu waliokaa nje ya nchi kwa miaka mingi kutokuja na kuvuruga utawala wetu kwa kugombea nafasi hii nyeti wakati hawajaishi humu nchini ili kuyafahamu matatizo yetu.................
Good thinking. Haya mawazo nayaafiki kwa asilimia mia moja kwani wengi 'hujirudisha' majimboni wakati wa uchaguzi ilhali hawajui matatizo ya jio husika. Ila haya mawazo yatapata upinzani mkali sana kwani wengi wa wanasiasa wanafaidika na mfumo wa sasa.
 
Ni kweli wawakilishi wengi wanakuja kama mamluki wakati wa uchaguzi, mfano batilida kugombea Arusha, Mpendazoe kugombea segerea nk ulikuwa ni uhuni wa kisiasa! Hawa mara nyingi ni watu wenye malengo ya mda mfupi ya kujinufaisha kwa nafasi zao huku wakiwaacha watu bila uwakilishi! Koffi Anan aliwahi kukataliwa kugombea urais wa Ghana kwa kigezo cha kuishi nje ya nchi kwa miaka mingi!
 
Back
Top Bottom