Katiba Mpya ihusishe haya

Katiba Mpya ihusishe haya

MPAMBANAJI.COM

JF-Expert Member
Joined
Mar 2, 2011
Posts
712
Reaction score
332
Pongezi kwa Serikali na tume ya Katiba Mpya

Katika hitimisho la Katiba naomba na haya yazingatiwe:

1.Wakuu wa mikoa wachaguliwe na wananchi kila baada ya miaka mitano wakati wa uchaguzi mkuu na asiwe katika mfumo wa chama cha siasa

2.msajili wa vyama vya siasa naye achaguliwe na wananchi wakati wa uchaguzi mkuu kila mara bada ya miaka 10 na sio Rais kama ilivyo sasa

3.Siku ya Ijumaa iwe ni mapumziko na kazi zote za kiofisi zianze saa 1:30 asubuhi hadi 11 jion ili kufidia siku ya Ijumaa ila jumamosi ni siku kama kawaida

4.Ikubalike japo Tanzania haina dini bali Bunge na shughuli zote za kiserikali zianze kwa sala ya jumla na kufungwa vivyo hivyo bila kutaja aina ya Mungu au mtume au Mkombozi Yesu.

5.Rais atakayeshinda ni yule tu atakayefikisha asilimia hamsini na kuendelea ya kura zote

6. Idadi ya vyama vya siasa viwe 6 tuu, ili kupunguza ukiritimba wa vyama, kuepuka migogoro ya maslahi kisiasa na pia gharama za kuendesha chaguzi mbalimbali.

Haya ndo yangu kwa sasa wadau
 
Pongezi kwa Serikali na tume ya Katiba Mpya

Katika hitimisho la Katiba naomba na haya yazingatiwe:

1.Wakuu wa mikoa wachaguliwe na wananchi kila baada ya miaka mitano wakati wa uchaguzi mkuu na asiwe katika mfumo wa chama cha siasa

2.msajili wa vyama vya siasa naye achaguliwe na wananchi wakati wa uchaguzi mkuu kila mara bada ya miaka 10 na sio Rais kama ilivyo sasa

3.Siku ya Ijumaa iwe ni mapumziko na kazi zote za kiofisi zianze saa 1:30 asubuhi hadi 11 jion ili kufidia siku ya Ijumaa ila jumamosi ni siku kama kawaida

4.Ikubalike japo Tanzania haina dini bali Bunge na shughuli zote za kiserikali zianze kwa sala ya jumla na kufungwa vivyo hivyo bila kutaja aina ya Mungu au mtume au Mkombozi Yesu.

5.Rais atakayeshinda ni yule tu atakayefikisha asilimia hamsini na kuendelea ya kura zote

6. Idadi ya vyama vya siasa viwe 6 tuu, ili kupunguza ukiritimba wa vyama, kuepuka migogoro ya maslahi kisiasa na pia gharama za kuendesha chaguzi mbalimbali.

Haya ndo yangu kwa sasa wadau

kwanza nianze kwa kusema nadhani maoni ungepeleka katika tume ya katiba kulekwenye web yao kuna e mail ya ku post
pili cjaelewa kwanini ijumaa? na jumamosi ni siku ya kawaida? kivipi? hujaeleweka
Tatu, bunge hapo, cjui kama huwa unackiliza Bunge, kwani huwa linataja imani flani? au yesu au mohamad (kumladhi kama nitakuwa sijaandika sahihi jina la huyo bwana)mi ninachochua huwa wanataja mwenyezi mungu baaasi au unataka waongeze na neno mizimu ya mababu?
 
Sawa kwa maoni yako. pia copy na kupest kwa e-mail yao

1.Ijumaa ni vyema ikawa hivyo kwani minong'ono tayari imeanza kwa siku hii kutambulika rasmi kwa waislamu kama ilivyo Jumapili kwa Wakristo
2.Juamosi huwa ni nusu siku kikazi kwa baadhi ya Ofisi hivyo iendelee hivyo hivyo
3. Kusuhu sala..tayari maoni ya Tanzania kuwa na dini imeanza na ni vyema ikaendelea kama ilivyo sasa
4. Kuhusu Yesu umemtaja vizuri na huja kosea

Pia sina mrengo wowote wa kidini kwa kusema hya
Aksante kwa maoni yako ila naogopa kutaja hilo jina laoko kwani nitakuwa nimekuballi we ni dumelang
 
Back
Top Bottom