Katiba Mpya itokane na Wananchi wenyewe

Katiba Mpya itokane na Wananchi wenyewe

Shatisa Luck

New Member
Joined
May 8, 2023
Posts
2
Reaction score
0
Maoni ya kupata Katiba mpya na safi itokane na WANANCHI wenyewe wa Kila makundi kupitia mikutano ya Kitongoji, Kijiji na mitaa na sio kutafuta wawakilishi ambao waliowengi wanatoa mawazo dhahania ya wenzao na sio wananchi. Ni HERI serikali itumie gharama kubwa ili kupata Katiba safi isiyona machafuko Wala ghasia.

Wajumbe wa Maoni ya katiba izingatie zaidi MAONI YA WANANCHI NA SIO WANASIASA japo siasa ni sehemu mojawapo ya maisha ya watu nchini
 
Ikifanyika hivyo itakuwa sawa sana.
Yaani makundi mbalimbali ya wananchi yakae yaandae draft bila kuwashirikisha wabunge.
Na bunge la Katiba kwa ajili ya kuidhinisha pia lisiwashirimishe wanasiasa!
Au kama ni lazima washiriki basi Vyama vya siasa vitoe 15% to 25% ya wajumbe wote!
 
Ikifanyika hivyo itakuwa sawa sana.
Yaani makundi mbalimbali ya wananchi yakae yaandae draft bila kuwashirikisha wabunge.
Na bunge la Katiba kwa ajili ya kuidhinisha pia lisiwashirimishe wanasiasa!
Au kama ni lazima washiriki basi Vyama vya siasa vitoe 15% to 25% ya wajumbe wote!
Tuko Watanzania milioni 60 hajuna uwanja unaoweza kutushikilia wote tukae tusainiane makubaliano yaani Katiba. Ingekuwa tuko wachache au ingekuwa ni kitu kimoja tukakubaliana sote 100% pia ingekuwa rahisi. Kwa vile tuko wengi na tuna mawazo tofauti, njia pekee ni kutumia wawakilishi tulipwachagua. Wawakilishi hawo ni Wabunge aina 3: Mbunge mmoja tumechagua kila jimbo la uchaguzi; Mbunge mmoja mmoja tumechagua kwa kila Kata (huyu huitwa Diwani); na Mbunge mmoja tumechagua kwa Nchi nzima (huyu huitwa Rais). Hawa ndiyo wana madaraka ya kutusema, watched wakae walete Katiba pendekezwa sisi Wananchi tupoge kura referendum. Tunakosea sana kuwadharau hawa kwa kuwaita "wanasiasa" kwa sababu hawa ni wateule wetu kwa kazi kama hizi. Hii ya kudai eti kuna makundi mengine kama wavivi au wamachinga au Wahandisi au Walemavu nk nk haina mshiko kwa sababu wite hawa wanawakilishwa kupitia majimbo yao (Mbunge), Kata zao (Madiwani), au Nchi yote (Rais). Mbona wengi ni CCM? Hakuna taabu, ndivyo Wananchi walivyochagua, lazima waheshimiwe. La sivyo mtu atasema mbona wengi ni weusi hakuna Wazungu? Mbona wote wanaongea Kiswahili hakuna wanaoongea Kifaransa? Mbona hakuna Wageni? Mbona hakuna Wahindu? Tutachoka, tuliochagua kwa hiari yetu wanatosha - yaani Rais, Wabunge na Madiwani. Tuwaachie.
 
Tuko Watanzania milioni 60 hajuna uwanja unaoweza kutushikilia wote tukae tusainiane makubaliano yaani Katiba. Ingekuwa tuko wachache au ingekuwa ni kitu kimoja tukakubaliana sote 100% pia ingekuwa rahisi. Kwa vile tuko wengi na tuna mawazo tofauti, njia pekee ni kutumia wawakilishi tulipwachagua. Wawakilishi hawo ni Wabunge aina 3: Mbunge mmoja tumechagua kila jimbo la uchaguzi; Mbunge mmoja mmoja tumechagua kwa kila Kata (huyu huitwa Diwani); na Mbunge mmoja tumechagua kwa Nchi nzima (huyu huitwa Rais). Hawa ndiyo wana madaraka ya kutusema, watched wakae walete Katiba pendekezwa sisi Wananchi tupoge kura referendum. Tunakosea sana kuwadharau hawa kwa kuwaita "wanasiasa" kwa sababu hawa ni wateule wetu kwa kazi kama hizi. Hii ya kudai eti kuna makundi mengine kama wavivi au wamachinga au Wahandisi au Walemavu nk nk haina mshiko kwa sababu wite hawa wanawakilishwa kupitia majimbo yao (Mbunge), Kata zao (Madiwani), au Nchi yote (Rais). Mbona wengi ni CCM? Hakuna taabu, ndivyo Wananchi walivyochagua, lazima waheshimiwe. La sivyo mtu atasema mbona wengi ni weusi hakuna Wazungu? Mbona wote wanaongea Kiswahili hakuna wanaoongea Kifaransa? Mbona hakuna Wageni? Mbona hakuna Wahindu? Tutachoka, tuliochagua kwa hiari yetu wanatosha - yaani Rais, Wabunge na Madiwani. Tuwaachie.
Hivi wewe kumbe uliwachagua hao wabunge na madiwani?🤣🤣🤣
Rejea hoja yangu... Hao wana platform yao. Tena kubwa tu! Na tambua kuwa Katiba ni mkataba kati ya viongozi na wanaoongozwa!
Sasa wanaoongozwa lazima washiriki mchakato tena Moja kwa Moja bila uwakilishi!
Kumbuka Katiba ya Warioba ilikwama baada ya wanasiasa kuingiza interests zao!
 
Back
Top Bottom