Katiba mpya izuie viongozi wa dini kujiingiza kwenye siasa

Katiba mpya izuie viongozi wa dini kujiingiza kwenye siasa

Ngongoseke

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2012
Posts
3,202
Reaction score
1,462
Habari zenu wa jukwaa, kutokana na matatizo yanayoendelea ndani ya nchi yetu, mimi kwa maoni yangu naona bora katiba mpya izuie kabisa viongozi wa dini kujiingiza kwenye siasa au kushiriki mambo ya siasa wabaki washauri tu, nadhani hili litawajengea heshima kubwa katika jamii kuliko haya tunayo yashuhudia kwa sasa,

Na nina imani itasaidia sana kurudisha imani ya nchi ambayo ukweli ipo ICU.

Mkuu, hapo utakuwa umeangalia upande mmoja. Tatizo la kifisadi linaloikumba nchi hii pamoja na matatizo mengine yanatokana na kukosa viongozi wenye hofu ya Mungu kwa imani yao.

Kauli za baadhi ya viongozi katika migogoro ya kidini baadhi ya sehemu kama Geita na kwingineko imetokana na viongozi kukosa weledi wa kiimani na ndio maana wanasiasa hukimbilia viongozi wa dini katika kutatua migogoro ya kidini.

Kwa hiyo, kuwa na viongozi wa kidini kushika nyadhifa mbalimbali za kisiasa ni point of advantage kwa wananchi kwani haki hutendeka! Kuna baadhi ya watumishi katika office za umma ninaowafamu, ni waumini wenye hofu ya Mungu (kwa imani zote) hakika akikuhudumia hutatamani kusikia mtu huyo kahamishwa idara.

Lakini wengine hao unawatetea wasiguswe na viongozi wa dini wao kuchomia matumbo yao tu, hawana lolote, Otherwise, labda ufunguke zaidi!
 
Una maanisha nini kwa kujiingiza kwenye siasa?Unamaanisha wasigombee AU wasitumie dini kupata uongozi! Unamaanisha wasikemee maovu ya watawala au wasifanye nini?! Baada ya ufafanuzi ndpo nitapata kuchangia vizuri uzi huu!
 
Habari zenu wa jukwaa
Kutokana na matatizo yanayoendelea ndani ya nchi yetu, mimi kwa maoni yangu naona bora katiba mpya izuie kabisa viongozi wa dini kujiingiza kwenye siasa au kushiriki mambo ya siasa wabaki washauri tu,nadhani hili litawajengea heshima kubwa katika jamii kuliko haya tunayo yashuhudia kwa sasa,
Na nina imani itasaidia sana kurudisha imani ya nchi ambayo ukweli ipo ICU


Naunga hoja mkono kwa asilimia zote! Ni bora waendelee na kumtumikia Mungu kuliko kujiingiza katika siasa hasa katika nchi ya kisecular kama Tanzania na ambayo ipo kwenye tension kubwa ya kugawanyika kidini.
 
Ni kweli kwa sababu ukitazama hata kinachopelekea taifa kugawanyika mpaka sasa kiasi kikubwa sana kuingiliwa na viongozi wa dini,
Ubaya unakuja hawa viongozi wa dini wengi wao wameegemea kwenye imani zao nakusahau kama hili ni taifala wote
 
Tuwakaribisha kwenye nyumba zetu za ibada, waje wasali kama waumini wengine but tusiwape nafasi kwenye mimbari zetu, watoe sadaka sawa but kamwe wasipewe nafasi ya kuongea lolote hata kusalimia au kutambulishwa.

Makanisa yetu na misikiti yetu wasiizindue wao, tuzindue wenyewe na michango tuchangishane wenyewe na ikitokea wakachanga basi iwe acknowldged kama ya muumini mwingine yoyote.

Sisi waumini tusiwape nafasi na ikiwezekana tuhoji pale viongozi wetu wa dini zetu wanapowakaribisha viongozi wa siasa na kuwapa airtime kwenye nyumba zetu za ibada.

Tukumbuke nyumba zetu za ibada ni kwa ajili ya kumwabudu mungu na sio majukwaa ya siasa. Tukatae wanasiasa kutaja na kuhubiri dini zetu kwenye majukwaa ya siasa kwa faida yao, hasa wabunge wetu.

Kama waumini tutaungana na kukataa uharamia huu tutashinda vita hii ya udini.

Karibuni kwa mjadala ila tusilenge chama chochote .
 
Wazo zuri lakini je makanisa na misikiti itawezekana? Maana viongozi wa dini nao ni tatizo sana

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
nyumba za ibada zimevamiwa, viongozi wa dini hawafanyi kazi za mungu wamekua watumwa wa dunia, kabla ya kuwashughulikia wanasiasa tuanze na hao viongozi wa dini.
 
nyumba za ibada zimevamiwa, viongozi wa dini hawafanyi kazi za mungu wamekua watumwa wa dunia, kabla ya kuwashughulikia wanasiasa tuanze na hao viongozi wa dini.
umepiga mule mula....ninachotaka mimi nikuanza na vionghozi wetu. Tuwanyooshe kwanza then tunamalizia mchezo. Ndio maana hapo juu nikasema hivi kwamba ni Lazima waumini tukatae hivi vitu kwanza, sio viongozi wetu, na wenyewe wanafurahi san akupiga picha nao, kula nao na kucheka nao ndio maana nataka tuanze sisi
 
Habari zenu wa jukwaa
Kutokana na matatizo yanayoendelea ndani ya nchi yetu, mimi kwa maoni yangu naona bora katiba mpya izuie kabisa viongozi wa dini kujiingiza kwenye siasa au kushiriki mambo ya siasa wabaki washauri tu,nadhani hili litawajengea heshima kubwa katika jamii kuliko haya tunayo yashuhudia kwa sasa,
Na nina imani itasaidia sana kurudisha imani ya nchi ambayo ukweli ipo ICU

Mkuu, hapo utakuwa umeangalia upande mmoja. Tatizo la kifisadi linaloikumba nchi hii pamoja na matatizo mengine yanatokana na kukosa viongozi wenye hofu ya Mungu kwa imani yao.

Kauli za baadhi ya viongozi katika migogoro ya kidini baadhi ya sehemu kama Geita na kwingineko imetokana na viongozi kukosa weledi wa kiimani na ndio maana wanasiasa hukimbilia viongozi wa dini katika kutatua migogoro ya kidini.

Kwa hiyo, kuwa na viongozi wa kidini kushika nyadhifa mbalimbali za kisiasa ni point of advantage kwa wananchi kwani haki hutendeka! Kuna baadhi ya watumishi katika office za umma ninaowafamu, ni waumini wenye hofu ya Mungu (kwa imani zote) hakika akikuhudumia hutatamani kusikia mtu huyo kahamishwa idara.

Lakini wengine hao unawatetea wasiguswe na viongozi wa dini wao kuchomia matumbo yao tu, hawana lolote, Otherwise, labda ufunguke zaidi!
 
Fikiria tena. Rasimu ya katiba inatoa uhuru kwa watanzanoa wote. wewe bado unataka kuwabagua kwa misingi ya imani zao wasiingie kwenye siasa.
 
Back
Top Bottom