Katiba Mpya ndiyo itakuwa legacy ya Rais Samia sio Zahanati na Madaraja

Katiba Mpya ndiyo itakuwa legacy ya Rais Samia sio Zahanati na Madaraja

Sir robby

JF-Expert Member
Joined
Jun 22, 2022
Posts
2,396
Reaction score
4,080
Wadau nawasalimu,

Katiba Mpya ni kilio cha Watanzania kwa hivi sasa. Tatizo la katiba iliyopo ni la muda mrefu sana, karibia miaka 60 ya Uhuru. Nchi imekuwa na Marais 6 kwa sasa, hakuna Rais aliyeibadilisha Katiba iliyopo, katiba ambayo iliyotungwa bila kuwashirikisha wananchi ni Katiba ya viongozi.

Wakati wa utawala wa Awamu ya 4 Rais Kikwete aliamua kuwapatia Watanzania Katiba Mpya na wananchi walishiriki kutoa maoni na mapendekezo yao lakini hakufanikiwa kutokana na mahafidhina wa chama chake kutokuta mabadiliko na kupelekea mchakato wa Katiba Mpya kufa.

Alipoingia Rais Magufuli yeye bila aibu hakutaka kabisa kusikia suala la Katiba mpya kwani Katiba iliyopo inawapa madaraka makubwa sana viongozi wetu ndio sababu ya kutokutaka mabadiliko ya Katiba Mpya.

Kutokana na Marais wa 5 waliopita kushindwa kabisa kuwapatia wananchi Katiba Mpya namshauri Rais Samia awapatie Watanzania Katiba Mpya kwa kuwashirikisha katika kuitunga kutoa maoni na mapendekezo hakika atakuwa kajitengenezea "Legacy isiyosahaulika" atakumbukwa kama shujaa wa Katiba Mpya katiba iliyowashinda watangulizi wake.

Kiu ya Watanzania ni kuona nchi yao inafanya mabadiliko ya Katiba ili iendane na mabadiliko ya mambo mengi.

20220604_235447.jpg
 
You are the greatest genius for today!

Bimkubwa Vasco da Gama hana Cha kupoteza kwa kutupa katiba mpya na ni kweli atakumbukwa daima kwa Hilo maana kujenga reli, Barabara na zahanati ni kazi ya tozo zetu na ilani yetu kijani.

Katiba iliyopo Sasa ya 1977 si ya chama ni ya Nyerere jeshi la mtu mmoja to protect himself na kuhakikisha anaabudiwa bongo, jina lake, maiti yake na hadi kivuli chake!!


Katiba mpya ya wabongo iwe hivi

1. UWaziri iwe kazi ya kuapply Ili mawaziri wawajibike na wasitutukane eti tuhamie Burundi

2 Mkuu wa mkoa na Mkuu wa wilaya vyeo hivyo ni ubadhirifu wa Mali ya umma nyie viongozi mbele za Allah mtaenda kutapishwa tozo zetu

3 Viti maalum vyote ni ubadhirifu wa Mali ya umma ukitaka ubunge gombania Jimbo . Hivi viti maalum wanawakilisha mtaa gani? Ni wizi wa Mali ya umma

4 Serikali ihakikishe elimu, afya na maji viwe Bure. ni kazi ya tozo zetu sio favour. Umeme isiwe bizness ya Tanesco Bali huduma tulipe kidogo . Serikali iweke ruzuku

5 Rais akifa akiwa madarakani kufanyike uchaguzi mkuu wa Rais sio kumsimika mtu ambae hakuchaguliwa na sanduku la kura. Hii katiba na vifungu vya kipumbavu walijiwekea kina Chengi vijisenti kana kwamba hawatakufa Wala kustaafu!!

6. Vyeo vikubwa serikalini viendane na weledi Sheria iseme sio kupeana favour za Beijing madanga ya wazee eti nayo yako ofisini nowadays!!hii nchi ndo maana MVUA imekata na tutabaki maskini milele!

7. Rais ashitakiwe kwa ubadhirifu au matumizi mabaya ya madaraka akiwa madarakani

8. Idadi ya wabunge ipunguzwe na mbunge elimu ya chini digrii moja sio bunge kujaza Vilaza wanaosinzia ikija mijadala ya kisomi

9 Raia waruhusiwe kuandamana na kukashifu serikali openly bila kutishiwa na kukamatwa kuteswa na kupigwa mabomu na maji ya washawasha maana hela inazotumia serikali ni tozo kutoka kwao.

10. Katiba ifute shule Kufundisha Siasa ya kijinga ya Ujamaa tuweke Free Market economy and entrepreneurship. Shule zifundishe in English kuanzia chekechea.

11. Katiba iseme hakuna Tena Rais Mwanamke maana Sasa Beijing vilaza wamejazana maofisini watoto wao hawana wa kuwalea!
 
Back
Top Bottom