Katibu BAWACHA Taifa: Tunategemea wanawake wasiopungua 3,000 wahudhurie maadhimisho yetu ya siku ya wanawake. Maandalizi yanaendelea

Katibu BAWACHA Taifa: Tunategemea wanawake wasiopungua 3,000 wahudhurie maadhimisho yetu ya siku ya wanawake. Maandalizi yanaendelea

McLaren

Member
Joined
Feb 19, 2025
Posts
53
Reaction score
78
Baraza la Wanawake wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo BAWACHA limewataka wanawake kujitokeza kwa wingi kushiriki maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yatakayofanyika Machi 8, 2025, katika Ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari, Katibu Mkuu wa BAWACHA Taifa, Pamela Maassay, amesema maandalizi yanaendelea katika ngazi zote za chama, huku msisitizo ukiwa ni kushirikisha idadi kubwa ya wanawake kutoka kila kona ya nchi.

"Tumejipanga kuhakikisha tunakuwa na maadhimisho yenye tija na yenye ujumbe mzito wa kuhamasisha usawa wa kijinsia. Tunatarajia wanawake wasiopungua 3,000 kuhudhuria, na tunawaomba viongozi wa mikoa, majimbo na kata kuhamasisha ushiriki wa wanawake kwa wingi," alisema Masay.

Ameongeza kuwa mgeni rasmi wa tukio hilo atakuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Lissu, akifuatana na viongozi wa chama pamoja na wageni waalikwa kutoka ndani na nje ya nchi.

Kaulimbiu ya mwaka huu ni "Kuharakisha usawa wa kijinsia kwa maendeleo endelevu," ambapo BAWACHA itatumia jukwaa hilo kuonesha mchango wa wanawake katika siasa, uchumi na jamii kwa ujumla.

Aidha, Maassay ameeleza kuwa moja ya ajenda kuu katika maadhimisho hayo ni kampeni ya "He for She," inayolenga kuwashirikisha wanaume katika kuhakikisha wanawake wanapata fursa sawa na kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa Taifa.

"Kwa miaka mingi, harakati za haki za wanawake zimekuwa zikiendeshwa na wanawake wenyewe, lakini sasa tunasisitiza kuwa huu ni wakati wa wanaume pia kushiriki kwa nguvu zote katika kusukuma mbele ajenda ya usawa wa kijinsia," alisisitiza.

 
Ameongeza kuwa mgeni rasmi wa tukio hilo atakuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Tundu Lisu
Chadema vituko haviishi

Sherehe ya wanawake mgeni Rasmi mwanaume

Halafu uongo mwingine huo eti wanatarajia wanawake elfu tatu kuhudhuria uongo mtupu hawana hao watu hata kufikisha elfu moja tu hawataweza toka mikoa yote hawawezi
 
Chadema vituko haviishi

Sherehe ya wanawake mgeni Rasmi mwanaume

Halafu uongo mwingine huo eti wanatarajia wanawake elfu tatu kuhudhuria uongo mtupu hawana hao watu hata kufikisha elfu moja tu hawataweza toka mikoa yote hawawezi

Msigwa alisema CHADEMA ina wananchama takriban 500k

Kwa hiyo kupata wanachama 3000 ni kitu rahisi sana
 
Back
Top Bottom