Pre GE2025 Katibu Mkuu CUF: Uchaguzi Mkuu CUF Utapita Bila Mgogoro, Wanachama hawana Tamaa ya Madaraka

Pre GE2025 Katibu Mkuu CUF: Uchaguzi Mkuu CUF Utapita Bila Mgogoro, Wanachama hawana Tamaa ya Madaraka

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF Mheshimiwa Hamad Masoud amesema kuelekeka uchaguzi Mkuu ndani ya chama hicho ngazi ya Taifa, hakutakua na mgogoro wowote kwa kuwa wanachama hao hawana tamaa ya madaraka

Hamad ameeleza hayo wakati akichukua fomu ya Kugombea nafasi ya Uenyekiti Taifa wa chama hicho katika Ofisi za Wilaya ya Magharibi B Unguja

Amesema kila mwananachama atatumia haki yake ya kikatiba na Demokrasia katika kuchukua fomu ya kugombea nafasi hiyo ili kuendelea harakati za chama

Kuhusu Sababu za kuchukua fomu hiyo Hamad amesema ni pamoja na kutekeleza maombi ya Mwenyekiti wao wasasa Profesa Lipumba ya kuona kuna mabadiliko ya uongozi kwa ngazi zote ikiwemo Taifa

Wakati hayo yakiendelea hapo jana Tayari wapenzi na wafuasi wa Profesa Lipumba walifika katika Ofisi za CUF kumchukulia Fomu Profesa Lipumba kuendelea kulinda kiti hicho

Chama cha Wananchi CUF kipo katika mchakato wa kupanga safu ya Uongozi ambapo mwanzoni mwa mwezi wa Septemba wanatarajia kufanya uchaguzi kwa ngazi ya Taifa
 
huyu jamaa alijikanyaga sana kujiunga na CUF, ni bora hata angejiunga na CHADEMA kama alihisi kujuinga na chama kidogo sana changamoto zingekua kubwa.
 
Back
Top Bottom