Katibu mkuu wa CHADEMA John Mnyika ateta na mabalozi walipowasili mahakamani 10-9-2021 katika kesi ya Mbowe


yaaani ni misaada tu imejaa kichwan kwenu mbna jpm aliwatimua, nchi iliendelea tena uchumi ulipaa
 
yaaani ni misaada tu imejaa kichwan kwenu mbna jpm aliwatimua, nchi iliendelea tena uchumi ulipaa
Mliposhtakiwa na Mh.Zitto au Mh Lissu wakati wa Huyo marehemu wenu mnayemtetea humu Jukwaani palikuwa hapatoshi kwa malalamiko yenu,hivyo misaada na serikali ya CCM ni kama uji na mgonjwa.Vipi kuhusu Utalii na Uwekezaji?Mmejiandaaje mkiwatimua Mabalozi wa Ubeberuni?
Je,huo uchumi uliopaa na nchi kuendelea uliporomoshwa na nini na lini?Tupeane Updates ili tufahamiane.
 
Acha wivu kafyeke kule porini majani ni mengi mnafuga nyoka tu.....
 

mdogo wangu, utalii ni msaada? uwekezaji ni msaada? misaada inahusiana vp na mabalozi, kuna nchi zinatuma misaada lakini hakuna mabalozi uku
 
"UNALAZIMISHA USEME,' huku ukisema upumbavu?
Umejuaje kwamba Mnyika alikua "akitoa maelezo ya mwenendo wa kesi"?

Huo mwenendo wa kesi haupatikani kwingine kokote isipokuwa kupitia kwa Mnyika?
 
Akipatikana na hatia atandikwe miaka mingi tu jela , kadhalika aachiwe asipopatikana na hatia .

Suala la kusema hukumu ndio itafanya mabalozi waendelee kuwepo au lah!,ni kujidanganya tu hawezi achiwa akikutwa na hatia et kisa wataondoka kwa kuwa kuna ugaidi.
Ugaidi una stage zake,hapa kinachofanyika ni preventative measures, na lesson to others, tulia dogo
 
Mimi ni mwana ccm na nakipenda chama changu, lakini Katika hili viongozi wangu hawakufiri vizuri, kama kulikuwa na elementi za haya mavitu wangeyaweka wazi Kwanza kiasi watu wakose imani Mh Mbowe vinginevyo Jambo hili linaweza kulingawa taifa
 
Kesi ya mbowe walioitung imewakali vibaya sana
 
Tusisahau kuwa, vita dhidi ya Ugaidi imepewa kipaumbele cha kwanza na Mataifa ya Magharibi na ndiyo maana Mabalozi waliposikia kesi inayogusa ugaidi, wakaelekezwa kuifuatilia vyema na kwa taarifa tu ni kwamba, wanatoa mrejesho kwao kila wanapotoka Mahakamani na humu Tanzania hamtawasikia wakisema lolote! Yeyote anayehusisha ujio wao Mahakamani na masuala ya kisiasa atakuwa ni mtu mpumbavu na mwenye akili ndogo sana!

Huwezi taja neno UGAIDI kisha utarajie Marekani na Ulaya wachukulie poa hata kama munataniana tu kisiasa! Kwao ugaidi ni adui namba moja tangu matukio ya Septemba 11! Tuachane na kesi hizi za kifala tugeukie Uchumi wetu ambao unaning'inia!

Kesi hii itatupunguzia watalii zaidi na zaidi!! Hatutaona matokeo leo lkn baadaye tutajuta!!
 
Mhe Mnyika anfanya kitu huitwa "posturing" au "namedropping". Yaani kaona weupe, kajisogeza, kuna mpiga picha, go! Muda haujafika, lori la Segerea halijaja, watu wanafanya chit chat, engage in small talk. Ni kitu kama hivi:
"HELLO hello".
"HOW DO YOU DO how do you do".
"MY NAME IS JOHN mine is George".
"IT IS VERY HUMID TODAY, ISN'T IT yes is terrible".

Mara honi inalia watu wanaanza kuangalia kwenye geti, karandinga la Ukonga linaingia mabango ya sio gaidi yanatandazwa polisi ngangari.

HAPAKUWA NA MAONGEZI YOYOTE HAPA, NI BLABLA TU WATU WAKIPOTEZA MUDA KUSUBIRI SAA.
 
Tatizo mnaichukulia Cdm kama kundi la kuku. Hicho ni chama kina mahusiano kina watu pia. Kama Ccm haitaki wengine wakutane na diplomats . Kwanini tusirudie mfumo wa chama kimoja ?! Wivu tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…