Pre GE2025 Katibu Mwenezi, BAWACHA: Baraza la Madiwani la Chama kimoja ni hatari kuliko ugonjwa

Pre GE2025 Katibu Mwenezi, BAWACHA: Baraza la Madiwani la Chama kimoja ni hatari kuliko ugonjwa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

upupu255

Senior Member
Joined
Sep 4, 2024
Posts
119
Reaction score
144
Katibu Mwenezi wa Baraza la Wanawake wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (BAWACHA) taifa Sigrada Mligo amewataka watanzania kufanya mabadiliko kwa kuchagua madiwani toka vyama vya siasa tofauti tofauti ili waweze kunufaika na rasimali zilizopo kwa kuwa nchi ina mali ikiwemo madini ya kutosha yatakayowezesha kupunguza ugumu wa maisha lakini serikali imeshindwa kuyafanyia kazi

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Sigrada ameeleza hayo mkoani Njombe wakati akizungumza kwenye mkutano wa hadhara na wananchi wa Makete uliofanyika katika eneo la sokoni Makete mjini ambapo amesema mfumo wa kikodi ya serikali umesababisha ugumu wa maisha hivyo hakuna mtu mwingine wa kumlaumu kwa kuwa nchi ya Tanzania haijawahi tawala na Chama kingine nje ya CCM.

 
Back
Top Bottom