Katibu Tawala Simiyu: Elimu ya kujikinga na Kipindupindu kutolewa kwa Lugha ya Kisukuma na Kiswahili

Katibu Tawala Simiyu: Elimu ya kujikinga na Kipindupindu kutolewa kwa Lugha ya Kisukuma na Kiswahili

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Snapinsta.app_460897373_1506635503303441_6459059412733288004_n_1080.jpg
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Prisca Kayombo amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu kutumia lugha mbili ya Kiswahili na Kisukuma ili kuweajengea Wananchi wasijua lugha ya Kiswahili uelewa wa namna ya kukabiliana na ugonjwa wa kipindupindu.

Aidha amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Meatu kuhakikisha kuwa Mji wa Meatu unakua safi hatua itakayosaidia kupunguza kuenea kwa ugonjwa wa kipindupindu

Katibu Tawala Kayombo ametoa maagizo hayo katika Mkutano na Wananchi wa Kata ya Mbogayabanya wakati wa siku ya Usafishaji Duniani Kimkoa Wilayani humo.
Snapinsta.app_461028490_638614921883845_4593781052514451594_n_1080.jpg
"Mkurugenzi wa Halmashauri mnapopita katika maeneo mnayoroa Elimu lugha mbili zitumike ili kueajengea Waanchi uelewa juu ya namna ya kuepuka ugonjwa huo."Alisisitiza katibu Tawala Kayombo.

Amewakumbusha Wananchi kujenga vyoo Bora na kuzingatia matumizi sahihi ili kuepuka kuenea ugonjwa wa kipindupindu.

Watu 47 wameripotiwa kupata ugonjwa wa kipindupindu katika Kata ya Mbogayabanya huku 3 wakipoteza maisha tangu kuingia kwa ugonjwa huo katika Kata hiyo.
Snapinsta.app_460943080_885100283115884_3973618233035141534_n_1080.jpg

Snapinsta.app_461184337_889763329721039_8465312899365171672_n_1080.jpg

Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Prisca Kayombo alipokagua chanzo kimojawapo cha Maji Wilayani Meatu ,Moja kati ya shughuli aliyoifanya katika maadhimisho ya Siku ya Usafishaji Duniani Kimkoa Wilayani Meatu.

Pia soma:
~
Kihongosi: Baadhi ya Mila na Tamaduni zinachangia Kipindupindu Simiyu
~ Kipindupindu Simiyu kimeshamiri, kinaua ni hatari! Mbona Serikali haiweki wazi 'status' ipoje?
~ Wataalam wa Afya waingia mtaani kufanya jitihada za kudhibiti magonjwa ya kuhara Mkoani Simiyu
 
Back
Top Bottom