Katibu wa Afya Hospitali ya Mwanyamala: Ulomi alipata ajali, mwili uliletwa December 11, 2024

Katibu wa Afya Hospitali ya Mwanyamala: Ulomi alipata ajali, mwili uliletwa December 11, 2024

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
1734365327912.jpeg

Mwili wa Mfanyabiashara aliyeripotiwa kupotea tangu December 11,2024 Jijini Dar es salaaam, Daisle Simon Ulomi, umekutwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mwanyamala huku Uongozi wa Hospitali hiyo ukisema Ulomi afikishwa Hospitalini hapo December 11,2024 majira ya jioni akiwa ameshafariki na taarifa zinaonesha alifariki baada ya kupata ajali.

Kupata matukio ya nyuma kuhusu watu wasiyojulikana ingia hapa: Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana

Katibu wa Afya Mwandamizi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwananyamala, Lydia Nzema, ameiambia Ayo “December 11,2024 jioni tulipokea mwili kutoka Zahanati ya Makuburi, akiwa ameshafariki lakini Polisi kesi, ni kesi ya ajali mwili uliopatikana umepata ajali ameshafariki, ina maana alishapata kama ni matibabu au kama Kituo cha Afya alichopelekwa ilikuwa Zahanati ya Makuburi.

"Mwili ulikuwa Unknown hatukujua ni nani na tumehifadhi kwenye chumba cha maiti, leo December 16,2024 wamekuja Ndugu wameutambua mwili na wamesema ni Ndugu yao huyo Mfanyabiashara (Ulomi), kuhusu taarifa zaidi za alipata ajali gani taarifa zitakuwa mochwari zimeandikwa na taarifa zaidi Polisi wanazo.”

Soma Pia:
 
Inasikitisha. Mbona hospital haikutangaza kama kuna mwili usiotambulika?
 
malisa_gj, ameandika:-
Kwa mujibu wa familia, Ulomi aliondoka nyumbani tar.11 December 2024 akidai kupigiwa simu na watu wa TRA kwenda kufuatilia kontena lake bandarini. Kwa mujibu wa Muliro siku hiyohiyo tar.11 Ulomi alipata ajali ya pilipiki na kukimbizwa kituo cha afya Makuburi (Ubungo External) kisha hospitali ya Mwananyamala. Kwa mujibu wa Katibu wa Hospitali ya Mwananyamala, walipokea mwili wa Ulomi tar.11 kutoka kituo cha afya Makuburi. Maana yake confirmation of death ilifanyika kituo cha afya Makuburi.

#MaswaliMuhimu:
1. Hao wanaoitwa "Wasamaria wema" waliomuokota Ulomi kwenye ajali na kumkimbiza kituo cha afya Makuburi ni akina nani? Na kwanini wakae kimya? Ina maana hawakuona mitandaoni ndugu wa Ulomi wakihangaika? Kwanini hawakujitokeza waseme "tulimuokota huyu mtu kwenye ajali tukampeleka Mwananyamala?" Au kati yao hakuna mwenye smartphone?

2. Kama kweli Ulomi alipata ajali maeneo ya Ubungo External ilikuaje ndugu wakadai simu yake mara ya mwisho imesoma Chang'ombe (Temeke)? Au yeye alipata ajali lakini simu ikaendelea na safari?

3. Katibu wa Hospitali ya Mwananyamala anasema mwili wa Ulomi ulipokelewa ukiwa hauna utambulisho wowote, kwahiyo waliuhifadhi kama "unknown case". Lakini familia ya Ulomi imemtafuta ndugu yao kwa siku 5 bila mafanikio. Na hapo Mwananyamala walifika pia. Kwanini hawakuowaoneshwa miili ambayo haijatambulika ili waone kama ndugu yao atakuwemo?

4. Je taarifa ya ajali haikutolewa Polisi? Kama ilitolewa, kwanini ndugu wa Ulomi walipoenda kufuatilia Polisi hawakuambiwa kuna ajali ya mtu asiyetambulika, mwili uko Mwananyamala nendeni mkaangalie?

5. Polisi wanadai hawakuweza kumtambua kwa majina maana hakua na kitambulisho chochote. Lakini alikua na pikipiki yenye namba za usajili MC 415 DQC. Kwanini hawakuingiza hizo namba kwenye mfumo wa TIRA ili wapate jina la mmiliki wa pikipiki hiyo?

6. Mbona haielezwi Ulomi alipata ajali na nini? Yani ajali ilihusisha pikipiki yake na kitu gani kingine? Lori? Daladala? Au aligongana na jini? Na kwenye ajali hiyo majeruhi alikua yeye tu?

Nadhani maswali ni mengi kuliko majibu. Kwaheri Ulomi, kama kuna mtu amehusika na kifo chako, Mungu atakulipia. Damu yako haitaenda bure 😭😭😭
 

Mwili wa Mfanyabiashara aliyeripotiwa kupotea tangu December 11,2024 Jijini Dar es salaaam, Daisle Simon Ulomi, umekutwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mwanyamala huku Uongozi wa Hospitali hiyo ukisema Ulomi afikishwa Hospitalini hapo December 11,2024 majira ya jioni akiwa ameshafariki na taarifa zinaonesha alifariki baada ya kupata ajali.

Kupata matukio ya nyuma kuhusu watu wasiyojulikana ingia hapa: Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana

Katibu wa Afya Mwandamizi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwananyamala, Lydia Nzema, ameiambia Ayo “December 11,2024 jioni tulipokea mwili kutoka Zahanati ya Makuburi, akiwa ameshafariki lakini Polisi kesi, ni kesi ya ajali mwili uliopatikana umepata ajali ameshafariki, ina maana alishapata kama ni matibabu au kama Kituo cha Afya alichopelekwa ilikuwa Zahanati ya Makuburi.

"Mwili ulikuwa Unknown hatukujua ni nani na tumehifadhi kwenye chumba cha maiti, leo December 16,2024 wamekuja Ndugu wameutambua mwili na wamesema ni Ndugu yao huyo Mfanyabiashara (Ulomi), kuhusu taarifa zaidi za alipata ajali gani taarifa zitakuwa mochwari zimeandikwa na taarifa zaidi Polisi wanazo.”

Soma Pia:
malisa_gj, ameandika:-
Kwa mujibu wa familia, Ulomi aliondoka nyumbani tar.11 December 2024 akidai kupigiwa simu na watu wa TRA kwenda kufuatilia kontena lake bandarini. Kwa mujibu wa Muliro siku hiyohiyo tar.11 Ulomi alipata ajali ya pilipiki na kukimbizwa kituo cha afya Makuburi (Ubungo External) kisha hospitali ya Mwananyamala. Kwa mujibu wa Katibu wa Hospitali ya Mwananyamala, walipokea mwili wa Ulomi tar.11 kutoka kituo cha afya Makuburi. Maana yake confirmation of death ilifanyika kituo cha afya Makuburi.

#MaswaliMuhimu:
1. Hao wanaoitwa "Wasamaria wema" waliomuokota Ulomi kwenye ajali na kumkimbiza kituo cha afya Makuburi ni akina nani? Na kwanini wakae kimya? Ina maana hawakuona mitandaoni ndugu wa Ulomi wakihangaika? Kwanini hawakujitokeza waseme "tulimuokota huyu mtu kwenye ajali tukampeleka Mwananyamala?" Au kati yao hakuna mwenye smartphone?

2. Kama kweli Ulomi alipata ajali maeneo ya Ubungo External ilikuaje ndugu wakadai simu yake mara ya mwisho imesoma Chang'ombe (Temeke)? Au yeye alipata ajali lakini simu ikaendelea na safari?

3. Katibu wa Hospitali ya Mwananyamala anasema mwili wa Ulomi ulipokelewa ukiwa hauna utambulisho wowote, kwahiyo waliuhifadhi kama "unknown case". Lakini familia ya Ulomi imemtafuta ndugu yao kwa siku 5 bila mafanikio. Na hapo Mwananyamala walifika pia. Kwanini hawakuowaoneshwa miili ambayo haijatambulika ili waone kama ndugu yao atakuwemo?

4. Je taarifa ya ajali haikutolewa Polisi? Kama ilitolewa, kwanini ndugu wa Ulomi walipoenda kufuatilia Polisi hawakuambiwa kuna ajali ya mtu asiyetambulika, mwili uko Mwananyamala nendeni mkaangalie?

5. Polisi wanadai hawakuweza kumtambua kwa majina maana hakua na kitambulisho chochote. Lakini alikua na pikipiki yenye namba za usajili MC 415 DQC. Kwanini hawakuingiza hizo namba kwenye mfumo wa TIRA ili wapate jina la mmiliki wa pikipiki hiyo?

6. Mbona haielezwi Ulomi alipata ajali na nini? Yani ajali ilihusisha pikipiki yake na kitu gani kingine? Lori? Daladala? Au aligongana na jini? Na kwenye ajali hiyo majeruhi alikua yeye tu?

Nadhani maswali ni mengi kuliko majibu. Kwaheri Ulomi, kama kuna mtu amehusika na kifo chako, Mungu atakulipia. Damu yako haitaenda bure 😭😭😭
A Staged Accident. Period.

Dalili zote kabisa zinaonyesha kwamba ajali hiyo ilikuwa ni ya kutengenezwa, it was an Assassination Plot by means of a Staged Road Accident.

Njia zinazopendelewa Sana kutumiwa na Wadhalimu 'Mamluki' katika kutekeleza udhalimu wao ( according to the experience from Russia) ni:-
1. Sumu (Poisoning).
2.A Staged Accidents, most preferably Road/Car crush.
 
A Staged Accident. Period.

Dalili zote kabisa zinaonyesha kwamba ajali hiyo ilikuwa ni ya kutengenezwa, it was an Assassination Plot by means of a Staged Road Accident.

Njia zinazopendelewa Sana kutumiwa na Wadhalimu 'Mamluki' katika kutekeleza udhalimu wao ( according to the experience from Russia) ni:-
1. Sumu (Poisoning).
2.A Staged Accidents, most preferably Road/Car crush.
 
Back
Top Bottom