Katika hili hatujafanikiwa na hatutafanikiwa ku bargain na Mungu.Tumwache tu afanye mambo yake

Katika hili hatujafanikiwa na hatutafanikiwa ku bargain na Mungu.Tumwache tu afanye mambo yake

Guru Master

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2017
Posts
226
Reaction score
594
tunapoishi tunaishi tukijiandaa kwa ajili ya kitu kimoja tu. maandalizi yetu sote yangepaswa yawe kwa ajili ya siku ya kufa. inawezekana mara nyingi kutokana na uzuri wa maisha kwa wengine husahau kuwa kifo kipo.

Kwa nini uogope Kifo?
sioni sababu ya kuogopa kifo.. ni kama unapoanza kusoma shule ni wazi unategemea kuna siku utafanya mtihani. hivyo kuanzia siku ya kwanza unakuwa tayari ukianza kujiandaa kwa ajili ya mtihani. ndivyo ilivyo kwa maisha. maisha haya ni kama tumeazimwa tu.

binadamu tumepewa akili na maarifa angalau tuweze kufikiria namna ya kupunguza vifo visivyo na lazima ila mwishowe vifo hutokea. haijalishi uwe tajiri kiasi gani, uwe na akili kiasi gani, uwezo maskini kiasi gani utakufa.

Je kuna uwezekano ukawa na dhambi duniani ila ukifa uka bargain na Mungu?

HAKUNA.

ukishakufa umekufa. huna uwezo tena wa kwenda ku bargain na Mungu. hata dunia nzima ingefunga na kuomba, hata dunia nzima ingelia na kuomboleza lakini imeandikwa katika
Waebrania 9:27 Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu.

siku unayokata roho tayari unakuwa umeingia hukumuni. na hukumu yako inakuja kwa matendo uliyoishi duniani. si kwa mambo mengine yeyote. ikiwa siku ya mwisho ulitubu dhambi zako ni kheri kwako Mungu wetu husamehe. sababu ni mwingi wa Neema na Rehema. lakini ikiwa ulikufa katika dhambi zako. haijalishi Maaskofu,Mapadre,Wachungaji,Wazee wa Kanisa, Waimba Kwaya Maarufu, Manabii, Mitume na Viongozi wakubwa kiasi gani watahudhuria mazishi yako na kukufanyia maombi.

kufa ni mara moja tu na mara ufapo unaingia hukumuni.

Biblia inajitosheleza. kibinadamu katika imani zetu tuliamua kuchukua mafundisho ya kipagani na kuyaingiza kwenye ukristo. ilhali biblia yenyewe inajitosheleza kwa kila jambo tulilo nalo katika maisha haya. tusi hangaike kubargain na Mungu tunapoondokewa na Mmoja ya mtu tuliye mpenda. tunajua inaumiza sana kupoteza mtu umpendaye na unatamani kwa sababu moja au nyingine kusawazisha na kusuluhisha yale ambayo ulimkosea akiwa hai au sababu ya kujisikia kuhukumiwa moyoni unaamini ukimwombea awekwe mahali pema pengine nawe atakusamehe au utasamehewa na Mungu.

hata dunia nzima ingepaza sauti kuwa huyu awekwe mahali pema. kama hakutenda yanayo mpendeza Mungu haitasaidia. kwa nini ? Mungu ni wa haki. huyu aliyefariki anaombewa na Maaskofu,Wachungaji ,Mapadre na Mwatu wengi.. je akifa maskini ambaye hafahamiani n hao wote itakuwaje? ACHENI KUSEMA R.I.P sababu haisaidii hata kumsogea nusu nchi ya sehemu aliyowekwa kutokana na matendo yake aliyotenda akiwa HAI.

na kuanzia kwenye kifo chake sisi tulio hai tunapaswa kuishi kulingana na maneno ya Mungu. kama marehemu alikuwa na dhambi mpaka anakata roho atawekwa sehemu anayostahili kulingana na maisha yake hapa duniani. hakuna sehemu ambayo roho yake itakaa kwanza kusubiri nguvu ya maombi ya walio hai kabla ya kupelekwa hukumuni.

Waebrania 9:27 Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu.
 
...Haya mambo bwana. Mbona kila nikiomba mahitaji yangu kwa huyo jamaa naona chenga tu. Au kuna ambao wanapewa.
 
Dunia hii inaongozwa na mashetani, wanafanya changizo kwenye masheree lakini mtu akiwa mgonjwa hawatoi msaada lakini akifa, Utawaona na R.I.P zao! unafki mtupu!!!
 
heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa...... maana yake nini? wale waliokufa wakiamini katika Mungu na Kristo Yesu na si kwamba wakifa then ndo waamini maana hakuna kitu kama hicho na ndo hapo tunakumbuka hadithi ya Tajiri na Maskin Lazaro.
nashukuru kwa neno hili pia. ndo maana mtume paulo akasema kuwa kwake yeye kuishi ni kristo na kufa faida .... "
Kwa maana kwangu mimi, kuishi ni Kristo na kufa ni faida. Wafilipi 1:21-25

Ufunuo wa Yohana : Mlango 14

13 Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao.
 
Hivi kwa ni Bwana Yesu alisema, Lazaro hakufa bali amelala?" Wakati wengine wakisema, Mwili wa Lazaro utakuwa unato harufu kwa kuharibika maana ni siku 4 tangu alazwe kaburini.
 
Kwahio mtu akifa tusimuwish peaceful rest?.,utakua msabato tu wewe
 
1. ku mwish kwenu kuna saidia nini? hakusaidii kwa sababu kama ameshapelekwa sehemu ya mateso kutokana na madhambi aliyofanya atabaki huko. haitabilisha kitu. ni kujidanganya tu kusema alazwe mahali pema peponi. ninyi siye mnayemchagulia yeye pa kulazwa. huwa analazwa anapostahili.

2. dhehebu langu sijataja lakini hata ningekuwa msabato si tatizo ikiwa wanafuata maandiko ya biblia kama yalivyo. kukimbizia hoja kwenye dhehebu ni ukosefu wa hoja. ungepinga hoja yangu kwa kutumia biblia ikiwa unaamini biblia. lakini kusema "utakua = utakuwa msabato tu wewe" si jibu la mtu ambaye ni mwelewa. narudia .. dini na dhehebu yangu havihusiani na haya.. BIBLIA INAHUSIKA.

Kwahio mtu akifa tusimuwish peaceful rest?.,utakua msabato tu wewe
 
1. ku mwish kwenu kuna saidia nini? hakusaidii kwa sababu kama ameshapelekwa sehemu ya mateso kutokana na madhambi aliyofanya atabaki huko. haitabilisha kitu. ni kujidanganya tu kusema alazwe mahali pema peponi. ninyi siye mnayemchagulia yeye pa kulazwa. huwa analazwa anapostahili.

2. dhehebu langu sijataja lakini hata ningekuwa msabato si tatizo ikiwa wanafuata maandiko ya biblia kama yalivyo. kukimbizia hoja kwenye dhehebu ni ukosefu wa hoja. ungepinga hoja yangu kwa kutumia biblia ikiwa unaamini biblia. lakini kusema "utakua = utakuwa msabato tu wewe" si jibu la mtu ambaye ni mwelewa. narudia .. dini na dhehebu yangu havihusiani na haya.. BIBLIA INAHUSIKA.
Sehemu ya mateso tena
Mbna biblia inasema wafu wamelala usingizi hawajui lolote
 
mstari gani tuenende kibiblia. unaukumbuka mfano wa Tajiri na Maskini Lazaro?

Luka 16:19-31
Mfano Wa Tajiri Na Maskini Lazaro
19 Akasema, “Palikuwa na tajiri mmoja aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, nguo za gharama kubwa, kila siku. 20 Na maskini mmoja, jina lake Lazaro, mwenye vidonda mwili mzima, alikuwa akiletwa mlangoni kwa huyo tajiri kila siku. 21 Lazaro alikuwa akitamani kula makombo yaliyodondoka mezani kwa tajiri. Hata mbwa walikuwa wakiramba vidonda vyake.

22 “Hatimaye, yule maskini alikufa. Malaika wakamchukua akakae pamoja na Ibrahimu mbinguni. Yule tajiri naye pia akafa, akazikwa.23 Alipokuwa kuzimuni ambapo alikuwa akiteseka, alita zama juu, akamwona Ibrahimu kwa mbali na Lazaro karibu yake. 24 Akaita, ‘Baba Ibrahimu, nionee huruma umtume Lazaro achovye japo ncha ya kidole chake katika maji aupoze ulimi wangu maana ninateseka kwenye moto huu.’ 25 Lakini Ibrahimu akamjibu, ‘Mwa nangu, kumbuka kwamba ulipokuwa hai ulipata kila kitu kizuri uli chotaka, ambapo Lazaro alipokea mabaya. Lakini sasa anafarijika hapa na wewe unateseka. 26 Isitoshe, kati yetu na ninyi huko, kumewekwa bonde kubwa lisilopitika ili wale wanaotaka kutoka huku kuja huko au kutoka huko kuja huku wasiweze.’27 Akasema, ‘Basi, baba, tafadhali umtume Lazaro aende nyumbani kwa baba yangu, 28 awaonye ndugu zangu, wasije wao pia wakaletwa mahali hapa pa mateso watakapokufa.’ 29 Ibrahimu akamjibu, ‘Ndugu zako wanazo sheria za Musa na maandiko ya Manabii. Itawapasa watii hayo.’ Lakini yule tajiri akazidi kumsihi, 30 ‘Hapana baba Ibrahimu, ndugu zangu hawatashawishiwa na hayo. Lakini mtu kutoka kuzimu akitumwa kwao watatubu na kuziacha dhambi zao.’

31 “Ibrahimu akamwambia, ‘Wasiposikiliza na kutii sheria za Musa na Maandiko ya manabii, hawatashawishika kutubu hata kama mtu akifufuka kutoka kuzimu.”’

Sehemu ya mateso tena
Mbna biblia inasema wafu wamelala usingizi hawajui lolote
 
...Haya mambo bwana. Mbona kila nikiomba mahitaji yangu kwa huyo jamaa naona chenga tu. Au kuna ambao wanapewa.
Ushamuita 'jamaa' majamaa wako wengi, toka nje hapo kwako msimamishe jamaa mwombe mahitaji yako,
jamaa ni nani? na kwanini umuombe jamaa?
 
...Haya mambo bwana. Mbona kila nikiomba mahitaji yangu kwa huyo jamaa naona chenga tu. Au kuna ambao wanapewa.
Acha dharau wewe, huyo unayemuita "huyo jamaa ni nani"??? Hivi kweli imefikia mahali BWANA MUNGU unamwita "huyo jamaa" kama vile uwaitavyo wahuni wenzako???

Halafu unategemea akusikilize maombi yako wakati huna hata adabu na heshima kwake? Mkuu Nktlogistics chunga sana kauli zako, chunga sana!
 
Acha kuishi kwa uwoga!
Dunia ni yetu tuitunze kama Bustani kwa furaha na Amani tele!
Sisi ni watoto wake wapenzi
 
Back
Top Bottom