Katika kosa kubwa ambalo Biden atalifanya ni kuhusu uamuzi wa kuiruhusu Ukraine kutumia silaha za masafa marefu

Katika kosa kubwa ambalo Biden atalifanya ni kuhusu uamuzi wa kuiruhusu Ukraine kutumia silaha za masafa marefu

KakaKiiza

JF-Expert Member
Joined
Feb 16, 2010
Posts
11,794
Reaction score
9,075
Biden ameondoa marufuku kwa Ukraine kutumia makombora ya Marekani kushambulia ndani ya Urusi

Joe Biden ameiruhusu Ukraine kushambulia ndani ya Urusi kwa makombora ya masafa marefu ya Marekani.

Rais Biden ameidhinisha Ukraine kutumia silaha za masafa marefu zinazotolewa na Marekani ndani ya Urusi kwa mashambulizi machache, maafisa wa Marekani wamesema.

Ukraine inapanga kufanya mashambulizi yake ya kwanza ya masafa marefu katika siku zijazo, duru zilisema, bila kufichua maelezo kutokana na wasiwasi wa kiusalama.

Hatua hiyo ya Marekani inajiri baada ya miezi kadhaa ya ombi la Volodymyr Zelenskyy kuruhusu jeshi la Ukraine kutumia silaha za Marekani kushambulia maeneo ya kijeshi ya Urusi mbali na mpaka wake.

Mabadiliko hayo yanafuatia Urusi kupeleka wanajeshi wa nchi kavu wa Korea Kaskazini ili kuongeza vikosi vyake, jambo ambalo limezua taharuki mjini Washington na Kyiv.

Mashambulio ya kwanza ya kina huenda yakatekelezwa kwa kutumia roketi za ATACMS, ambazo zina masafa ya hadi maili 190, kulingana na vyanzo.

Kwa Mtazamo wangu nikwamba sasa hii vita inakuja kuwa vita ya ukanda ambayo italeta maafa makubwa sana labda na sema labda kwa rais mpya atakayeingia apige marufuku kuendelea kutumia Siraha za masafa marefu vinginevyo mambo yatakuwa magu sana!

Biden.jpeg
 
Unajua kila siku jaribu kumwangalia mtu anayesema mgombane na jirani yako! je atakusaidaje maana siyo kusema ohooo nitakupa mishale angalia mishale ikoje siyo unaingia kichwa kichwa kumbe mwenziyo level ya mishale alishavuka anamiliki gobole utaumia wewe
 
Biden ameondoa marufuku kwa Ukraine kutumia makombora ya Marekani kushambulia ndani ya Urusi

Joe Biden ameiruhusu Ukraine kushambulia ndani ya Urusi kwa makombora ya masafa marefu ya Marekani.

Rais Biden ameidhinisha Ukraine kutumia silaha za masafa marefu zinazotolewa na Marekani ndani ya Urusi kwa mashambulizi machache, maafisa wa Marekani wamesema.

Ukraine inapanga kufanya mashambulizi yake ya kwanza ya masafa marefu katika siku zijazo, duru zilisema, bila kufichua maelezo kutokana na wasiwasi wa kiusalama.

Hatua hiyo ya Marekani inajiri baada ya miezi kadhaa ya ombi la Volodymyr Zelenskyy kuruhusu jeshi la Ukraine kutumia silaha za Marekani kushambulia maeneo ya kijeshi ya Urusi mbali na mpaka wake.

Mabadiliko hayo yanafuatia Urusi kupeleka wanajeshi wa nchi kavu wa Korea Kaskazini ili kuongeza vikosi vyake, jambo ambalo limezua taharuki mjini Washington na Kyiv.

Mashambulio ya kwanza ya kina huenda yakatekelezwa kwa kutumia roketi za ATACMS, ambazo zina masafa ya hadi maili 190, kulingana na vyanzo.

Kwa Mtazamo wangu nikwamba sasa hii vita inakuja kuwa vita ya ukanda ambayo italeta maafa makubwa sana labda na sema labda kwa rais mpya atakayeingia apige marufuku kuendelea kutumia Siraha za masafa marefu vinginevyo mambo yatakuwa magu sana!!!
Anataka kuhakikisha kuwa mpaka anakabidhi madaraka amemwaribia trump kwa kiasi kikubwa kadri awezavyo.
Bado hujaona hapa mpaka anakabidgi madaraka anataka kuacha kateua hadi majaji..
 
Unajua kila siku jaribu kumwangalia mtu anayesema mgombane na jirani yako! je atakusaidaje maana siyo kusema ohooo nitakupa mishale angalia mishale ikoje siyo unaingia kichwa kichwa kumbe mwenziyo level mishale alishavuka anamiliki gobole utaumia wewe
Fanya mambo yako...kama unayo lakini....
Hao sio level yako...
 
Russia siyo ya kuilinganisha ni hizi nchi zenu Fikiria anapambana na nchi zote za NATO na bado anakiwasha Hivyo kuweni na umakini!Kwa kila jambo siyo ushabiki wa Smba na Yanga!
 
Russia siyo ya kuilinganisha ni hizi nchi zenu Fikiria anapambana na nchi zote za NATO na bado anakiwasha Hivyo kuweni na umakini!Kwa kila jambo siyo ushabiki wa Smba na Yanga!
Inaifahamu vizuri NATO wewe,siku NATO akitia timu hapo Rasia Hana Cha kufanya za ya kulipilua nuke,anaifaha vzr NATO ndo maana huto sikia kaigusa ncho yeyote ya NATO
 
Russia siyo ya kuilinganisha ni hizi nchi zenu Fikiria anapambana na nchi zote za NATO na bado anakiwasha Hivyo kuweni na umakini!Kwa kila jambo siyo ushabiki wa Smba na Yanga!
NATO wanapambana na Rusia wapi?

Kiufupi hii vita ni kama Ukrain kafungwa mikono,
Wanachofanya nato ni kumpa Ukrain silaha kadhaa huku matumizi yake nayo yakiwa ni ya masharti, huku yeye Putin akijipigia tu popote ndani ya Ukrain.

NATO wangeamua kupambana na Putin hiyo vita saa hii ingekuwa ilishaisha
 
NATO wanapambana na Rusia wapi?

Kiufupi hii vita ni kama Ukrain kafungwa mikono,
Wanachofanya nato ni kumpa Ukrain silaha kadhaa huku matumizi yake nayo yakiwa ni ya masharti, huku yeye Putin akijipigia tu popote ndani ya Ukrain.

NATO wangeamua kupambana na Putin hiyo vita saa hii ingekuwa ilishaisha
Ukraine kafungwa mikono nanani Ukraine atengeneze silaha zake uone kama atapangiwa na mtu
 
Back
Top Bottom