Ahaa nimekuelewa kaka, kumbe kuajiriwa ni udhaifu mkubwa sana! Nakubaliana na wewe ni bora umiliki mashine ya kukoboa ukobolee watu kuliko kuwa CEO wa Microsoft au hata Raisi wa nchi maana hizo ni ajira tu.
Kinachotakiwa ni mtu binafsi kuona how much unaingiza kwa siku. No matter umeajiriwa au umejiari, usije kataa kazi kwa mfano ya kulipwa Tsh 50,000/- kwa siku kwa sababu tu unamiliki kibanda cha mama ntilie kinacho kupa Tsh 20, 000/-. Kimsingi uwe unamili kampuni au umeajiriwa zote ni kazi tu (ajira) tofauti iliyopo ni kwamba job description ya upande wa kuajiriwa inasimamiwa na mtu mwingine. Ofcourse kuna mengi ya kufafanua ila all in all ni kwamba kujiajiri kupo na kuajiriwa kupo.
Yeah ni kweli ndiyo maana wanaokoboa mahindi mitaani wana hela kuliko CEO wa Microsoft na Citibank. Pia ni rahisi tu kuwa CEO wa kampuni kama Microsoft hata mtoto wa darasa la kwanza anaweza.Yeah kujiajiri ni faida kubwa sana kwasababu una uwezo wa kuwa na kipato kikubwa kikubwa kuliko hao unaowaona hapo.
Financial freedom ni muhimu sana hasa dunia ya leo inayohitaji akili ya ziada ku-survive.