Sitasahau na nitasimulia wapendwa wangu kuwa Mikoa 3 kama sio 4 chama chetu pendwa kilijipitisha bila kupigwa kwenye local gov election 2019, eti vyama vingine wagombea wote kabisa mkoa mzima walikosea?? Hii dhambi wale wote walioiandaa, walioitekeleza, walioinyamazia na kunufaika na tendo hilo la dhuluma akiwemo Waziri husika, Wakurugenzi wa Halmashauri, Maafisa uchaguzi, Watendaji wa Kata na wengine hata kama wana madaraka makubwa ya kumfanya lolote yeyote na hatuwezi wafanya lolote, liendelee kuwatesa mioyoni mwao ktk kipindi cha uhai wao, wawarithishe na vizazi vyao. Hatuna la kuwafanya lkn Mungu anajua wao na kizazi chao kitakachowapata.
Yaani sijui wanajisikiaje hadi sasa mioyoni mwao. Bahati mbaya ni kundi kubwa sana lililosimamia dhuluma hii na tunao makanisani na misikiti wakiamini hawakutenda kosa lolote. Mbaya zaidi tumetengeneza kundi la watu wanaoamini wizi huu si dhambi na sio kosa bali ni mbinu.