Katoro -Geita kupatiwa Wilaya ya Kipolisi na kujengewa Kituo cha Polisi

Katoro -Geita kupatiwa Wilaya ya Kipolisi na kujengewa Kituo cha Polisi

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760

WhatsApp Image 2024-08-13 at 09.07.32_9bcbcc70.jpg
Serikali imesema itaupatia Mji mdogo wa Katoro Mkoa wa Geita Wilaya ya Kipolisi na kuujengea Kituo kipya cha Polisi chenye hadhi ya Wilaya ili kuimarisha Ulinzi na Usalama wa raia na mali zao.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Daniel Sillo wakati wa ziara ya Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Taifa Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akiwa Mkoani Geita.
WhatsApp Image 2024-08-13 at 09.07.33_ae6bd7c4.jpg
Naibu Waziri Sillo, amesema sababu za kupeleka hitajio hilo ni kutokana na Mji wa Katoro wenye watu zaidi ya laki tatu kukua kibiashara na kiuchumi kwa kasi.

"Kituo cha Polisi kilichopo kipo katikati ya makazi ya watu na maeneo ya biashara habari njema ni kwamba IGP alituma timu yake hapa walishafanya tathimini hivyo mnajengewa Kituo kipya cha kisasa na mnapatiwa Wilaya ya Kipolisi hapa Katoro," alisema.

Aidha, Sillo amewahimiza Polisi kata nchini kuendelea kutoa elimu ya Polisi jamii kwa Wananchi na Viongozi wa Serikali za mitaa kuunda vikundi vya ulinzi shirikishi ili kupambana na kutokomeza uharifu unaojitokeza maeneo mbalimbali ikiwemo wizi wa mifugo unaotajwa kuwepo kwa wingi katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa.

"Wananchi mnapata taarifa za wezi, mnakaa nazo na wengine kuishi nao naomba toeni taarifa kwa Jeshi la Polisi ili sheria ichukue mkondo wake," alisema Sillo.
 
MAJI ya shingo yamenifika mwana mkiwa sisikii Wala sioni la kuambiwa mama kizimkazi Mafi debe mwashambwa AKA mke wa bashite mkumbushe Mama tozo mda wa kampeni bado
 
Hivyo siyo vituo vya polisi ni vituo vya utekaji watu au watu wasiojulikana japo kuwa wanajulikana
 
Back
Top Bottom