Katuni ya MBOWE na Halima MDEE

Katuni ya MBOWE na Halima MDEE

Monica Mgeni

Member
Joined
Oct 7, 2021
Posts
82
Reaction score
134
IMG-20220517-WA0005.jpg
 
Kanuni za Chama

6.5.2 Kwa mujibu wa Ibara 5.4.3 na 5.4.4 ya Katiba, mwanachama yeyote hatachukuliwa hatua za kinidhamu ama kuonywa ama kuachishwa ama kufukuzwa uanachama bila kwanza:
(a) Kujulishwa makosa yake kwa maandishi na kutakiwa kutoa majibu katika muda usiopungua wiki mbili.
(b) (c) (d) Kupewa nafasi ya kujitetea mbele ya kikao kinachohusika.
Mwanachama atajulishwa kwa maandishi uamuzi wa kikao mnamo wiki mbili baada ya kusikilizwa.
Kamati Kuu inaweza kuchukua hatua za dharura bila kuzingatia utaratibu wa kifungu (a) na (b) hapo juu kama itaona maslahi ya Chama kwa ujumla yanaweza kuathiriwa isipokuwa mwachama au kiongozi anayelalamikiwa atalazimika kuitwa kwenye kikao husika.

Hapo tu kuna waliopewa taarifa kwa simu na bila kufafanuliwa makosa yao ili wapate muda wa kutoa utetezi.
Ukiendelea mbele...

6.5.6 Kiongozi yeyote hatachukuliwa hatua za kinidhamu bila kwanza kupewa mashitaka kwa maandishi na mamlaka husika na kupewa nafasi ya kujibu mashitaka kwa maandishi.

6.5.7 Kiongozi mhusika, zaidi ya utetezi wa maandishi, atapewa nafasi ya kujieleza bayana mbele ya kikao cha mamlaka ya nidhamu.

6.5.8 Kiongozi aliyeadhibiwa atapewa taarifa ya misingi ya maamuzi ya mamlaka ya nidhamu ili kumwezesha kuamua kukata rufani au la.

Katika wote hakuna aliyepewa mashitaka kwa maandishi wala nafasi ya kutoa utetezi wala taarifa ya msingi ya mamlaka ya nidhamu. Mpaka hapo mwenendo mzima wa kuwafukuza uanachama ukawa batili.

Ukiwa na swali jingine uliza.
 
Tatizo la wafrika wengi ni pale wanapokuwa wanaandaa hizi katiba kwa malengo yao na ili zije kuwalinda kwa baadae. Shida inakuja pale ambapo zari hilo linapowaangukia wengine. Viongozi wale wale wanaona wivu. Hawa Akina Halima Mdee na wenzake sio wajinga walifafanya hivyo kwa makusudi wakijua hakuna litakalotokea baya kwani wanaijua vizuri katiba yao na mapungufu yake.
Pia hayo hayo ndo yalifanyika kwa Lipumba wa CUF.
Suruhisho ni viongozi kufanyia mambo kwa uwazi na kuweka vitu kwa maslahi ya wote, na sio kujiandalia Kinga kwa wao. Sasa hizo Kinga ndo zimewaangukia Akina mdee. Wamama mmpeupiga mwingi hongereni. Na Kazi iendelee.
 
Mti wenye mizizi ameuegemea Mbowe, Covid 19 wamekalia nyundo isiyo na mizizi. Waingereza wanasema their days are numbered.
 
Back
Top Bottom