Kauli hii inamhusu yupi kati ya mke na HG?


Hebu hebu jipange upya "HUELEWEKI"
 

Kumlea mume kuna maana gani?Kama ni kumpikia,kumfulia,kuhakikish nyumba inakua safi na hata kununua aina ya chakula nyumbani huyo atakua Dada,tofauti na haya ni yapi majukumu ya mke kwa mumewe?
 
Mwanamke kwa maana ya jinsia ya kike aliyekua huwa hafundishwi bali hufundwa

Anayefundishwa ni Msichana tena darasani. Anafundisha Hisabati, maarifa, sayansi kimu, Jografia na ndugu zao..... Ili apate maarifa ya dunia ili atakapokuja kuwa Mwanamke aisaidie jamii wakiwemo wanaume kuleta maendeleo ya familia yake na taifa kwa ujumla.

Baada ya kusema hayo, Nawasalimu wanawake wote wa MMU.
 
Babu,inatakiwa tuanze na wale wanaosema ukimuelimisha "mwanamke"umeelimisha jamii nzima!
 
Kumlea mume kuna maana gani?Kama ni kumpikia,kumfulia,kuhakikish nyumba inakua safi na hata kununua aina ya chakula nyumbani huyo atakua Dada,tofauti na haya ni yapi majukumu ya mke kwa mumewe?

Mbona majukumu ni mengi tu kaka yangu yanayomuhusu mke,
Hivi bila kukaa vizuri na mumeo, kumsikiliza ushauri wake,
kupanga maisha yenu ya baadae, kuratibu mikakati yote ya nyumbani,
bashasha na Mashamsham yanayohitajika kwa mke kumfanyia mume,
hicho chakula kilichopikwa na dada kitalika????????????
huo usafi ndani ya nyumba utaonekana, kwanza baba watoto ndo huyooooo nyumbani hatorudi mapema
.
 
Babu,inatakiwa tuanze na wale wanaosema ukimuelimisha "mwanamke"umeelimisha jamii nzima!
Kiswahili bana.........kigumu kinoma!

Umwelimishe mwanamke.......... Yaani ukamtafute bibi yangu mamshanga uanze kumwelimisha? Unataka kutiwa bakora?
 
Kiswahili bana.........kigumu kinoma!

Umwelimishe mwanamke.......... Yaani ukamtafute bibi yangu mamshanga uanze kumwelimisha? Unataka kutiwa bakora?

Ha ha ha ha umenichekesha hapo kwenye bluu
 
Tausi,hebu niambie majukumu ya mke kwa mumewe halafu tujadili mengine!
 
Kiustaarabu haumuiti "House Girl",...its an insult.
Kibongo bongo unaita "Dada",...ina mpa respect na anafeel as a part of the family.

Back to the topic:No comment

... ile avatar imekuwaje tena??
 

...dahhh,....nimejitahidi sana kujaribu kukuelewa, ila kwa hili Eiyer ni halali yako kuchanganyikiwa...
maana ushaweka na hitimisho mbili zinazokinzana vile vile.
 
kwa kuongezea tu Dena zipo familia nyingi ambazo HG anaendelezwa kielimu kama evening class za 'o' level au veta kujifunza ufundi stadi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…